CCM kwenu hoja ni nini?

CCM kwenu hoja ni nini?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,176
Reaction score
48,460
Leo nataka kujifunza toka kwa wana CCM waliomo JF kwamba wanaposema kwamba wapinzani hawana hoja kwenye jambo fulani huwa wanamaanisha nini hasa? Huwa wanamaanisha hoja ni kuunga mkono ama kupongeza kila kitu kinachofanywa na viongozi wa CCM ama huwa wanamaanisha nini?

Nilishawahi kuuliza kwa misamiati ya siasa za CCM "sera" inamaanisha nini mpaka leo sijapatiwa jibu. Utawasikia wakisema wapinzani hawana sera, sasa ukiwauliza sera ndiyo nini wananuna. Sasa hivi sasa wameibuka na huu msamiati mpya wa "Hoja" kwamba wapinzani hawana hoja ama wameishiwa hoja.

CCM mkituambia kwa mtazamo wenu "hoja" ni nini labda itatusaidia kufanya mijadala yenye tija na nyie. Kama wapinzani hawana hoja itatusaidia kupima kama na CCM nao wana hoja. CCM wa JF tuambieni ili iwe hoja inatakiwa iwe na sifa na vigezo gani!?
 
Kwa uzi huu poa zao hazitaonekana wajumbe ndio wa Lumumba. Akili zao zipo likizo kwao ni ndio kwa kila limtokalo kinywani mfalme juha et al. Bora matumbo yao yamevimbiwa baasi.
 
Huwa wanasubiri neno kisha wanalibeba kama kasuku na kuishia kuliimba hapa jukwaani. Sasa hivi pia utawasikia wakisema cdm humu jukwaani wanaporomosha matusi, ukiwauliza mbona sheria za jukwaa zinakataza matusi inakuwaje wao waone michango ya wengine ni matusi na hakuna ban? unakuta hawana majibu. Nikuhakikishie hakuna anayejua sera ni nini wala hoja ni nini. Wenyewe wanajua hoja ni kukubali kila anachosema magu na serekali.
 
tindo unawachokoza binamu zako hivyo, watakujia na matarumbeta kama kina mama wa Dar es salaam!
 
HOJA NI KUSEMA ANATEKELEZA ILANI YETU, WAKATI HUOHUO MTU HUYOHUYO ANASEMA HAKUNA ANACHOKIFANYA
 
HOJA NI KUSEMA ANATEKELEZA ILANI YETU, WAKATI HUOHUO MTU HUYOHUYO ANASEMA HAKUNA ANACHOKIFANYA
Karibu Kada kwenye mjadala. Kwa ivo kwa ufupisho hoja ni ukigeugeu kama vile ule wa kusema kwamba hela za Tegeta Escrow si za Umma halafu badaye tena mnashangilia wanapokamatwa Rugemalira na Seth?
 
Back
Top Bottom