VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,140
- 18,004
Katika siku za hivi karibuni, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara Mwigulu Nchemba amekuwa akitembea katika kila kona ya nchi ya Tanzania na mfuasi mwenzetu wa CCM aitwaye Tesha. Mfuasi huyu anadaiwa (hasa na Mwigulu) kumwagiwa tindikali na wafuasi wa CHADEMA wakati wa harakati za Uchaguzi Mdogo wa Ubunge Jimbo la Igunga.
[COLOR=#000000 [B]Mwigulu Nchemba[/B] ameshazunguka sehemu mbalimbali akiwa naTesha-wa-Igunga. Mwigulu anaomba uungwaji mkono wa watanzania kupitia mhanga huyu wa tindikali. Ni hivi katibuni tu Mwigulu Nchemba alikuwa na Tesha-wa -Igunga katika Kampeni za uchaguzi za Udiwani wa Arusha.[/COLOR]
Nia hasa ya Mwigulu Nchemba ya kutembea na kuutangazia umma kuwa Tesha-wa-Igunga amemwagiwa tindikali na CHADEMA na kuwa kama alivyo sasa ilikuwa ni kupaka matope CHADEMA na kuonesha chama hicho kama chama cha unyama na hakifai kuaminiwa na kuungwa mkono na watanzania.
Nia nyingine ni kuanzisha kesi dhidi ya CHADEMA. Hili sasa linafanywa na Polisi na Kurugenzi ya Mashtaka. Lakini,vyombo hivi vya kisheria vilikuwa wapi tangu uchaguzi wa Igunga hadi Mwigulu Nchemba alipoanza kutembeana Tesha-wa-Igunga? Vipi kuhusu Saed Kubenea na Ndimara Tegambwage waliomwagiwa Tindikali hata kabla ya Tesha-wa-Igunga? Nani alizunguka nao? Wao hawana thamani?
Siasa ni hoja,sera na ushawishi.Si vinginevyo. Ushindi wa mezani umepitwa na wakati. Si kila mtu anafurahia ‘kunyanyaswa' kwa CHADEMA.Wengine wanaona huruma na kuona kuwa chema kinakatazwa kisiwasaidie watanzania.
Tesha-wa-Igunga hataisaidia chochote CCM yetu zaidi ya kupandikiza umakini wa kutenda,KUCHUNGUZA na kusema kwa CHADEMA. CCM,katika hali hii,haitabaki salama.Italindwa,itatumikiwa lakini ipo siku itasalitiwa na kukimbiwa.
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
[COLOR=#000000 [B]Mwigulu Nchemba[/B] ameshazunguka sehemu mbalimbali akiwa naTesha-wa-Igunga. Mwigulu anaomba uungwaji mkono wa watanzania kupitia mhanga huyu wa tindikali. Ni hivi katibuni tu Mwigulu Nchemba alikuwa na Tesha-wa -Igunga katika Kampeni za uchaguzi za Udiwani wa Arusha.[/COLOR]
Nia hasa ya Mwigulu Nchemba ya kutembea na kuutangazia umma kuwa Tesha-wa-Igunga amemwagiwa tindikali na CHADEMA na kuwa kama alivyo sasa ilikuwa ni kupaka matope CHADEMA na kuonesha chama hicho kama chama cha unyama na hakifai kuaminiwa na kuungwa mkono na watanzania.
Nia nyingine ni kuanzisha kesi dhidi ya CHADEMA. Hili sasa linafanywa na Polisi na Kurugenzi ya Mashtaka. Lakini,vyombo hivi vya kisheria vilikuwa wapi tangu uchaguzi wa Igunga hadi Mwigulu Nchemba alipoanza kutembeana Tesha-wa-Igunga? Vipi kuhusu Saed Kubenea na Ndimara Tegambwage waliomwagiwa Tindikali hata kabla ya Tesha-wa-Igunga? Nani alizunguka nao? Wao hawana thamani?
Siasa ni hoja,sera na ushawishi.Si vinginevyo. Ushindi wa mezani umepitwa na wakati. Si kila mtu anafurahia ‘kunyanyaswa' kwa CHADEMA.Wengine wanaona huruma na kuona kuwa chema kinakatazwa kisiwasaidie watanzania.
Tesha-wa-Igunga hataisaidia chochote CCM yetu zaidi ya kupandikiza umakini wa kutenda,KUCHUNGUZA na kusema kwa CHADEMA. CCM,katika hali hii,haitabaki salama.Italindwa,itatumikiwa lakini ipo siku itasalitiwa na kukimbiwa.
Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam