GE2025 CCM kuitisha Mkutano Mkuu kwa njia ya Mtandao, Je ni njia ya kuwakwepa/ kuwaogopa Wajumbe?

GE2025 CCM kuitisha Mkutano Mkuu kwa njia ya Mtandao, Je ni njia ya kuwakwepa/ kuwaogopa Wajumbe?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Sir John Deere

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2017
Posts
14,162
Reaction score
27,197
CCM imetangaza kuitisha Mkutano Mkuu wa dharura siku ya jumamosi bila kuwekwa wazi agenda za mkutano huo.

Hii ni kwa mara ya kwanza katika historia ya chama hicho hasa kwa mkutano mzito kama huo wenye wajumbe zaidi ya elfu 2 nchi nzima.

Makatibu wa mikoa na wilaya wameagizwa kufanya maandalizi kwa maana ya kumbi za mikutano na vifaa vya mawasiliano.

Binafsi kwa tathmini fupi sana niliyoifanya mkutano huo hautakua na tija kwa kuwa mazingira yetu hasa kwa upande wa sayansi na teknolojia tunayajua.

Ushauri wangu ni Bora mkutano usogezwe mbele lakini Kila mjumbe apate kuhudhuria yeye mwenye kikao cha mkutano mkuu ni kikao kizito kinachotoa maazimio mazito.
 
Ajenda imevuja: Majina yote ya wagombea wa nafasi ya ubunge na udiwani kurudi.
Mkutano mkuu hauusiki na mchakato wa kupitisha wagombea Ubunge na Udiwani ingawa kurudisha majina yote ni sahihi.

Kukata majina kabla ya kupigiwa kura ni uonevu na kinyume cha katiba.

Waliotowa hongo majina yao yarudi wameliwa.
 
Mkutano mkuu hauusiki na mchakato wa kupitisha wagombea Ubunge na Udiwani ingawa kurudisha majina yote ni sahihi.

Kukata majina kabla ya kupigiwa kura ni uonevu na kinyume cha katiba.

Waliotowa hongo majina yao yarudi wameliwa.
Kanuni kaitunga nani? Ataitengua nani?
 
Kwamba wajumbe watakuwa hawaonani, Wabongo bhana 😂 Mbona viongozi wa mataifa huko nje wanafanya hv Kwahy nao wanaogopana?
 
CCM imetangaza kuitisha Mkutano Mkuu wa dharura siku ya jumamosi bila kuwekwa wazi agenda za mkutano huo.

Hii ni kwa mara ya kwanza katika historia ya chama hicho hasa kwa mkutano mzito kama huo wenye wajumbe zaidi ya elfu 2 nchi nzima.

Makatibu wa mikoa na wilaya wameagizwa kufanya maandalizi kwa maana ya kumbi za mikutano na vifaa vya mawasiliano.

Binafsi kwa tathmini fupi sana niliyoifanya mkutano huo hautakua na tija kwa kuwa mazingira yetu hasa kwa upande wa sayansi na teknolojia tunayajua.

Ushauri wangu ni Bora mkutano usogezwe mbele lakini Kila mjumbe apate kuhudhuria yeye mwenye kikao cha mkutano mkuu ni kikao kizito kinachotoa maazimio mazito.
Wanajaribu kutumia digital
 
Hii ni njia nzuri, mjumbe anaweza kua blocked/ being taken away easily iwapo tu ataonekana analeta hoja za kupinga.
 
Ndio faida za kukua technology - hapo CCM itaokoa fedha nyingi ambazo zingelipwa ktk vikao, usafiri na chakula.

SSH big up!
 
Back
Top Bottom