CCM inamdhalilisha Rais Samia

CCM inamdhalilisha Rais Samia

Hakupitia mchujo wowote, na hakuwahi kugombea Urais.

Ni Rais sababu ya KIFO, Si uchaguzi.
Kha! Kwa hiyo mheshimiwa Rais ni Rais wa kifo?
Yaani tumtambue kuwa sio wa matakwa ya wananchi bali yupo kwa matakwa ya kifo?
Sikuwahi kuwaza hilo na hata chief chawa Lucas Mwashambwa nadhani hilo hajawahi kulifikiri!

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Ccm wawe jasiri kuachana na huu utaratibu wa sasa. Unaweza kuja kuwaletea madhara ikiwa wananchi watamkataa kwa kura nyingi. Isitoshe rais si malaika, anaweza kuwa dhaifu nchi ikaharibika, miaka 10 si mchezo kuja kurekebisha. Ipo siku huu ubabe utafika mwisho, tuangalie historia ya nchi jirani kama Zambia, Malawi, Kenya... ipo siku

CCM, kama kawaida yao, wametengeneza precedence ya kijinga, hiyo ya kusema kuwa kila anayekuwa Rais ni lazima aachwe amalize miaka 10 bila ya kupingwa wala kushindanishwa na mtu yeyote. Kwa huo upumbavu, ina maana uchaguzi tunaoufanya kila baada ya miaka 5, ni maagizo tu.

Siku akipatikana Rais kichaa, anaharibu kila kitu, lakini kwa hùu ujinga wa CCM, bado watamwacha amalize miaka 10!!
 
Bila aibu, baadhi ya viongozi wa CCM wanafanya vitendo vya kumdhalilisha Rais Samia.

Tumesikia kelele za baadhi ya viongozi wa CCM kuwa eti mwaka 2025, kwa upande wa CCM, itachapishwa fomu moja tu ya mgombea wa Urais, nayo atapewa Rais Samia.

Mimi nauona huu udhalilishaji dhidi ya Rais. Tafsiri ya kuchapisha fomu moja ni kwamba Rais Samia akishindanishwa, hawezi kushinda. Je, fikra hizo zina ukweli wowote? Kwa nini wamfanyie hivyo Rais Samia?

Ni nani hao ambao wanaamini kuwa Rais Samia akishindanishwa nao, hawezi kuwashinda? Ni hawa hawa wateule wake au kuna wengine?
Wewe unaamini hata akishindanishwa. na Musukuma, atashinda?
 
Nchi ina matahira wengi sana, jitu mpaka leo halijui hata utaratibu wa CCM mgombea anapogombea awamu ya pili.

Ngoja nikuulize mleta mada, eti una mtoto?
Hii awamu karithi, sasa kama karithi ni awamu ya ngapi karithi? Si ya pili? Utaratibu upoje kwa awamu ya pili?
 
Ngoja

Mkapa 2000 alishindanishwa na nani?

Kikwete 2010 alishindanishwa na nani?

Shujaa Magufuli 2020 alishindanishwa na nani?!

Niko pale......
1995 Mkapa alishindanishwa na Jakaya Kikwete na Cleopa Msuya n.k

2005 Kikwete alishindanishwa na Dr.Salim A. Salim na Prof.Mark Mwandosya n.k

2015 Magufuli alishindanishwa na Balozi Amina Ally & Dr. Asha Rose Migiro n.k

Samia amepata urais kikatiba hajawahi kipitia kwenye mchujo ndani ya chama. 2025 CCM wafanye mchakato hata kama ni danganya toto.
 
Habari ndio hiyo......hata Magu asingemshinda Membe.
Membe alikuwa mwepesi zaidi ya pamba. Alienda ACT Wazalendo kugombea urais akaambilia kula 80k hata Sugu wa Mbeya alikuwa na ushawishi zaidi ya mwanausalama mbobevu.

Labda ungesema Lowassa.
 
Bila aibu, baadhi ya viongozi wa CCM wanafanya vitendo vya kumdhalilisha Rais Samia.

Tumesikia kelele za baadhi ya viongozi wa CCM kuwa eti mwaka 2025, kwa upande wa CCM, itachapishwa fomu moja tu ya mgombea wa Urais, nayo atapewa Rais Samia.

Mimi nauona huu udhalilishaji dhidi ya Rais. Tafsiri ya kuchapisha fomu moja ni kwamba Rais Samia akishindanishwa, hawezi kushinda. Je, fikra hizo zina ukweli wowote? Kwa nini wamfanyie hivyo Rais Samia?

Ni nani hao ambao wanaamini kuwa Rais Samia akishindanishwa nao, hawezi kuwashinda? Ni hawa hawa wateule wake au kuna wengine?
Hiyo ni tafsiri Yako lakini utamaduni wa ccm awamu ya Pili Rais hashindanishwi na mtu Toka enzi za JK, Magufuli na Sasa CCM.

Mwisho hata wangemshindanisha hakuna wa kumshinda.
 
Nchi ina matahira wengi sana, jitu mpaka leo halijui hata utaratibu wa CCM mgombea anapogombea awamu ya pili.

Ngoja nikuulize mleta mada, eti una mtoto?
Utaratibu!!!imeandikwa sehemu? Kama mi utaratibu kwanini inatumika nguvu kubwa sana kuwaambia watu wa ccm kuwa watachapisha fomu 1? Acha kutetea ujinga.
 
Hiyo ni tafsiri Yako lakini utamaduni wa ccm awamu ya Pili Rais hashindanishwi na mtu Toka enzi za JK, Magufuli na Sasa CCM.

Mwisho hata wangemshindanisha hakuna wa kumshinda.

Kama kuna uhakika kuwa Samia atawashinda wagombea wowote watakaojitokeza, kwa nini wawazuie watu wengine kugombea?
 
Kama kuna uhakika kuwa Samia atawashinda wagombea wowote watakaojitokeza, kwa nini wawazuie watu wengine kugombea?
Jibu ni utamaduni wa ccm,Huwa hawspendi mgombea wao kuonekana alikuwa anapingwa na Baadhi Yao.

Wasubirie 2030 wawashiane moto
 
Jibu ni utamaduni wa ccm,Huwa hawspendi mgombea wao kuonekana alikuwa anapingwa na Baadhi Yao.

Wasubirie 2030 wawashiane moto

Japo, utamaduni wa namna hiyo hauna afya kwa chama wala nchi, kuna haja gani ya kuchapisha hata hiyo fomu moja? Si wasubirie tu uchaguzi akapambane na wagombea wa vyama vingine kuliko kupoteza muda na fedha kwa kufanya mambo ya maigizo?
 
Japo, utamaduni wa namna hiyo hauna afya kwa chama wala nchi, kuna haja gani ya kuchapisha hata hiyo fomu moja? Si wasubirie tu uchaguzi akapambane na wagombea wa vyama vingine kuliko kupoteza muda na fedha kwa kufanya mambo ya maigizo?
Utaratibu lazima ufuatwe hata kama Fomu ni Moja.

Tija ipo mbona huko Kwenu Kwa Machadema mna mgombea 1 wa Maisha hata hiyo Fomu 1 Huwa haichapishwi? 😆😆
 
Utaratibu lazima ufuatwe hata kama Fomu ni Moja.

Tija ipo mbona huko Kwenu Kwa Machadema mna mgombea 1 wa Maisha hata hiyo Fomu 1 Huwa haichapishwi?

Usiseme kwenu. Yaelekea hujui.

Nijuacho ni kuwa CHADEMA hakuna mtu amewahi kukataliwa kuchukua fomu na kuomba nafasi yoyote. Na sijawahi kuona tamko lolote likieleza kuwa fomu ya kugombea uongozi kwenye nafasi yoyote ya uongozi itakuwa moja.
 
Usiseme kwenu. Yaelekea hujui.

Nijuacho ni kuwa CHADEMA hakuna mtu amewahi kukataliwa kuchukua fomu na kuomba nafasi yoyote. Na sijawahi kuona tamko lolote likieleza kuwa fomu ya kugombea uongozi kwenye nafasi yoyote ya uongozi itakuwa moja.
Sio tuu huko Chadema wamekataliwa Bali Sultan anakutimua kwenye chama au kukuua ,usidhani wote wajinga kama wewe.eg Zito,Wangwe etc

View: https://twitter.com/ccm_tanzania/status/1781685285954228436?t=tCrv4OzkgE99ogjzkoUacQ&s=19
 
Back
Top Bottom