Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,146
- 48,382
Ukimsikiliza Samia Suluhu Hassan anaponadi Ahadi zake, unaweza kudhani anayoyasema leo kuwa atayatekeleza atakapotangazwa mshindi, labda alishindwa kuyatekeleza kwa kuwa CCM iliyokuwa inaongoza nchi ilimkatalia.
Lakini ukitafakari kwa makini unagundua hiyo CCM ya miaka minne iliyopita ilikuwa inaongozwa na yeye na pia ndiye aliyekuwa Rais.
Huko majimboni wagombea ubunge na udiwani wanatoa ahadi za kujiapiza na kujimaliza utadhani kwenye majimbo wanayogombea wabunge na madiwani walikuwa siyo wa chama chao.
Mwisho wa siku unagundua kumbe CCM inayotaka kuingia madarakani, ndiyo CCM ileile inayotaka kutolewa madarakani.
Watanzania wanashiriki kwenye maigizo ya kiwango duni sana lakini yanayokuzwa na Ombwe la kutokuwepo kwa uchaguzi HALISI.
Lakini ukitafakari kwa makini unagundua hiyo CCM ya miaka minne iliyopita ilikuwa inaongozwa na yeye na pia ndiye aliyekuwa Rais.
Huko majimboni wagombea ubunge na udiwani wanatoa ahadi za kujiapiza na kujimaliza utadhani kwenye majimbo wanayogombea wabunge na madiwani walikuwa siyo wa chama chao.
Mwisho wa siku unagundua kumbe CCM inayotaka kuingia madarakani, ndiyo CCM ileile inayotaka kutolewa madarakani.
Watanzania wanashiriki kwenye maigizo ya kiwango duni sana lakini yanayokuzwa na Ombwe la kutokuwepo kwa uchaguzi HALISI.