Inafahamika kwamba alikuwa Nchini Kenya ' eti ' kwa Mwaliko wa mmoja wa wagombea urais wa nchi hiyo Ndugu Raila Odinga , kama kawaida ya waafrika, akapewa fursa ya kuzungumza ama kusalimia umati , akatumia nafasi hiyo kuwashawishi wakenya kumchagua Odinga ! Kana kwamba yeye anamfahamu sana Raila kuliko wakenya wenyewe , maajabu ya mwaka ! Na alienda mbali zaidi kwa kuwaasa wakenya kwamba wasichague upande wa pili wenye wagombea ambao hawataweza hata kusafiri nchi jirani kwa sababu ya vikwazo vya kimataifa , hapa alimlenga Ndugu Uhuru Kenyatta na William Lutto ( rejea mambo ya THE HAGUE ) , Niweke wazi tu kwamba sina ugomvi wowote na Raila , bali sioni uhalali wowote kidiplomasia kwa foreigner kufanya kampeni za kisiasa , nakumbuka miaka ya nyuma kidogo John Komba na bendi yake ya TOT walivurumishiwa mawe juu ya jukwaa la kampeni wakimnadi Bakili Muluzi nchini Malawi , Huwezi kuamini ! Ndugu Komba na kitambi chake alitimua mbio vibaya mno , kwa siku kadhaa hali ya sisi watz tuliokuwa tunafanya biashara kwenye nchi ile ilikuwa tete sana , maana ilionekana kwamba msimamo wa John Komba na TOT yake ndiyo ulikuwa msimamo wa Tanzania ! Hebu wajuzi wa sheria za kimataifa watusaidie jambo hili , Nawasilisha .