Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,838
- 50,542
Kuna propaganda inaenezwa na CCM kwamba ndani ya CHADEMA ukipingana na Mwenyekiti taifa wa chama hicho, basi ni lazima uuawe. Mbowe ana madhaifu yake kama binadamu mwingine yeyote yule, lakini hili la kusingizia kuua wapinzani wake limevuka Mpaka.
Alipokufa Chacha Wangwe kwa ajali kule Kibaigwa, tuliona jinsi CCM walivyotengeneza hisia miongoni mwa watanzania kwamba Wangwe kauawa na Mbowe kwa kuwa eti alikuwa anataka kugombea uenyekiti wa CHADEMA taifa.
Siku ya mazishi ya Wangwe kule Tarime kulikuwa na tafrani iliyofadhiliwa na CCM kiasi kwamba ilionekana kama vile Mbowe angeshambuliwa. Baada ya mazishi ya Wangwe, uchaguzi ukarudiwa na Charles Mwera wa CHADEMA akashinda na wananchi wa Tarime wakakataa Propaganda ya CCM kwamba Mbowe ndiyo alihusika kumuua Wangwe.
Ben Saanane Mwanachadema ambaye alikuwa anaibukia kwenye mijadala ya mitandaoni, akiwa ni kilongola kijana kwenye kuukosoa utawala wa Rais John Magufuli, alipotea ghafla na mpaka leo hajulikani alipo. Mara hii tena CCM wakaleta propaganda kwamba aulizwe Mbowe wapi alipo Saanane!
Juzi msemaji wa serikali (kama Akaunti iliyotumika ni ya kwake) mara tu baada ya Mbowe kuishutumu serika kuwa ni mshukiwa namba moja wa mashambulizi dhidi ya Lissu, msemaji huyo wa Serikali aliandika maneno kwamba inawezekana Mbowe naye ndiye mshukiwa namba moja.
Lakini CCM ndiyo inatowa mawaziri na ndiyo yenye rais anayeongoza nchi. Shutuma kwamba Mbowe anaua wanachadema wanaopingana naye ni ya kijinga ingawa inafikirikisha sana. Kama CCM ndiyo wenye dola kwa sasa wanashindwaje kutumia dola kukusanya ushahidi wa kutosha ili kumtia hatiani Mbowe?
Kama leo wanasisitiza kwamba mwenye ushahidi kuhusu Lissu kushambuliwa aupeleke Polisi ni kwa nini wao CCM hawapeleki ushahidi polisi kuthibitisha kwamba Mbowe huwa anaua wapinzani zake ndani ya CHADEMA?
Waziri wa sheria ni CCM, Waziri wa mambo ya ndani ya nchi ni CCM, Waziri wa Ulinzi na jeshi la kujenga taifa ni CCM, waziri anayesisimamia Idara ya Usalama wa Taifa ni CCM na Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya Tanzania ni CCM. Kwa nini CCM isitumie fursa hiyo kumuadabisha Mbowe?
Kwa nini CCM inamlea Mbowe pamoja na kujua uovu wake wote wa "kuua" wapinzani zake ndani ya CHADEMA?
Alipokufa Chacha Wangwe kwa ajali kule Kibaigwa, tuliona jinsi CCM walivyotengeneza hisia miongoni mwa watanzania kwamba Wangwe kauawa na Mbowe kwa kuwa eti alikuwa anataka kugombea uenyekiti wa CHADEMA taifa.
Siku ya mazishi ya Wangwe kule Tarime kulikuwa na tafrani iliyofadhiliwa na CCM kiasi kwamba ilionekana kama vile Mbowe angeshambuliwa. Baada ya mazishi ya Wangwe, uchaguzi ukarudiwa na Charles Mwera wa CHADEMA akashinda na wananchi wa Tarime wakakataa Propaganda ya CCM kwamba Mbowe ndiyo alihusika kumuua Wangwe.
Ben Saanane Mwanachadema ambaye alikuwa anaibukia kwenye mijadala ya mitandaoni, akiwa ni kilongola kijana kwenye kuukosoa utawala wa Rais John Magufuli, alipotea ghafla na mpaka leo hajulikani alipo. Mara hii tena CCM wakaleta propaganda kwamba aulizwe Mbowe wapi alipo Saanane!
Juzi msemaji wa serikali (kama Akaunti iliyotumika ni ya kwake) mara tu baada ya Mbowe kuishutumu serika kuwa ni mshukiwa namba moja wa mashambulizi dhidi ya Lissu, msemaji huyo wa Serikali aliandika maneno kwamba inawezekana Mbowe naye ndiye mshukiwa namba moja.
Lakini CCM ndiyo inatowa mawaziri na ndiyo yenye rais anayeongoza nchi. Shutuma kwamba Mbowe anaua wanachadema wanaopingana naye ni ya kijinga ingawa inafikirikisha sana. Kama CCM ndiyo wenye dola kwa sasa wanashindwaje kutumia dola kukusanya ushahidi wa kutosha ili kumtia hatiani Mbowe?
Kama leo wanasisitiza kwamba mwenye ushahidi kuhusu Lissu kushambuliwa aupeleke Polisi ni kwa nini wao CCM hawapeleki ushahidi polisi kuthibitisha kwamba Mbowe huwa anaua wapinzani zake ndani ya CHADEMA?
Waziri wa sheria ni CCM, Waziri wa mambo ya ndani ya nchi ni CCM, Waziri wa Ulinzi na jeshi la kujenga taifa ni CCM, waziri anayesisimamia Idara ya Usalama wa Taifa ni CCM na Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya Tanzania ni CCM. Kwa nini CCM isitumie fursa hiyo kumuadabisha Mbowe?
Kwa nini CCM inamlea Mbowe pamoja na kujua uovu wake wote wa "kuua" wapinzani zake ndani ya CHADEMA?