CCM hali tete,NEC ni tegemeo

CCM hali tete,NEC ni tegemeo

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Mambo hayaendí. Vituko,mwitiko na mtikisiko umetamalaki. Kwanza,Katiba mpya imegoma. Hakika,katiba mpya ingekuwa chapuo muhimu kwa CCM katika kampeni za mwaka huu-kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba. Pili,UKAWA wanavyokaa kimya kumtaja mgombea wao wa Urais ni pigo kwa CCM. Chama kilijipanga kumshambulia na kumsawajisha mgombea wa UKAWA na ndipo wetu angetangazwa. Ukimya wa UKAWA ni kuminywa kwa CCM.

Tatu,CCM kila uchao inapiga mahesabu ya nani awe mgombea wa Urais. Awe mwenye kashfa au sifa? Awe mwenye mvuto au uvundo? Awe toka Serikalini kulikoandamwa na kila rangi ya rushwa au toka nje ya Serikali ya awamu ya nne? Hali tete.

Nne,kashfa za ufisadi ni doa kuu kuelekea Oktoba. Pamoja na Serikali kuwasafisha watuhumiwa,mbele ya wananchi watuhumiwa hao ni wachafu na wasiofaa. Mbaya zaidi,watuhumiwa hao ndio wenye nguvu hata ya kupenya kwenye Urais. Kashfa za kifisadi zinazotajwa ni pamoja na Richmond,EPA na Escrow. Wananchi wanazikumbuka na wanawakumbuka watuhumiwa.

Tumaini la CCM yetu ni NEC ya Jaji Damian Lubuva. NEC inategemewa kufanya mambo ili uchaguzi wa Oktoba uote mbawa. CCM ipate muda wa kujipanga. Ipate ushindi. Lakini,hakuna dalili za NEC kuiponya au kuipunguzia maumivu CCM. Itapambana hivyohivyo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Hakuna mgombea ccm watakae mpitisha akose kashfa hasa ya ufisadi. Hakuna aliye msafi ndani ya chama cha mapinduzi.

Maana chama chenyewe ni mchafu kunuka kwa kila aina ya uchafu unaowahitaji Watanzania wakiweke kando.

CCM iko kwenye wakati mgumu sana like no any other time in history. Hadi wanafikiria kuiingiza nchi kwenye machafuko kwa kuahirisha uchaguzi ili eti wajipange kuweza kushinda!

CCM imepoteza uhalali wa kisiasa Kwa muda mrefu na sasa inaanza kujipotezea hata uhalali wa kisheria.
 
Hakuna mgombea ccm watakae mpitisha akose kashfa hasa ya ufisadi. Hakuna aliye msafi ndani ya chama cha mapinduzi.
Kinana anaandaliwa kuliokoa jahazi kwa kusimama mwenyewe kugombea urais kwa tiketi ya CHAMA hicho.
Vita itakuwa ni je, hawa jamaa ambao wamewekeza mapesa yao kwenye harakati za kuuwania urais kwa tiketi ya chama hicho watakubari kumwona Kinana anapitishwa?
Watamuunga mkono au watapigia debe upinzani ili kutimiza kauli ya "heri tukose wote"?
 
CCM ni maiti anayesubili mazishi hakiwezi kujikwamua tena ila tu easy wizi waibe tu ndo pona yao ila naamini tutacheza nao mziki kwenye banda moja ama zetu au zao!
 
Mambo hayaendí. Vituko,mwitiko na mtikisiko umetamalaki. Kwanza,Katiba mpya imegoma. Hakika,katiba mpya ingekuwa chapuo muhimu kwa CCM katika kampeni za mwaka huu-kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba. Pili,UKAWA wanavyokaa kimya kumtaja mgombea wao wa Urais ni pigo kwa CCM. Chama kilijipanga kumshambulia na kumsawajisha mgombea wa UKAWA na ndipo wetu angetangazwa. Ukimya wa UKAWA ni kuminywa kwa CCM.

Tatu,CCM kila uchao inapiga mahesabu ya nani awe mgombea wa Urais. Awe mwenye kashfa au sifa? Awe mwenye mvuto au uvundo? Awe toka Serikalini kulikoandamwa na kila rangi ya rushwa au toka nje ya Serikali ya awamu ya nne? Hali tete.

Nne,kashfa za ufisadi ni doa kuu kuelekea Oktoba. Pamoja na Serikali kuwasafisha watuhumiwa,mbele ya wananchi watuhumiwa hao ni wachafu na wasiofaa. Mbaya zaidi,watuhumiwa hao ndio wenye nguvu hata ya kupenya kwenye Urais. Kashfa za kifisadi zinazotajwa ni pamoja na Richmond,EPA na Escrow. Wananchi wanazikumbuka na wanawakumbuka watuhumiwa.

Tumaini la CCM yetu ni NEC ya Jaji Damian Lubuva. NEC inategemewa kufanya mambo ili uchaguzi wa Oktoba uote mbawa. CCM ipate muda wa kujipanga. Ipate ushindi. Lakini,hakuna dalili za NEC kuiponya au kuipunguzia maumivu CCM. Itapambana hivyohivyo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Naona taratiiiiiiibu dawa inaanza kufanya kazi.. wewe na Pasco sikuhizi naona mnakaribia kupona..ila nina wasiwasi na nyie isijekuwa mnataka tuwapokee halafu mchore ramani.Tupo macho!!!
 
Mambo hayaendí. Vituko,mwitiko na mtikisiko umetamalaki. Kwanza,Katiba mpya imegoma. Hakika,katiba mpya ingekuwa chapuo muhimu kwa CCM katika kampeni za mwaka huu-kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba. Pili,UKAWA wanavyokaa kimya kumtaja mgombea wao wa Urais ni pigo kwa CCM. Chama kilijipanga kumshambulia na kumsawajisha mgombea wa UKAWA na ndipo wetu angetangazwa. Ukimya wa UKAWA ni kuminywa kwa CCM.

Tatu,CCM kila uchao inapiga mahesabu ya nani awe mgombea wa Urais. Awe mwenye kashfa au sifa? Awe mwenye mvuto au uvundo? Awe toka Serikalini kulikoandamwa na kila rangi ya rushwa au toka nje ya Serikali ya awamu ya nne? Hali tete.

Nne,kashfa za ufisadi ni doa kuu kuelekea Oktoba. Pamoja na Serikali kuwasafisha watuhumiwa,mbele ya wananchi watuhumiwa hao ni wachafu na wasiofaa. Mbaya zaidi,watuhumiwa hao ndio wenye nguvu hata ya kupenya kwenye Urais. Kashfa za kifisadi zinazotajwa ni pamoja na Richmond,EPA na Escrow. Wananchi wanazikumbuka na wanawakumbuka watuhumiwa.

Tumaini la CCM yetu ni NEC ya Jaji Damian Lubuva. NEC inategemewa kufanya mambo ili uchaguzi wa Oktoba uote mbawa. CCM ipate muda wa kujipanga. Ipate ushindi. Lakini,hakuna dalili za NEC kuiponya au kuipunguzia maumivu CCM. Itapambana hivyohivyo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Mzee tupatupa umesahau mlivyommwagia sifa kemkem huyu mh. mtukufu mwenyekitu wetu? wapo waliowatahadharisha lakini mliweka pamba masikioni. Ona alikowapeleka sasa mlidhani mnawakomoa wapinzani wenu kumbe mnajitengenezea shimo taratibu. Hakuna pa kutokea lazima mzame mwaka huu.
 
Mzee Tupatupa ili chama chenu kisibomoke kwa nini msijikite kwenye ubunge tu na huo urais mkaacha kwa mtindo wa kubali yaishe? Maana huo urais ndio utakao UA chama kabisa
 
CCM ingekuwa na watu wa kweli kama mzee wangu TUPATUPA nadhani isingenuka uvundo huu ambao vijana tunauogopa,tunaingia kwenye siasa moja kwa moja upinzani
 
Edward Lowasa ambaye anapigiwa upatu agombee Urais kupitia CCM dalili ni wazi atapoteana kama sio kupata stroke ya matokea asiyoyatarajia

wakati "The Dream Team, Wanaoshikamana Wakati wa Mavuno" wanachanga KARATA ni vizuri kasi ya kuwashambulia ikaongezwa ili wapatwe na Kwiki kila wakisikia UKAWA. Hatimaye washindwe kabla ya mchuano
 
Ndio maana wanajitahidi kupitisha ile sheria ya mitandao ili wapumue.....
 
Wewe Tupatupa ni lini CCM iliingia kwenye uchaguzi pasipokuwa na minyukano? Kama CCM imeshindwa kujipanga kwa ajili ya uchaguzi tangu 2005 mpaka 2015 itawezaje kujipanga kwa miaka 2 hata kama uchaguzi hautafanyika Oktoba 2015? Ni lini CCM haikua na mgombea fisadi, 2005 JK alisikika ni mgombea aliyetumia rushwa kuliko wagombea wote na mwenyekiti wa CCM wa wakati huo Benjamini William Mkapa alituthibitishia kuwa 'Wagombea wote wametumia rushwa. Tofauti ni kiasi tu. Hivyo wote wamapungukiwa na utukufu' Lakini pamoja na kujulikana kuwa JK ni mla rushwa alipata 81% ya kula zote zilizopigwa. Tafsiri yake ni kuwa kwa Watanzania, rushwa sio tatizo na wanampenda mtoa rushwa. Na ndiyo maana hata wewe katika hoja zako unasema ' mafisadi ndiyo wenye nguvu kuliko waadilifu na huo ndiyo ukweli kizazi hiki kinampenda mtu asiyemwadilifu ie mla rushwa, mwongo na mzinzi
Mambo hayaendí. Vituko,mwitiko na mtikisiko umetamalaki. Kwanza,Katiba mpya imegoma. Hakika,katiba mpya ingekuwa chapuo muhimu kwa CCM katika kampeni za mwaka huu-kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba. Pili,UKAWA wanavyokaa kimya kumtaja mgombea wao wa Urais ni pigo kwa CCM. Chama kilijipanga kumshambulia na kumsawajisha mgombea wa UKAWA na ndipo wetu angetangazwa. Ukimya wa UKAWA ni kuminywa kwa CCM.

Tatu,CCM kila uchao inapiga mahesabu ya nani awe mgombea wa Urais. Awe mwenye kashfa au sifa? Awe mwenye mvuto au uvundo? Awe toka Serikalini kulikoandamwa na kila rangi ya rushwa au toka nje ya Serikali ya awamu ya nne? Hali tete.

Nne,kashfa za ufisadi ni doa kuu kuelekea Oktoba. Pamoja na Serikali kuwasafisha watuhumiwa,mbele ya wananchi watuhumiwa hao ni wachafu na wasiofaa. Mbaya zaidi,watuhumiwa hao ndio wenye nguvu hata ya kupenya kwenye Urais. Kashfa za kifisadi zinazotajwa ni pamoja na Richmond,EPA na Escrow. Wananchi wanazikumbuka na wanawakumbuka watuhumiwa.

Tumaini la CCM yetu ni NEC ya Jaji Damian Lubuva. NEC inategemewa kufanya mambo ili uchaguzi wa Oktoba uote mbawa. CCM ipate muda wa kujipanga. Ipate ushindi. Lakini,hakuna dalili za NEC kuiponya au kuipunguzia maumivu CCM. Itapambana hivyohivyo!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Back
Top Bottom