CCM kumekucha: Raila Odinga sasa amponza Magufuli!

CCM kumekucha: Raila Odinga sasa amponza Magufuli!

Huenda magufuli alifanyiwa ukarimu wa hali ya juu kiasi cha kuchanganyikiwa na kuropoka bila kufikiri. Nafikiri baada ya ukarimu ule kupita sasa atakuwa anajutia maneno yake baada ya kutafakari. Kwa kweli kauli kama hii inaweza hata kuhatarisha jumuiya ya Afrika Mashariki, sababu itaonekana kama kuna baadhi ya nchi zinaingilia mambo ya ndani ya nchi zingine.
Wewe ni hamnazo na hizi ndo huwa tunaziita nidhamu za uoga..! Magufuli hakuiwakilisha Tanzania katika hili..! ..! The guy is real bright na kamwe hakurupuki kama wewe, kama hauamini waulize wana wa Kigamboni walipomwambia awaombe radhi juu ya kauli yake nzuri kwamba wapinge mbizi kama hawezi kulipia nauli mpya..!
 
Mkuu, hiyo ndiyo Hali halisi na inawezekana huo ndio msimamo Wa serikali na chama tawala cha CCM.

Ameyasema in black and white. Hatuna haja ya kumtaka uthibitisho wala ufafanuzi. kilichopo Kama si msimamo Wa serikali Au chama chake basi wasemaji wa hizi taasisi inabidi Watuambie
 
siwezi kushangaa kwa kauli kama hiyo magufuli ni mlopokaji kwani Igunga alifanya nini! amesahau kule kwake alipita kwenye tundu la sindano
 
Ametoa maneno ya ku msupport odinga kama Magufuli, au Selikari? Upepo tu utapita
 
Wewe ni hamnazo na hizi ndo huwa tunaziita nidhamu za uoga..! Magufuli hakuiwakilisha Tanzania katika hili..! ..! The guy is real bright na kamwe hakurupuki kama wewe, kama hauamini waulize wana wa Kigamboni walipomwambia awaombe radhi juu ya kauli yake nzuri kwamba wapinge mbizi kama hawezi kulipia nauli mpya..!
Magufuli ametokota hata kama ukimtetea vipi. Tatizo la magamba huwa kasoro zenu hamzioni na ndio maana hata rushwa mnailea maana mnaona ni sawa tu na haina shida. Sasa kama rushwa na wizi wa mali ya umma mnaona ni sawa, itakuwaje kuropoka?
 
Who says it? Where he says it? What he says? As who? Muhimu sana maswali haya
 
mkuu wataalamu wa sheria za kikanda na kimataifa itabidi watueleze hali km hii inakuwaje.
je katiba ya kenya inaruhusu mgombea kupigiwa debe na foreigner?

sheria zetu je zinaruhusu citizen wa tz kwenda kumpigia kampeni mgombea wa nchi nyingine? inawezekana magufuli akawa ameweka precedent ktk shauri hili. tijadili.
Hapo kwenye red ... ni akina nani hao??????!!!!!
 
Magufuli ametokota hata kama ukimtetea vipi. Tatizo la magamba huwa kasoro zenu hamzioni na ndio maana hata rushwa mnailea maana mnaona ni sawa tu na haina shida. Sasa kama rushwa na wizi wa mali ya umma mnaona ni sawa, itakuwaje kuropoka?
You are missing a point, tunazungumzia kauli ya Magufuli ghafla unakuja na issue za kulea ufisadi. Mbona sijawahi kusupport ulezi wa ufisadi kutoka kwa ccm? Haya ndo madhara ya kukurupuka, poor you.
 
Acheni uvivu wa kufikiri na siasa za chini ya vitanda, magufuli ameongea Kama rafiki wa raila na hajaongea kwa niaba ya CCM au serikali , mnalikuza jambo hili kwa maslahi ya ovyo ovyo tu, gazeti la raia mwema siku hizi nalo linaandika udaku tu.Magufuli na raila ni marafiki hata nje ya uwaziri wao Ana haki Kama raia yeyote kummunga mkono raila kwa uwazi bila kificho Kama alivyofanya.Nashangaa Huyu wenje ambaye hata mwanza wamemchoka anakurupuka kutoa matamko yasiokuwa na msingi, acheni watu wafanye siasa za maana sio kuongea usikike kuwa wewe ni msemaji au wa waziri kivuli wa mambo ya Nje.
PhD hili si jambo la urafiki tu hata kidogo. Tunamwongelea Waziri na Mbunge wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kumpigia kampeni mgombea katika nchi ya kigeni tena ni jirani zetu. Hapa kunaweza kuwa na mgogoro wa kidiplomasia na kimahusiano. Halikadhalika sikubaliani na jibu la Nape. Nakumbuka kuona barua ya mwaliko hapa JF na ilitaja Chama cha CCM, je kuna mahusiano Kati ya CCM na ODM kiasi cha kada wake kualikwa na kwenda kupiga kampeni ya waziwazi? Haya yanaitaji maelezo ya chama hata Kama ni kukanusha tu kuhusika kwa Chama kwa hali yoyote ile.
 
Inafahamika kwamba alikuwa Nchini Kenya ' eti ' kwa Mwaliko wa mmoja wa wagombea urais wa nchi hiyo Ndugu Raila Odinga , kama kawaida ya waafrika, akapewa fursa ya kuzungumza ama kusalimia umati , akatumia nafasi hiyo kuwashawishi wakenya kumchagua Odinga ! Kana kwamba yeye anamfahamu sana Raila kuliko wakenya wenyewe , maajabu ya mwaka ! Na alienda mbali zaidi kwa kuwaasa wakenya kwamba wasichague upande wa pili wenye wagombea ambao hawataweza hata kusafiri nchi jirani kwa sababu ya vikwazo vya kimataifa , hapa alimlenga Ndugu Uhuru Kenyatta na William Lutto ( rejea mambo ya THE HAGUE ) , Niweke wazi tu kwamba sina ugomvi wowote na Raila , bali sioni uhalali wowote kidiplomasia kwa foreigner kufanya kampeni za kisiasa , nakumbuka miaka ya nyuma kidogo John Komba na bendi yake ya TOT walivurumishiwa mawe juu ya jukwaa la kampeni wakimnadi Bakili Muluzi nchini Malawi , Huwezi kuamini ! Ndugu Komba na kitambi chake alitimua mbio vibaya mno , kwa siku kadhaa hali ya sisi watz tuliokuwa tunafanya biashara kwenye nchi ile ilikuwa tete sana , maana ilionekana kwamba msimamo wa John Komba na TOT yake ndiyo ulikuwa msimamo wa Tanzania ! Hebu wajuzi wa sheria za kimataifa watusaidie jambo hili , Nawasilisha .
 
Acheni uvivu wa kufikiri na siasa za chini ya vitanda, magufuli ameongea Kama rafiki wa raila na hajaongea kwa niaba ya CCM au serikali , mnalikuza jambo hili kwa maslahi ya ovyo ovyo tu, gazeti la raia mwema siku hizi nalo linaandika udaku tu.Magufuli na raila ni marafiki hata nje ya uwaziri wao Ana haki Kama raia yeyote kummunga mkono raila kwa uwazi bila kificho Kama alivyofanya.

Nashangaa Huyu wenje ambaye hata mwanza wamemchoka anakurupuka kutoa matamko yasiokuwa na msingi, acheni watu wafanye siasa za maana sio kuongea usikike kuwa wewe ni msemaji au wa waziri kivuli wa mambo ya Nje.
Mm nakubaliana nawe lakini Magufuli km mwanasiasa hakutakiwa kuuacha urafiki wake na odinga utumike kisiasa, kwa sababu kiukweli watanzania watajua ndo msimamo wa serikali. kama angezungumza kwa ujumla na kuwatakia wakenya kampain njema isingegua shida. tatizo ni pale anapochagua kumpigia debe odinga. mwanasiasa makini hawezi kufanya hivyo!
 
Acha dharau na ujiulize hivi:

1. Je, Magufuri ni raia wa nchi gani wakati anatoa maoni au kupiga kampeni za kisiasa?

2. Je, Magufuri anayo hadhi gani kimataifa, na matamshi au matendo yake kwenye ardhi ya nchi nyingine yana athari gani kwa nchi yetu?

3. Je, diplomasia yetu na nchi zingine ikoje, hasa ushiriki wetu kwenye siasa za nchi zingine?

USILETE KASHFA HAPA.

Unajua hizi ID za uongo zinawapa kiburi mno , mimi nimeuliza kwa nia njema kabisa ili kujua kama kuna uhalali wa kisheria kwa foreigner kufanya kampeni ? Sasa huu ndiyo utumbo wa PhD feki ! Jibu lilitakiwa kuwa ndiyo au hapana , na kwa nini , baaasi , longolongo hizi sijui ni kutaka sifa au sijui ndiyo posho za Lumumba !
 
Acheni uvivu wa kufikiri na siasa za chini ya vitanda, magufuli ameongea Kama rafiki wa raila na hajaongea kwa niaba ya CCM au serikali , mnalikuza jambo hili kwa maslahi ya ovyo ovyo tu, gazeti la raia mwema siku hizi nalo linaandika udaku tu.Magufuli na raila ni marafiki hata nje ya uwaziri wao Ana haki Kama raia yeyote kummunga mkono raila kwa uwazi bila kificho Kama alivyofanya.

Nashangaa Huyu wenje ambaye hata mwanza wamemchoka anakurupuka kutoa matamko yasiokuwa na msingi, acheni watu wafanye siasa za maana sio kuongea usikike kuwa wewe ni msemaji au wa waziri kivuli wa mambo ya Nje.
Tatizo mkuu hata kwenye mambo ya msingi kama hili unaleta uccm na uchadema! watanzania tufike mahali uwezo wetu wa kufikiri upite mahaba yetu kwa vyama vyetu. Nadgani mtoa mada ana hoja ya msingi tu mkubwa wangu. Ni kweli wao ni marafiki, but ukumbuke huyu pia ni waziri. kidiplomasia inaleta utata sababu ya kofia yake ya uwaziri.Hapa nadhani swala ni busara tu ndio imepunguka, ingawa of course hana kosa kisheria kukampeni for Raila. Na hilo ndio wadau wanadhani waziri anapaswa kuwa makini na kauli zake, apunguze mihemuko isiyo na tija! Kumbuka kuna siku alimwomba Rais azidi kutalii nje ya nchi coz inatusaidia kupata chochote kitu kutoka kwa wafadhili. Hivi ni lazima kwa rais kwenda kila wakati nje ili tupate misaada? alikuwa anatuambia kwamba hatuna alternative nyingine ya ku develop without wafadhili? Je kaka unadhani kauli hii ilikuwa sahihi? sikwamba ili mfedhehesha Rais? Mheshimiwa anahuruka ya kuropoka na hili ndilo mtoa maada alikuwa anataka tumjadili ili ikibidi ajirekebishe!
 
magufuli hana break ktk kujikomba kwa watu, alijikomba kwa mbowe hadi mbowe akashangaa ktk hotuba yake ya bungeni kwa wizara yake.NIlijiuliza sana kama magufuli anajua kuwa Huyo pizani wa Zimbabwe alinanyang`anywa ushindi kam CCM wafanyavyo, na kuhusu raila sijui kam huyu bogus anajua nini anafanya na serikali yake imesimama wapi?
 
Mnataka kusema chadema wanapoenda ujeruman kwa christian party wanatuwakilisha na watu wa dini nyingne?
 
Tusiandikie mate,
tumsikilize Mh. Raila Odinga akimtambulisha Dr. Magufuli kama waziri wa ujenzi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndani ya dakika moja na sekunde 37 za mwanzo za clip hii na kuzungumzia kampeni yake ya kutaka Urais wa Kenya na kumtaka Dr. John Pombe Magufuli afikishe salamu za shukrani kwa mshikamano wake kumpa moyo juu ya hamu yake mh. Odinga kuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya.:

Raila's speech during ODM delegates conference 07/Dec/2012


Source: ktnkenya.tv
 
Last edited by a moderator:
ulimbukeni tu ndio unaomfanya Dr. makufuri aweweseke kiasi kama hiki
 
Back
Top Bottom