Wadau leo ninapenda niliweke hili suala uwanjani kwa kuwa naamini humu kuna wana CCM, wana Chadema, nk. Kwa ujumla ccm ni zao la TANU na ASP na kwa mantiki hiyo tokea mwaka 1961 ccm iko madarakani. Ni kuanzia huo mwaka walichukua majukumu ya kusimamia maendeleo ya nchi kama vile kujenga Barabara, reli, kuwekeza kwenye umeme,Huduma za usafirishaji( majini ,nchi kavu na angani). Pia ilipewa majukumu ya kusimamia uwepo na ubora wa Huduma za kijamii kama vile Huduma za Afya, elimu na upatikanaji wa Maji.
Jambo la kushangaza kila mwaka wa uchaguzi Hiki chama cha CCM kinakuja na ajenda zilezile kuwa wachaguliwe wajenge miundombinu, barabara , reli , hospitali,shule, nk. Hata mwaka 2015 walikuja na hizo ajenda na mwaka huu hakuna kilichobadirika katika ahadi zao kwa wapiga kura. Sasa jambo la kujiuliza je hawa CCM ni kweli kuna uwezekano wa kupata suluhu ya changamoto ambazo kwa miaka 60 wameshindwa kuzitatua?
Je CCM mmekosa ahadi nyingine kiasi kwamba kila mwaka wa uchaguzi mnarudi na hizo ahadi kana kwamba hamkuwa kwenye madaraka? Je hamuoni ni muda sahihi wa kukaa pembeni kupisha mawazo na njia mbadala wa kutatua kero za wananchi? Please njooni na hoja na siyo vioja, karibuni.
Jambo la kushangaza kila mwaka wa uchaguzi Hiki chama cha CCM kinakuja na ajenda zilezile kuwa wachaguliwe wajenge miundombinu, barabara , reli , hospitali,shule, nk. Hata mwaka 2015 walikuja na hizo ajenda na mwaka huu hakuna kilichobadirika katika ahadi zao kwa wapiga kura. Sasa jambo la kujiuliza je hawa CCM ni kweli kuna uwezekano wa kupata suluhu ya changamoto ambazo kwa miaka 60 wameshindwa kuzitatua?
Je CCM mmekosa ahadi nyingine kiasi kwamba kila mwaka wa uchaguzi mnarudi na hizo ahadi kana kwamba hamkuwa kwenye madaraka? Je hamuoni ni muda sahihi wa kukaa pembeni kupisha mawazo na njia mbadala wa kutatua kero za wananchi? Please njooni na hoja na siyo vioja, karibuni.