jmushi1
Platinum Member
- Nov 2, 2007
- 26,375
- 25,455
Wanajamvi, kwanza nianze na definition hii hapa chini.
“Single-party dictatorships are regimes in which one party dominates politics. In single-party dictatorships, a single party has access to political posts and control over policy.”
Kwasababu nchi yetu ni ya kidemokrasia, na inayotakiwa kufuata multiparty system (kikatiba), kuzuia shughuli za vyama hivyo ni uvunjaji wa katiba. Ni uvunjaji wa katiba wenye sifa kuu za udikteta.
Tokea tukubaliane na mfumo wa kidemokrasia wa vyama vingi, hatujawahi kupata chama tofauti na CCM. Ambao matatizo yote ya Taifa hili wao ndiyo wako responsible.
Hatujawahi kupata viongozi wa chama tofauti, kwasababu pia kuna party dictatorship, ambayo inasimamiwa na party leader ili kukwamisha maendeleo ya demokrasia. Hapo udikteta wa chama unasimamiwa na viongozi wa serikali na makada wa chama.
Mfano rais ambaye ni mwenyekiti wa chama, anapotumia madaraka yake kukiuka katiba ya kidemokrasia na kushinda uchaguzi kwa kupitia mabao ya mikono, ukandamizaji wa vyama pinzani, kuminya uhuru wao wa kikatiba, kuwatisha, kuwateka, kuwaua nk.
Kama tunasema tuna demokrasia, halafu tuna katiba ambayo kuna mwananchi yoyote anaweza akawa juu yake, hilo tatizo kubwa mno na matokeo yake ndo haya ya party dictatorship!
Kwenye demokrasia ya kweli, no one is above the law na kwasababu mwenyekiti wa CCM amekuwa above the law miaka yote toka tupate uhuru, na hata baada ya mabadiliko ya katiba kuingiza demokrasia ya vyama vingi, bado Mwenyekiti wa CCM yuko above the law. Na nyakati nyingine wanachama wa CCM wako above the law. Hata Mwenyekiti wao ambaye ndiye dikteta mkuu, aliwahi kusema “hao wa kijani wasiguswe”
Sasa kwa ujinga wetu, eti CCM wanataka kutupa lecture kuhusu demokrasia?! Huwa nashagazwa sana na akili zetu sisi Watanzania! Ama ni haki yetu kufanyiwa haya yote? Maana naona watu ni kama hawajitambui kwa kiasi kikubwa, na ndiyo maana tumefika hapa tulipo.
Na huyu Rais wa sasa ndo amefumbuwa wengi macho hadi katiba mpya inaanza kudaiwa kidogo. Lakini bado kabisa inapokuja kwenye mwamko. Halafu pia upinzani umenishangaza sana kwa kuendelea kushiriki viini macho! Sijui ni idadi kidogo ya wabunge waliopatikana?
Kwa maoni yangu, hata hao wabunge waliopatikana, ni CCM tu iliamua kuwaachia ili kuuficha udikteta wao! Maana huyu mwenyekiti wao wa sasa si anatumia madaraka yale yale ambayo ni “above the law”?
“Single-party dictatorships are regimes in which one party dominates politics. In single-party dictatorships, a single party has access to political posts and control over policy.”
Kwasababu nchi yetu ni ya kidemokrasia, na inayotakiwa kufuata multiparty system (kikatiba), kuzuia shughuli za vyama hivyo ni uvunjaji wa katiba. Ni uvunjaji wa katiba wenye sifa kuu za udikteta.
Tokea tukubaliane na mfumo wa kidemokrasia wa vyama vingi, hatujawahi kupata chama tofauti na CCM. Ambao matatizo yote ya Taifa hili wao ndiyo wako responsible.
Hatujawahi kupata viongozi wa chama tofauti, kwasababu pia kuna party dictatorship, ambayo inasimamiwa na party leader ili kukwamisha maendeleo ya demokrasia. Hapo udikteta wa chama unasimamiwa na viongozi wa serikali na makada wa chama.
Mfano rais ambaye ni mwenyekiti wa chama, anapotumia madaraka yake kukiuka katiba ya kidemokrasia na kushinda uchaguzi kwa kupitia mabao ya mikono, ukandamizaji wa vyama pinzani, kuminya uhuru wao wa kikatiba, kuwatisha, kuwateka, kuwaua nk.
Kama tunasema tuna demokrasia, halafu tuna katiba ambayo kuna mwananchi yoyote anaweza akawa juu yake, hilo tatizo kubwa mno na matokeo yake ndo haya ya party dictatorship!
Kwenye demokrasia ya kweli, no one is above the law na kwasababu mwenyekiti wa CCM amekuwa above the law miaka yote toka tupate uhuru, na hata baada ya mabadiliko ya katiba kuingiza demokrasia ya vyama vingi, bado Mwenyekiti wa CCM yuko above the law. Na nyakati nyingine wanachama wa CCM wako above the law. Hata Mwenyekiti wao ambaye ndiye dikteta mkuu, aliwahi kusema “hao wa kijani wasiguswe”
Sasa kwa ujinga wetu, eti CCM wanataka kutupa lecture kuhusu demokrasia?! Huwa nashagazwa sana na akili zetu sisi Watanzania! Ama ni haki yetu kufanyiwa haya yote? Maana naona watu ni kama hawajitambui kwa kiasi kikubwa, na ndiyo maana tumefika hapa tulipo.
Na huyu Rais wa sasa ndo amefumbuwa wengi macho hadi katiba mpya inaanza kudaiwa kidogo. Lakini bado kabisa inapokuja kwenye mwamko. Halafu pia upinzani umenishangaza sana kwa kuendelea kushiriki viini macho! Sijui ni idadi kidogo ya wabunge waliopatikana?
Kwa maoni yangu, hata hao wabunge waliopatikana, ni CCM tu iliamua kuwaachia ili kuuficha udikteta wao! Maana huyu mwenyekiti wao wa sasa si anatumia madaraka yale yale ambayo ni “above the law”?