Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,565
- 2,484
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kigamboni, jijini Dar es Salaam, kimekemea na kulaani vikali vitendo vya baadhi ya watia nia wa nafasi za ubunge na udiwani kuanza kampeni kabla ya wakati pamoja na kutoa rushwa, kinyume na taratibu na sheria za nchi.
Akitoa taarifa hiyo wakati wa uwasilishaji wa tathmini ya utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kipindi cha mwaka 2020 hadi 2025 katika Kata ya Kibada, ambapo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kigamboni, Yahya Sikunjema, amesema chama kwa kushirikiana na mamlaka za serikali hakitasita kuchukua hatua kali kwa wote watakaobainika kukiuka maadili ya uchaguzi kwa kutoa rushwa.
Amesema utekelezaji wa ilani hiyo umefikia asilimia 99, jambo linalodhihirisha dhamira ya chama hicho katika kutimiza ahadi kwa wananchi.
Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Kibada, Amini Sambo, amesema utekelezaji wa ilani umeendelea kuleta mafanikio makubwa kwa wananchi, ikiwemo kutatua changamoto zilizodumu kwa muda mrefu, kama vile ujenzi wa barabara ya Kibada hadi Mwasonga yenye urefu wa kilomita 45 kwa kiwango cha lami.
Pia soma Pre GE2025 - CCM Kuzuia Watia Nia Mapema: Kuminya Demokrasia au Kuthibiti Nidhamu ya Chama?
Katika tukio hilo pia alikuwepo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Kibada, Mboni Mbegu, ambaye alieleza namna wanawake wanavyoendelea kunufaika na utekelezaji wa ilani hiyo, hasa kupitia miradi ya maendeleo na uwezeshaji kiuchumi ambapo amewahasa wanawake kuchukua fursa za kuingia katika kugombea nafasi mbalimbali.
Akitoa taarifa hiyo wakati wa uwasilishaji wa tathmini ya utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kipindi cha mwaka 2020 hadi 2025 katika Kata ya Kibada, ambapo Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kigamboni, Yahya Sikunjema, amesema chama kwa kushirikiana na mamlaka za serikali hakitasita kuchukua hatua kali kwa wote watakaobainika kukiuka maadili ya uchaguzi kwa kutoa rushwa.
Amesema utekelezaji wa ilani hiyo umefikia asilimia 99, jambo linalodhihirisha dhamira ya chama hicho katika kutimiza ahadi kwa wananchi.
Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Kibada, Amini Sambo, amesema utekelezaji wa ilani umeendelea kuleta mafanikio makubwa kwa wananchi, ikiwemo kutatua changamoto zilizodumu kwa muda mrefu, kama vile ujenzi wa barabara ya Kibada hadi Mwasonga yenye urefu wa kilomita 45 kwa kiwango cha lami.
Pia soma Pre GE2025 - CCM Kuzuia Watia Nia Mapema: Kuminya Demokrasia au Kuthibiti Nidhamu ya Chama?
Katika tukio hilo pia alikuwepo Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Kata ya Kibada, Mboni Mbegu, ambaye alieleza namna wanawake wanavyoendelea kunufaika na utekelezaji wa ilani hiyo, hasa kupitia miradi ya maendeleo na uwezeshaji kiuchumi ambapo amewahasa wanawake kuchukua fursa za kuingia katika kugombea nafasi mbalimbali.