CCM na demokrasia ya Shangazi Mwajuma

CCM na demokrasia ya Shangazi Mwajuma

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,006
Mimi, nilipokuwa mtoto mdogo kule Songea Ruvuma, nililelewa na shangazi yangu aliyeitwa Mwajuma. Shangazi Mwajuma alikuwa na demokrasia fulanifulani ya kiini macho. Wakati ule sikuwa na uelewa wa kutosha kuhusu demokrasia yake. Ya kwake haikuhusisha kupigwa kwa kura. Yake ilikuwa demokrasia ya kukisia na kependelea. Ilikuwa ya kulenga kupendelea mtoto fulani.

Kulenga mshindi au mfaidika hata kabla ya kutekelezwa kwa jambo. Hasa wakati wa kula. Kwa shangazi Mwajuma tulikuwa watoto watatu. Wawili wa kwake na mimi. Mimi nilikuwa wa katikati kiumri. Wote tulikuwa wavulana. Mkubwa kabisa na mdogo kabisa walikuwa wa kwake. Basi, Shangazi Mwajuma alikuwa akiwapendelea watoto wake kwa umahiri na kupokezana.

Mimi nilibaki kushangaa na kupitwa na demokrasia-kandamizi hiyo. Demokrasia iliyokuwa-kama hii ya CCM-ya kiini macho. Siwezi kumsahau Shangazi Mwajuma. Kuna siku, kukiwa na nyama, anadai kuwa mtoto wa kwanza achukue anazotaka kutoka kwenye bakuli ili kuonesha kuwa yeye ndye mkubwa wetu. Siku nyingine nafasi ya upendeleo hupewa mtoto wa mwisho (kiziwanda/kitindamimba). Kwa namna hiyo hiyo.

Ukubwani ndiyo nayaona yale ya Shangazi Mwajuma kupitia CCM. CCM imejaa demokrasia bandia na ya karata-tatu. Mlengwa hujitokeza tangu mwanzo hata kama hubezwabezwa. Kitendo cha leo cha wagombea wawili wa Uspika (Dr. Tulia Ackson na Bwana Abdullah Mwinyi) kujitoa na kumuacha pekee Bwana Job Yustino Ndugai kuwa mgombea wa Uspika kimenikumbusha Shangazi Mwajuma na demokrasia bandia yake.

Kulikuwa na haja gani wengine kuchukua fomu na hata kupitishwa na CC na NEC? Wabunge wa CCM wana nafasi gani tena kumchagua mgombea wa Uspika ikiwa mgombea amechaguliwa na Kamati Kuu ambayo ndiyo iliyochuja na kuacha majina matatu mwanzoni. CCM inacopy na kupaste demokrasia ya Shangazi Mwajuma!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
 
Leo mzee tupatupa umenikumbusha mbali kwani mimi nililelewa na mama wa kambo hiyo ya kwako ilikuwa cha mtoto. Ila nilichokigundua kwetu sisi waafrka na hasa pengine Watanzania tunaongozwa na hila na unafiki wa hali ya juu, sio msomi wala ngumbaro. Unaweza kukuta mtu ni msomi lakini full kujikombakomba na wakati mwingine anajikomba hata kwa aliyemzidi kwa elimu kisa tu anamzidi cheo. Basi kutii amri ya mkubwa wako sio tatizo lakini mpaka ya kijinga kweli kisa upate ulaji!! Hiyo demokrasia ya kiini macho ndio leo wazungu wanatung'ong'a eti kura toka Znz za kumpitisha Magufuli ni halali lakini huko ZnZ uchaguzi uliharibika!! Na hicho unachokiona hapo bungeni kumteua spika na naibu ni muendelezo huohuo wa ujinga wetu waafrika na hasa watanzania.
 
Ccm inapaswa iige demokrasia kama waliyonayo chadema
 
hahahaaa,,,,hivi ile proposal ya dual citizenship ilikufa
 
Kwa mambo yanayoendelea wenye macho ndio wanaona rangi halisi za ccm. Kudhalilisha wagombea ni kawaida yao
 
Mimi, nilipokuwa mtoto mdogo kule Songea Ruvuma, nililelewa na shangazi yangu aliyeitwa Mwajuma. Shangazi Mwajuma alikuwa na demokrasia fulanifulani ya kiini macho. Wakati ule sikuwa na uelewa wa kutosha kuhusu demokrasia yake. Ya kwake haikuhusisha kupigwa kwa kura. Yake ilikuwa demokrasia ya kukisia na kependelea. Ilikuwa ya kulenga kupendelea mtoto fulani.

Kulenga mshindi au mfaidika hata kabla ya kutekelezwa kwa jambo. Hasa wakati wa kula. Kwa shangazi Mwajuma tulikuwa watoto watatu. Wawili wa kwake na mimi. Mimi nilikuwa wa katikati kiumri. Wote tulikuwa wavulana. Mkubwa kabisa na mdogo kabisa walikuwa wa kwake. Basi, Shangazi Mwajuma alikuwa akiwapendelea watoto wake kwa umahiri na kupokezana.

Mimi nilibaki kushangaa na kupitwa na demokrasia-kandamizi hiyo. Demokrasia iliyokuwa-kama hii ya CCM-ya kiini macho. Siwezi kumsahau Shangazi Mwajuma. Kuna siku, kukiwa na nyama, anadai kuwa mtoto wa kwanza achukue anazotaka kutoka kwenye bakuli ili kuonesha kuwa yeye ndye mkubwa wetu. Siku nyingine nafasi ya upendeleo hupewa mtoto wa mwisho (kiziwanda/kitendamimba). Kwa namna hiyo hiiyo.

Ukubwani ndiyo nayaona yale ya Shangazi Mwajuma kupitia CCM. CCM imejaa demokrasia bandia na ya karata-tatu. Mlengwa hujitokeza tangu mwanzo hata kama hubezwabezwa. Kitendo cha leo cha wagombea wawili wa Uspika (Dr. Tulia Ackson na Bwana Abdullah Mwinyi) kujitoa na kumuacha pekee Bwana Job Yustino Ndugai kuwa mgombea wa Uspika kimenikumbusha Shangazi Mwajuma na demokrasia bandia yake.

Kulikuwa na haja gani wengine kuchukua fomu na hata kupitishwa na CC na NEC? Wabunge wa CCM wana nafasi gani tena kumchagua mgombea wa Uspika ikiwa mgombea amechaguliwa na Kamati Kuu ambayo ndiyo iliyochuja na kuacha majina matatu mwanzoni. CCM inacopy na kupaste demokrasia ya Shangazi Mwajuma!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)

Yale yale ya Urais wallah tuombeane heri tu lakini hakuna dhambi mbaya duniani kama ya ubaguzi na unafiki na hii ni sumu inawatafuna mdogomdogo.
 
Wamewanyima nafasi makusudi watu wenye nia zaidi ya tisa kwa kuwapitisha watu walienda kujitoa baadae.

Wako sawa lakini wa viwango vya chama hiki tawala.
 
baada ya kuona Dr Tulia atamwagwa chini kwa aibu, ikabidi wote wawili wajifanye wanamuunga mkono Ndugai ili kwenye unaibu spika wabunge wa ccm wamwonee hurumaa wampe kura, sasa cheki JK atakavyobaki midomo wazi, Hapo ndipo utagundua Zimwi likijualo halikuli likakwisha, Lowassa anaijua ccm mpk kwenye utumbo.

Safari ndo inaanza
 
Yale yale ya Urais wallah tuombeane heri tu lakini hakuna dhambi mbaya duniani kama ya ubaguzi na unafiki na hii ni sumu inawatafuna mdogomdogo.

Wanalenga kumkomoa zungu wakati kapambana jimboni,kweli hii demokrasia ya shangazi mwajuma
 
Watu wanatembea na ndizi, pilipili mfukoni longtime walishajua pale kuna ubwabwa leo
 
Demoracia tanzania na ccm imeshatushinda, kinachofanyika ni twende twende tu bora tufike
 
Ila nimeipenda hii stork,shangazi mwajuma,it is the best kwa mwezi huu
 
Kinachonichekesha ni pale unaambiwa kura za wawakilishi zanzibar ni halali, kura za raisi wa jamhuri wa muungano ni halali, kura za seif na shein sio halali wakati ni mtu yule yule aliyepiga hizo kura kwa wakati mmoja, mimi najiuliza kwa nini tusiache haya mambo ya democracia, hii ni aibu , tunaonekana taifa zima hatuko sawa na hatujielewi.
 
Leo mzee tupatupa umenikumbusha mbali kwani mimi nililelewa na mama wa kambo hiyo ya kwako ilikuwa cha mtoto. Ila nilichokigundua kwetu sisi waafrka na hasa pengine Watanzania tunaongozwa na hila na unafiki wa hali ya juu, sio msomi wala ngumbaro. Unaweza kukuta mtu ni msomi lakini full kujikombakomba na wakati mwingine anajikomba hata kwa aliyemzidi kwa elimu kisa tu anamzidi cheo. Basi kutii amri ya mkubwa wako sio tatizo lakini mpaka ya kijinga kweli kisa upate ulaji!! Hiyo demokrasia ya kiini macho ndio leo wazungu wanatung'ong'a eti kura toka Znz za kumpitisha Magufuli ni halali lakini huko ZnZ uchaguzi uliharibika!! Na hicho unachokiona hapo bungeni kumteua spika na naibu ni muendelezo huohuo wa ujinga wetu waafrika na hasa watanzania.

ndugu yangu,mtu akifikia kiwango cha juu cha ubinafsi,elimu yake na akili yake huenda likizo.
 
Nacho jiuliza humu ndani jf, lin wana CDM mtaamin kuwa mnakurupuka? ``Kazi Tu'' imewashida sasa mnawaaminsha watu kuwa cdm kuna demokrasia?? Kweli nyani haoni kundule
 
Na nimeona Nnauye anaweweseka kwa hofu ya baadhi ya wana ccm kutompigia kura Job Ndugai, si umesikia akisema "sina shaka kuwa wabunge wa ccm watampa kura Ndugai"
 
Back
Top Bottom