ccm na maisha ya bata.

Ringo Edmund

JF-Expert Member
May 10, 2010
4,879
1,125
katika viumbe vyote vinavyoishi humu duniani vina tabia moja inayofanana nayo ni kupenda watoto wao haswa ikiwa ni wadogo huwalinda na kuwaongoza ila kuna kiumbe mmoja ananishangaza sana nae ni bata huyu tofauti yake na wazazi wote wa viumbe duniani na binadamu akiwepo ni tabia yake ya kuongozwa na watoto.
bata siku zote husahau kama yupo watoto na anatakiwa kuwaongoza katika njia salama.
siku zote ukikutana na bata na watoto wana safari ujue huo msafara unaongozwa na watoto.

ccm wana mkutano janwani kesho nikitafakari madhumuni ya huo mkutano siyaoni.
maswali ni mengi kuliko majibu.
hivi ccm hawana mpango?
bajeti ya huo mkutano mtaitoa wapi?
agenda zake ni zipi?
je maana ya kuwa madarakani ni nini?

chadema na wapinzani wa kweli wanahaki ya kujijenga na kujitangaza kupitia najukwaa ya siasa ili ilani yao ieleweke 2015 wangekuwa madarakani tungewahukumu kupitia ilani na jinsi walivyoitekeleza.
 
Back
Top Bottom