CCM kukurupuka kwenu kutawagharimu zaidi

CCM kukurupuka kwenu kutawagharimu zaidi

Bm_boy

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2013
Posts
547
Reaction score
348
Salam JF

Kumekua na propaganda nyingi kila kukicha juu ya Dr Slaa.. Mara amehama, mara kachukizwa na ujio wa EL na Bla bla kibao. Na bila mashaka, yote haya yanaratibiwa na Team Lumumba.

Kwangu mimi, nafikiri wamefanikiwa kuwapa hofu Wanachadema kwa asilimia flani..

Ila wakumbuke siku Dr akijitokeza hadharani, tena natamani aendelee kujificha hadi 8.8.2015, Chadema watakapo fanya mkutano wa kihistoria uwanja wa Taifa kama tulivyo taarifiwa.. huku dunia ikiutazama ndipo awachane makavu, na ndio liwe anguko la CCM mazima.

CCM wamekua wakiweka planning wasizojua matokeo yake badae. Kwenye List ya mafisadi walikua zaidi ya kumi, tena EL alikua namba kama sikosei ni 9 lakini Chadema waliamua ku deal na EL kwasababu ya nguvu walioiona aliyokua nayo ndani CCM.. Kwa kulijua hilo walijua wakifanikiwa kumdhoofisha EL tumeidhoofisha CCM.

CCM bila kujua wakababia wakaona EL ndio anatuchafulia chama sasa la msingi ni kumng'oa, wakaja na operation Vua gamba.. Ikagonga mwamba mwisho wa siku ni kuamua kumkata, matokeo yake ndio haya.

Sasa nataka niwaambie CCM, hizi propaganda zenu za kubabia ndio zinawamaliza. Sasa hivi macho ya Watanzania wote yapo Chadema na zaidi ni kujua kweli Dr anahama. Ila siku Dr akija hadharani na kukanusha hili, ndilo litakua anguko la CCM la mwisho.

Na hapa waliopewa kazi ya kukusanya rambi rambi za kifo cha CCM basi wafanye kazi yao ya uhakika.

Uwanja utarindima shangwe na nderemo atakapoonekana Dr Slaa.

Asante CCM kwa hili
Nawasilisha
 
mambooo matamu mwaka huu.... tutashuhudia mengi mnoooo
CCM hawatakiwi kujibu chochote, anayetakiwa kujibu ni Luhanjo, je ni kweli alimpigia simu Kikwete kuhusu richmond na Kikwete akakataa mkataba usivunjwe na kupelekea kashfa kwa watu wasiohusika huku yeye akipeta, je ni yeye aliyezuia utekelezaji wa mapendekezo ya Mwakyembe na kusababisha Taifa kuendelea kupata hasara za umeme wa gharama ya juu, kumbe ni mradi wa watu wachache walioko magogoni?
 
CCM imecheza ngoma ya Chadema bila kumuelewa mpiga ngoma anatumia nini. CCM ikumbuke kuwa chadema haikulala toka uchaguzi wa 2010.
 
Hatimae Magufuli anabaki mpweke.UKAWA na Mashabiki wa Lowasa wao hawana time na Magufuli,wanampamba na kumtetea Lowasa tu
 
Na hapa bado trela.huyu Lowasa atakapoanza kutambulishwa mikoani alipokuwa akifunika wakati wa kutia nia,ndo mjadala kuhusu Magufuli utafungwa kabisa
 
Sio kwamba wanakurupuka bali kila mmoja anataka awe RAIS kupitia "kitengo"
 
Duh, sasa kama hivyo ndivyo mbona unatoa siri, jamaa si wataandaa plan nyingine mwisho inakuwa mchezo usioisha?
 
Bavicha anatoa ushauri kwa CCM.

Kwi kwi kwi!!

Tunaionea huruma ccm kwani kuwa kambi ya upinzani kunatakiwa kuwa na wabunge kamili na siyo wabunge wa mipasho kama waliojazana ccm kina kibajaji,profesa wa mazingaombwe
 
CCM imecheza ngoma ya Chadema bila kumuelewa mpiga ngoma anatumia nini. CCM ikumbuke kuwa chadema haikulala toka uchaguzi wa 2010.

Mkuu ccm wamepanda mtumbwi wa vibwengo
 
Back
Top Bottom