JOESKY
JF-Expert Member
- Mar 25, 2015
- 823
- 2,045
Kwa siku za hivi karibuni mara baada ya kuanza bunge kumezuka mambo ambayo kwakweli sisi kama Wananchi na Watanzania hatukuzoea kabisa tangu tupate uhuru wetu 1961.
Kuna mambo yanaendelea Bungeni yanatia hasira na kuchochea laana ambayo hatutaki itokee katika hili taifa lililoasisiwa na marehemu baba wa taifa JK Nyerere.
Sasa kwa trend hii ya kila mbunge ambaye anapewa muda wa kuchangia waliomtuma wananchi wake bungeni yeye ana dedicate muda huo "KUPIGA KAMPENI ZA KIBADILISHA KATIBA ILI RAIS ATAWALE MILELE" Anasahau kuwa hicho anachokisema sicho tunachokihitaji sisi wananchi.
Ni kitu cha aibu kuona mbunge unapaza sauti yako kupiga kampeni ili Rais asalie madarakani milele tena inasikitisha wameanza mapema sana kabla hata mwaka mmoja haujaisha toka aingie madarakani kwa awamu ya pili.
Kwa hili linaloendelea bungeni ni aibu tena aibu kubwa sana. Hatuwezi kuwa watu wa kupigia promo mambo ambayo hayana manufaa yoyote kama hili. Natamani wabunge wasome nyakati wasije wakapalilia na kurutubisha dhambi ya kutaka kuiletea dhahama nchi yetu.
Nimesikitishwa sana na haya yanayoendelea bungeni. Hatukuzoea kuona bunge la ajabu kama hili hata kama tunasema bunge la Tanzania ni dhaifu hata Profesa Mussa Assad alishawahi kulisema hili ila kwa awamu hii hili limethibitika waziwazi.
Ushauri wa bure Bashiru na Polepole wapeni hata course hao wabunge wenu wanakiaibisha chama na taifa kwa jumla.
Naishia hapa japo nina mengi ya kuandika
Kuna mambo yanaendelea Bungeni yanatia hasira na kuchochea laana ambayo hatutaki itokee katika hili taifa lililoasisiwa na marehemu baba wa taifa JK Nyerere.
Sasa kwa trend hii ya kila mbunge ambaye anapewa muda wa kuchangia waliomtuma wananchi wake bungeni yeye ana dedicate muda huo "KUPIGA KAMPENI ZA KIBADILISHA KATIBA ILI RAIS ATAWALE MILELE" Anasahau kuwa hicho anachokisema sicho tunachokihitaji sisi wananchi.
Ni kitu cha aibu kuona mbunge unapaza sauti yako kupiga kampeni ili Rais asalie madarakani milele tena inasikitisha wameanza mapema sana kabla hata mwaka mmoja haujaisha toka aingie madarakani kwa awamu ya pili.
Kwa hili linaloendelea bungeni ni aibu tena aibu kubwa sana. Hatuwezi kuwa watu wa kupigia promo mambo ambayo hayana manufaa yoyote kama hili. Natamani wabunge wasome nyakati wasije wakapalilia na kurutubisha dhambi ya kutaka kuiletea dhahama nchi yetu.
Nimesikitishwa sana na haya yanayoendelea bungeni. Hatukuzoea kuona bunge la ajabu kama hili hata kama tunasema bunge la Tanzania ni dhaifu hata Profesa Mussa Assad alishawahi kulisema hili ila kwa awamu hii hili limethibitika waziwazi.
Ushauri wa bure Bashiru na Polepole wapeni hata course hao wabunge wenu wanakiaibisha chama na taifa kwa jumla.
Naishia hapa japo nina mengi ya kuandika
