MLONDWE
Member
- Mar 18, 2013
- 30
- 12
Leo tumechapisha katika gazeti hili habari ya kusikitisha kwamba Waraka wa CCM kwa wanachama wake kushinikiza watetee matakwa ya chama hicho wakati wakitoa maoni yao katika Mabaraza ya Katiba, umezua mtafaruku mkoani Iringa, baada ya Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Said El-Maamry kumzuia mmoja wa wajumbe wa Mabaraza hayo kutumia waraka huo kutoa maoni.
Mjumbe huyo wa Tume alimzuia mmoja wa wajumbe waliokuwa wakichangia maoni kwenye mapendekezo ya Rasimu ya Kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kubaini kwamba alichokuwa akichangia kilitokana na maelekezo ya CCM kama yalivyo katika Waraka uliotokana na kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho iliyokutana mjini Dodoma, Juni 10, mwaka huu.
Tunasema habari hizo ni za kusikitisha kwa sababu mbili kubwa. Kwanza, mjumbe huyo wa Tume alikuwa anatimiza wajibu wake kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa kuhusiana na uendeshaji wa Mabaraza hayo, lakini hatua yake hiyo ilizua tafrani kubwa, kwani baada ya mjumbe huyo wa Baraza la Katiba kutoridhishwa na hatua ya kuzuiwa kutoa maoni kwa kukariri Waraka wa CCM, alishinikiza wajumbe wa mkutano huo wamfukuze Mjumbe huyo wa Tume sio tu kwa kile alichoeleza kwamba anapingana na maelekezo ya Tume ya kuwaacha wananchi watoe mawazo yao kwa uhuru, bali pia kwamba wajumbe wenzake hawakuwa na imani naye.
Pili, habari hizo zinasikitisha kwa sababu chanzo cha mtafaruku huo ni CCM, ambacho ndicho chama tawala kilichounda Serikali iliyo madarakani. Kimsingi, Serikali ya chama hicho ndio iliyoamua nchi yetu ipate Katiba mpya na ilihakikisha sheria husika inatungwa na kupitishwa na Bunge. Hivyo, chama hicho kingetegemewa kiwe mfano bora kwa kuheshimu na kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa katika mchakato mzima wa kupata Katiba mpya.
Hivyo, lilikuwa jambo la kushangaza kuona chama hicho kikitoa Waraka wa kuwaelekeza wanachama wake nini cha kusema na vifungu gani vya Rasimu hiyo wavikubali na vipi wavikatae. Waraka huo wa kurasa 32 hakika unabeba matakwa na masilahi ya viongozi wa chama hicho, mbali na kuwapora wanachama wake haki na uhuru wa kuamua nini kiingizwe katika Katiba mpya na nini kiachwe.
Sasa tunaelewa kwa nini baadhi ya watu wanakuwa kama kasuku wanapotoa mapendekezo na pia kwa nini baadhi yao walitoa rushwa na kutumia udini ili wachaguliwe kuingia katika Mabaraza hayo ya Katiba. Kumbe walitegemea kwamba wingi wa kura za wajumbe wa itikadi moja katika mabaraza hayo ndio ungeamua hatima na mwelekeo wa Katiba mpya.
Vitimbwi tunavyoendelea kushuhudia, kikiwamo hiki cha CCM kuandaa Waraka wa kuwalazimisha wanachama wake kutoa maoni kwa kuzingatia matakwa ya viongozi wake vinatia wasiwasi kama kweli mwishowe itapatikana Katiba iliyoridhiwa na wananchi au Katiba ya viongozi kama zile zilizotangulia.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliagiza na kuonya kwamba wananchi waachwe watoe maoni yao kuhusu Katiba wanayoitaka pasipo kuingiliwa au kushawishiwa na mtu au chombo chochote. Tume pia ilisema wingi wa kura za watu wenye itikadi moja katika Mabaraza hayo hakitakuwa kigezo katika kuandika Katiba mpya. Tunakubaliana na Tume pale inaposisitiza kwamba itazingatia uzito wa hoja na sio wingi wa hoja.
Mjumbe huyo wa Tume alimzuia mmoja wa wajumbe waliokuwa wakichangia maoni kwenye mapendekezo ya Rasimu ya Kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya kubaini kwamba alichokuwa akichangia kilitokana na maelekezo ya CCM kama yalivyo katika Waraka uliotokana na kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho iliyokutana mjini Dodoma, Juni 10, mwaka huu.
Tunasema habari hizo ni za kusikitisha kwa sababu mbili kubwa. Kwanza, mjumbe huyo wa Tume alikuwa anatimiza wajibu wake kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa kuhusiana na uendeshaji wa Mabaraza hayo, lakini hatua yake hiyo ilizua tafrani kubwa, kwani baada ya mjumbe huyo wa Baraza la Katiba kutoridhishwa na hatua ya kuzuiwa kutoa maoni kwa kukariri Waraka wa CCM, alishinikiza wajumbe wa mkutano huo wamfukuze Mjumbe huyo wa Tume sio tu kwa kile alichoeleza kwamba anapingana na maelekezo ya Tume ya kuwaacha wananchi watoe mawazo yao kwa uhuru, bali pia kwamba wajumbe wenzake hawakuwa na imani naye.
Pili, habari hizo zinasikitisha kwa sababu chanzo cha mtafaruku huo ni CCM, ambacho ndicho chama tawala kilichounda Serikali iliyo madarakani. Kimsingi, Serikali ya chama hicho ndio iliyoamua nchi yetu ipate Katiba mpya na ilihakikisha sheria husika inatungwa na kupitishwa na Bunge. Hivyo, chama hicho kingetegemewa kiwe mfano bora kwa kuheshimu na kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa katika mchakato mzima wa kupata Katiba mpya.
Hivyo, lilikuwa jambo la kushangaza kuona chama hicho kikitoa Waraka wa kuwaelekeza wanachama wake nini cha kusema na vifungu gani vya Rasimu hiyo wavikubali na vipi wavikatae. Waraka huo wa kurasa 32 hakika unabeba matakwa na masilahi ya viongozi wa chama hicho, mbali na kuwapora wanachama wake haki na uhuru wa kuamua nini kiingizwe katika Katiba mpya na nini kiachwe.
Sasa tunaelewa kwa nini baadhi ya watu wanakuwa kama kasuku wanapotoa mapendekezo na pia kwa nini baadhi yao walitoa rushwa na kutumia udini ili wachaguliwe kuingia katika Mabaraza hayo ya Katiba. Kumbe walitegemea kwamba wingi wa kura za wajumbe wa itikadi moja katika mabaraza hayo ndio ungeamua hatima na mwelekeo wa Katiba mpya.
Vitimbwi tunavyoendelea kushuhudia, kikiwamo hiki cha CCM kuandaa Waraka wa kuwalazimisha wanachama wake kutoa maoni kwa kuzingatia matakwa ya viongozi wake vinatia wasiwasi kama kweli mwishowe itapatikana Katiba iliyoridhiwa na wananchi au Katiba ya viongozi kama zile zilizotangulia.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliagiza na kuonya kwamba wananchi waachwe watoe maoni yao kuhusu Katiba wanayoitaka pasipo kuingiliwa au kushawishiwa na mtu au chombo chochote. Tume pia ilisema wingi wa kura za watu wenye itikadi moja katika Mabaraza hayo hakitakuwa kigezo katika kuandika Katiba mpya. Tunakubaliana na Tume pale inaposisitiza kwamba itazingatia uzito wa hoja na sio wingi wa hoja.