Eng. Y. Bihagaze
JF-Expert Member
- Sep 8, 2011
- 1,488
- 908
Faida za Muungano ni zipi kwa Tanganyika na Zanzibar?kila nchi inafaidikaje kwa uwepo wa muungano huu?ziwekwe wazi ili wananchi wapime kwa mizani kama kuna faida au laa
Ndugu BONGOLALA kwa sasa Zanzibar inainyonya "Tanganyika" kwani yapo mambo mengi ambayo Wazanzibari wanafaidi na wana haki ya kuyafanya ilihali Wadanganyika hawawezi kuyafanya. Hii sio haki hata siku moja achilia mbali mchango katika gharama za kuendesha mambo ya Muungano ni almost unabebwa na Wadanganyika. Thats why naungana na wanaodhani kuwa Muungano wa dhati ni wa serekali 1 Unguja na Pemba ninakuwa mikoa kama Pwani na Lindi. Kwa wanaotaka Muungano wa kinafiki wanataka serekali 2, kwa wanaotaka Muungano ujifie wenyewe bila lawama kwa mtu wanataka serekali 3.
Ingawa hatujabahatika kuwa Na Muungano Tanzania, hiki kidogo kinachoitwa MUUNGANIKO nacho pia Chama Changu CCM mnataka kukiangamiza.
KWANINI CC ya Chama, ichoke kutafakari? Mchoke kugundua Moshi unaofuka Kwa kasi mpya Na kuuzuia Kwa kuweka makalio?..CCM Mna lengo gani Na Nchi hii? Mnataka mpaka Tuuane miongoni mwetu ndipo furaha Yenu ikamilike? KWANINI Muwe na Ibilisi mbaya kabisa this way..
CCM ingekuwa Na Ubinaadam lau mngepiga mbiu tuwe na MUUNGANO yaani Serikali Moja, Nchi Moja, Taifa Na wataifa wamoja Na Raisi Mmoja. Kuendelea kushinikiza serikali mbili ni kupalilia zaidi matatizo yaliyowashinda mnayoyafaham Fika.
Hakuna Kura iliyofanyika up-to now but dalili zote Za Wazenji kuupinga Muunganiko huu ziko wazi kabisa Na mnazijua. Au utaitisha Kura ya kitaifa Na wazi Kwamba 44:1 itafanya Kazi, wazanzibar wote wakipiga kura maskini ni watu wasiozidi milioni moja ambao watafunikwa Kwa mbali na Watanzania bara. Ujinga umetufikisha hapa sasa werevu ututoe hapa.
Hiyo CC ya Chama inayoshinikiza muunganiko huu uendelee Ina wajumbe wangapi? Kutoka bara ni wangapi na visiwani wangapi? Tuwe fare Kwa hili.
Huu Muunganiko wa serikali mbili mnaoshinikiza udumishwe JE asilimia Ngapi ya Wazanzibar Wanautaka?? Na vikao vya kuongelea Nchi ya watu vinafanyika upande mmoja wa Nchi kila siku. Mie kwangu sioni Kama ni Busara kuutumia wingi wetu, Nguvu zetu kuwakandamiza wachache wazanzibar Kwa Sababu tu waliingia mkenge wenyewe that time. Mie sipendi Mtu aonewe Hata kama SIO jamaa yangu KWANINI Umuonee??
Mambo haya yawe wazi, ifanyike Kura ya kitaifa, wazanzibar wengi wakisema hatutaki hiki kitu sioni Sababu ya kulazimishana. Au wabara wakisema hawataki hii makitu inaondolewa tu. SIO watu wawili watatu walioshiba minyoo matumboni mwao waamue Kwa Ujinga Mustakabali wa mamilioni ya Raia Kwa Manufaa binafsi..
CCM ingekuwa Na Utu AMA ingepiga mbiu ya Muungano au kukubali zigo jipya la serikali tatu SIO Muunganiko huu ambao hakuna hata mwana ccm mmoja anayeuelewa. {Unarithi mavi na unaendelea kuyahifadhi ndani ya nyumba yako kwa sababu baba alisema yatageuka kuwa almasi siku moja. }Kuendelea kushinikiza Muunganiko huu CCM inajua wazi Wazanzibar watachokifanya Na inataka wakifanye ili waikoshe mikono Yao.. Mie Sijui wakoje.. Kama wachawi
Vile..
Wazanzibar waliingia mkenge kwenye muungano huu, maskini zanzibar, kila wakijaribu kujitoa wakoloni wao tanganyika kupitia ccm wamekaba tu!
umenena vema. CCM wangesimamia Serikali Moja ingekaa vizuri sana hiyo. Kwa hali iliyopo Zanzibar watakataa Serikali moja kwa malengo wanayoyajua wao. Tanganyika hatupotezi kitu katika hilo. Kitachowapata mbele kitakuwa chao. Kiutu, ni hekina tu tunawapa angalizo kwamba Serikali Tatu haitakubaliwa in the long run kwa sababu mfumo huo utaleta zigo la serikali ya Muungano ambalo ni gharama ya uendeshaji nchi isiyokuwa na sababu wala umuhimu utaokulika kwenye eneo ambalo linaelekea kwenye Federation ya nchi pengine sita au saba.
Katika Serikali moja ni kwamba Zanzibar itapata bahati ya kuingia kwenye Federation ya EAC wakiwa na upendeleo maalum ndani ya Tanganyika. Hii ni bahati ya mtende kuota jangwani ambayo mwenye busara yeyote angeiona. In reality, Serikali Tatu ni dhana unviable; ni boya ambalo litapasuka mara tu litapotupwa majini na kuvunja muungano. Zanzibar kukataa Serikali Moja wanapoteza kabisa bahati ya upendeleo ndani ya Tanganyika. CCM ingekuwa makini ingewapelekea huu msimamo wakatae wenyewe. Waliokubali Serikali Tatu katika uhalisia hawataki Muungano. Kama CCM inautaka muungano njia ya kuuendea ni kuitisha serikali moja. Mbili hapana kwa sababu hakuna anayezitaka. That would be where to go for CCM.
Ndugu BONGOLALA kwa sasa Zanzibar inainyonya "Tanganyika" kwani yapo mambo mengi ambayo Wazanzibari wanafaidi na wana haki ya kuyafanya ilihali Wadanganyika hawawezi kuyafanya. Hii sio haki hata siku moja achilia mbali mchango katika gharama za kuendesha mambo ya Muungano ni almost unabebwa na Wadanganyika. Thats why naungana na wanaodhani kuwa Muungano wa dhati ni wa serekali 1 Unguja na Pemba ninakuwa mikoa kama Pwani na Lindi. Kwa wanaotaka Muungano wa kinafiki wanataka serekali 2, kwa wanaotaka Muungano ujifie wenyewe bila lawama kwa mtu wanataka serekali 3.
Basi warioba kawakashifu watanganyika coz kakuiteni watanzania bara,tanzania tanganyika ndio sahihi.Yes!Lakini umekosea sehemu moja tu,sisi sio wadanganyika sisi ni WATANGANYIKA,naomba usituvunjie heshima!!!
umenena vema. CCM wangesimamia Serikali Moja ingekaa vizuri sana hiyo. Kwa hali iliyopo Zanzibar watakataa Serikali moja kwa malengo wanayoyajua wao. Tanganyika hatupotezi kitu katika hilo. Kitachowapata mbele kitakuwa chao. Kiutu, ni hekina tu tunawapa angalizo kwamba Serikali Tatu haitakubaliwa in the long run kwa sababu mfumo huo utaleta zigo la serikali ya Muungano ambalo ni gharama ya uendeshaji nchi isiyokuwa na sababu wala umuhimu utaokulika kwenye eneo ambalo linaelekea kwenye Federation ya nchi pengine sita au saba.
Katika Serikali moja ni kwamba Zanzibar itapata bahati ya kuingia kwenye Federation ya EAC wakiwa na upendeleo maalum ndani ya Tanganyika. Hii ni bahati ya mtende kuota jangwani ambayo mwenye busara yeyote angeiona. In reality, Serikali Tatu ni dhana unviable; ni boya ambalo litapasuka mara tu litapotupwa majini na kuvunja muungano. Zanzibar kukataa Serikali Moja wanapoteza kabisa bahati ya upendeleo ndani ya Tanganyika. CCM ingekuwa makini ingewapelekea huu msimamo wakatae wenyewe. Waliokubali Serikali Tatu katika uhalisia hawataki Muungano. Kama CCM inautaka muungano njia ya kuuendea ni kuitisha serikali moja. Mbili hapana kwa sababu hakuna anayezitaka. That would be where to go for CCM.
Ili Muungano uendelee it is either serikali moja au mbili. Serikali 3 (which is just delayed kuvunja muungano) ni sawa na kuuvunja muungano. Ni afadhali basi tuuvunje tu sasa hivi. Kwa nini hawa wazee wananoa mapanga ili vijana waje wauvunje kirahisi wakati wao watakuwa wameondoka? Warioba asitudanganye. halafu kama serikali tatu ni mapendekezo tu bado, mbona tayari wameandaa katiba inayotambua serikali tatu? Anatu preempt! Mimi naona tujadili kwanza aina ya muungano, tukishakubaliana ndipo katiba inayotambua tulichokubaliana ije tuijadili.Kukaba haitowasaidia ccm kuwabadilisha mawazo waz'br,bila ya zanzibar yenye mamlaka kamili muungano bye!bye!