Siku hizi kuna press conference karibia kila siku za mikoa mbalimbali za viongozi wa CHADEMA mikoani kukikimbia chama cha CHADEMA...
Jamani hata kama chama hakipendwi mbona huu utaratibu umenyooka sana na uko so systimastically!? Yaani unaona kabisa ni script za kuandaliwa😂😂😂
Halafu sasa sababu wanazotoa ni full vichekesho.. Yaani CCM imeishiwa... I me hang any I kiss mpaka mambo inayofanya Nata mtoto mdogo anawashangaa na kuwacheka
Hizi script za sasa ni baada ya ile ya G55 kufemea vibaya sana. Haikuchelewa kujulikana kwamba asilimia 95 ni watani zangu wachaga. Hili lilikuwa bonge moja la kosa la kimkakati
Sasa wakaja na plan B ya kurekebisha kosa la kwanza.. Viongozi wa mikoa mbalimbali kuhama chama
Cha kujiuliza ni hiki.
Mbona wanahama viongozi tu bila wanachama wowote!?😂😂😂 halafu wote kwa press conference mahususi? Zinazorushwa na chombo kilekile🤔🤣
CCM maji ya shingo na mfa maji haachi kutapatapa
Mimi nadhani kama kuna chama kinachokufa maji ni chadema wala sio CCM.
Ndani ya siasa hakuna rafiki wa kudumu wala hakuna adui wa kudumu.
Rafiki yako anaweza kuwa adui yako kesho na adui yako anaweza kuwa rafiki yako kesho.
Pia mifumo ya uendeshaji wa siasa ikiwa pamoja na mifumo ya propaganda za kisiasa hukubadilika kulingana na mabadiliko ya nyakati na mazingira.
Mwaka 2015 tulishuhudia mafuriko ya makundi ya watu toka sehemu mbalimbali za TZ waliokuwa waliunga mkono safari ya matumaini ya mzee Lowasa kuanzia ndani ya CCM hadi ndani ya chadema.BILA SHAKA WATU WALIAMINISHWA KUWA MZEE LOWASA KAWAHONGA PESA WAMUUNGE MKONO.
Mwaka mmoja baada ya uchaguzi watu walewale wakaanza mmojammoja wabunge kwa madiwani kuunga mkono juhudi za rais Magufuli.WATU WAKAAMINISHWA TENA KWAMBA MAGUFULI KAWANUNUA WAONDOKE CHADEMA NA KURUDI CCM.
Mwisho wa yote ikawa yuleyule Lowasa waliekuwa nyuma yake na yeye AKARUDI NYUMBANI KUUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS MAGUFULI.
Yanayotokea kwa sasa ndani ya chadema ni matokeo ya kiburi kinachotokana na ulemavu wa MWILI na akili alionao Tundu Lisu!.
Baada ya uchaguzi uliompa nafasi ya kuwa mwenyekiti wa Chadema mwenyekiti mstaafu Freeman Mbowe alimwambia PAUNDWE KAMATI YA KUTIBU MAJERAHA kutokana na yale manenomaneno yaliyopita wakati wa kampeni!
Mwenyekiti Lisu akavimba kichwa kwa kuona kwamba ameshakuwa mwenyekiti kwahiyo hahitaji mtu wa kumfundisha namna ya kufanya kazi!.
Matokeo ya kudharau ushauri wa mtangulizi wake ndio haya yanayotokea sasa na nyinyi mnaanza kuilaumu CCM . Kwa uhakika nyinyi ndio mnaokufa maji kwakuwa nyinyi ndio mnaotapatapa huku na huko.
CCM NI MOJA NA CCM IKO IMARA ZAIDI KULIKO ILIVYOKUWA MIAKA 5 ILIYOPITA.
Pambaneni na hali zenu , na acheni kuiingiza CCM kwenye michezo yenu ya KITOTO.