CCM na siasa za marehemu

CCM na siasa za marehemu

Sio kila mwanasiasa anayetangulia mbele za haki ameuwawa. Ila ile ya Chacha, CHADEMA hawawezi kuikwepa.

Sasa wakati kesi ilipokuwa mahakamani, magamba mlikuwa wapi msipeleke ushahidi? Kisa katiba mpya mmebanwa sasa mnatafuta kisingizio..elewa hata siku moja haki ya mtu haipotei.
 
Hivi mimi na wewe nani mpotoshoji? Jenerali Imran Kombe hakuwahi, hata kwa kukaimu, kuwa Katibu Mkuu wa CCM! Sijui uzushi wako umeutoa wapi? Maneno "CCM imepoteza dira" ni kweli yaliwahi kutamkwa na Katibu Mkuu wa CCM aliyekuwa akiitwa Horace Kolimba na alifariki miezi michache baada ya kuwekwa kiti moto na wenye chama lakini sio kwa kuuwawa na Polisi au kwa risasi.

Kolimba alikufa wakati akihojiwa sio miezi michache baadae!
 
Inasikitisha sana kwa ccm chama kikongwe kutumia mbinu za kishetani kama hizi.
 
Napenda mtu kama huyu anatoa mada na vielelezo sio propaganda za watu wakunuliwa
Imrani Kombe hakuwa Katibu Mkuu bali mkuu wa usalama wa Taifa mstaafu.Kwa huyu naweza kuitetea serikali!!!
 
Mtu anaye engineer siasa hizi ni wa kumulikwa na jamii nzima.
 
hiyo nchi ina laana wengine huku tulipo tunaona hata aibu kujiita watanzania, kwani hakuna jema la kujivunia na kamwe sirudi mpaka ccm watoke madarakani
 
I am sure CHACHA didn't demise in natural way!

Ok fine una uhakika wa hayo uliyosema.mlishindwa nini kuwachukulia hatua wauaji wa Wangwe,ili nyinyi mpumue maana najua wakati ule CDM ilikua imewakalia kooni vibaya hadi kufikia ya kuwataja mafisadi 11 hadharani na Rais mstaafu mmoja na Rais alie madarakani pia.huoni huo ndio ulikua mtaji wa kuisambaratisha CDM?.Je utakubaliana na mimi kuna udhaifu mkubwa wa kiutawala ? kikundi kama CDM kinaweza kuondoa uhai wa Raia mmoja hakuna hatua zinazochukuliwa.Mnawaogopa nini CHADEMA hadi mshindwe kuwashughulikia?Matokeo yake mnakuja na vimbinu vya watoto wa shule ya msingi vya ugaidi wa Rwakatare.Naomba nikuite mkuu kwa sababu ni ustaarabu wa JF.Mtaaminika na nani siku zote mlikua wapi na mauaji ya Wangwe?Ina maana mlitishwa na wauaji hadi mkaogopa kuwakamata?Hii kama sio kijidharirisha ni nini? mtu una mgambo,polisi, magereza,wanausalama na jeshi unatishwa na watu ambao hawana hata Sungusungu tu.MNAJIAIBISHA SANA.
 
Back
Top Bottom