CCM hawasemi tu lakini wanapumulia mashine

CCM hawasemi tu lakini wanapumulia mashine

Kwani UKAWA walisema? Ukweli ni kwamba..lakuvunda halina ubani! Kungekuwa na maroroso mngesikia tu...ccm ni imara zaidi na zaidi
 
Baada ya October tuwekeane Marufuku mtu asituletee Ngonjera za 2010 kuwa Mlishinda ila kura ndo zimeibiwa na kuchakachuliwa. Miaka Minne iliyopita mlisema Slaa alishinda ila aliibiwa kura leo 2015 Mnasema alipata kura 2.2 M hivo hana ubavu wa kuitoa CCM
 
Wataficha lakn watasema tu........hali ni mbaya sana lumumba.
 
Mkuu mbona wameshasema? Wameshaanika aibu yao hadharani mchani kwamba hawana sera wala ushawishi wakuwawezesha kushinda. Na sasa kama mfa maji anavyoweza kushika hata wimbi la maji akijua ni ubao, wametangaza hadharani "kutafuta ushindi kwa goli lua mikono" na "mbinu zozote zile" hata haramu maadamu waendelee na ufisadi.

Kinchoonekana hawa watu wanajua bila kutawala hawawezi kuishi na hivyo wako tayari kuingiza nchi kwenye machafuko kitu ambacho sasa ni dhahiri kwa viapo hivyo kwamba wako tayari hata kuvunja katiba ili mradi waendelee kuishi kwa kutunyonga.

Sasa tuwasilikilizeni na kuwadharau kwa muda. Wakianza kuleta za kuleta tuwadhibiti kwa jywa hawatushindi na sasa tuko wengi sana na tumetapakaa kila kona ya nchi.

Usalama wao ni kufanya siasa za kistaarabu na amani.

Watambue vurugu walizozoea, na wowote wa katiba na haki za Watanzania hatutavumilia na wajue itakula kwao.

Hii nchi siyo yao ni ya Watanzania ambao wameikataa ccm kwa gharama yoyote!.
 
Baada ya October tuwekeane Marufuku mtu asituletee Ngonjera za 2010 kuwa Mlishinda ila kura ndo zimeibiwa na kuchakachuliwa. Miaka Minne iliyopita mlisema Slaa alishinda ila aliibiwa kura leo 2015 Mnasema alipata kura 2.2 M hivo hana ubavu wa kuitoa CCM

Ungejua 2010 na 2015 ni vitu viwili tofauti
 
Nilicheka sana jana, JK ili kutaka kuonyesha kwamba hakuna tatizo akajikuta anacheza miziki yote iliyokuwa inapigwa! Nilicheka sana nikajua kweli mzee kavurugwa!

Ukiona mtu mzima analia mbele za watu ....
 
Hakuna wa kumzuia Lowassa chini ya UKAWA kushinda uchaguzi wa mwaka huu.
Hata huyo Magufuli analijua hili basi tu hana jinsi ila angeweza angeshasurrender.
 
Kwani UKAWA walisema? Ukweli ni kwamba..lakuvunda halina ubani! Kungekuwa na maroroso mngesikia tu...ccm ni imara zaidi na zaidi

Kibaya zaidi mnachekeana kinafiki asilimia kubwa ya wanaccm watakao piga kura mwaka huu ni mkomoeni.
 
Huu ni wakati wa mabadiliko kila mtu anaejitambua anajua cha kufanya ,ila ukawa inatisha hata wao kimya kimya wanakubali
 
Back
Top Bottom