CCM, Chadema wachapana makonde mbele ya waziri

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,318
33,125
Nahodha%201(16).jpg

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamshi Vuai Nahodha


Ziara ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamshi Vuai Nahodha, imekumbwa na vurugu mjini hapa Wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya kufuatia vijana wanaosadikika kuwa ni wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuupokea msafara wake kwa bendera za chama hicho huku wakionyesha alama ya vidole viwili.
Kutokana na hali hiyo, vijana wa Cham Cha Mapinduzi (CCM) (mabaunsa) waliamua kujibu mapigo kwa kuanza kutembeza mkong’oto wa nguvu kwa vijana wa Chadema hivyo kusababisha amani kutoweka kwa muda mfupi katika eneo hilo.
Tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 3:45 asubuhi katika eneo la njia panda ya kuingia forodhani na barabara kuu iendayo Sumbawanga wakati msafara wa waziri huyo ukielekea katika hoteli ya Al-Noor ambako alikwenda kwa ajili ya kusomewa taarifa ya Wilaya ya Mbozi.
Baada ya msafara wa magari ya viongozi wa CCM, Polisi na Uhamiaji waliofuatana na waziri huyo kuingia mjini Tunduma vijana waliokuwa wamejipanga pembeni mwa barabara walianza kuzomea huku wakionyesha alama ya vidole viwili inayotumiwa na Chadema, mmoja wa vijana hao alikuwa na bendera moja ya chama hicho akipeperusha juu.
Kufuatia hali hiyo, vijana wa CCM ambao waliokuwa wamevalia fulana nyeupe zilizoandikwa mgongoni CCM Imara waliwavamia vijana wa Chadema waliokuwa wakizomea msafara huo na kumkamata kijana mmoja aliyekuwa na bendera hiyo na kuanza kumpa kipigo.
Baada ya vurugu hizo ambazo zilidumu kwa takribani dakika kumi, polisi waliokuwa wakilinda usalama wa msafara wa Waziri huyo waliingilia kati kwa kumtia nguvuni kijana aliyekuwa akipewa kipigo na vijana wa CCM ili kuokoa maisha yake ambayo yalikuwa hatarini na kumpeleka katika Kituo cha Polisi Tunduma.
Kijana huyo ambaye jina lake halikuweza kujulikana mara moja wakati akipigwa na mabaunsa wa CCM, alichaniwa nguo zake huku akibebwa juu juu. Baada ya kufikishwa kituo cha polisi vurugu hizo zilisimama na polisi kutanda barabara yote kuanzia hoteli ya Al-Noor hadi ofisi za CCM kata ya Tunduma.
Waziri Nahodha akizungumza na wananchi katika viwanja vya CCM Kata ya Tunduma, alisema hajafurahishwa na vurugu zilizotokea na kuwaagiza askari chini ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Advocate Nyombi, kuimarisha ulinzi katika mji wa Tunduma.
Alisema wafanyabiashara wa soko mjini Tunduma wafanye biashara zao kwa amani kwa sababu biashara inayofanywa kwa amani inakuwa na tija.
“Lipo jambo ambalo sikulipendelea sana leo (jana) wakati napita niliona hali ya utulivu siyo nzuri, nikiwa kama waziri mwenye dhamana siwezi kuona hali hii ikiendelea, naomba askari chini ya RPC (kamanda wa polisi mkoa) imarisheni ulinzi haraka,” alisema Nahodha.
Alisema mji huo unatakiwa kuimarishwa ulinzi kwani zinafanyika biashara za aina mbalimbali za halali na haramu na kuna mkusanyiko wa watu kutoka nchi mbalimbali.
Alisema wale wanaofanya biashara haramu watambue kuwa sasa likizo imekwisha, hivyo polisi wachukue hatua haraka kuanzia jana kwa kuimarisha ulinzi.
Aliongeza kuwa wale wanaofanya biashara halali wasibughudhiwe waachwe waendelee kufanya kazi zao kwa utulivu na wale wanaofanya biashara ya kubadilisha fedha Benki Kuu ya Tanzania (BoT) iwawekee utaratibu mzuri ili kusitokee wizi wa watu kuibiwa fedha zao.
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Tunduma, Daniel Mwashuya, alisema mji huo ulishikandikana kuwa na amani, lakini sasa imewezekana kwani ndani ya chama wamejipanga kusaidia kuiimarisha.
“Tunduma sasa ni safi, wana Tunduma wanataka amani, hawa wanaoleta vurugu katika mji wetu tutawaminya kwa ukucha, tunawaweza na kwa tukio la leo wengine wametimkia mabondeni,” alisema Mwashuya.
Mji huo ambao upo mpakani kwa mara kadhaa umekuwa ukikubwa na vurugu zisizoisha hali ambayo imekuwa ikiharatisha usalama wa wakazi wake. Mara kadhaa wanaofanya vurugu hizo wamekuwa wakikimbilia upande wa pili wa nchi jirani ya Zambia.
Akizungumzia kijana wa Chadema aliyekamatwa, Kamanda Nyombi alisema kuwa alipelekwa katika kituo cha Polisi cha Tunduma, ingawa hakueleza sababu za kukamatwa kwake.



CHANZO: NIPASHE
 
Hivi ni kwa nini waliokuwa wanampiga huyo kijana nao hawakukamatwa? Nasema hivyo kwa sababu naona waliamua kuchukua sheria mkononi na kwa mujibu wa sheria za nchi yetu, hilo nalo ni kosa.
 
Kwa mujibu wa habari hii:

1 - Kwa nini mabaunsa wafanye kazi ya ulinzi wakati polisi walikuwepo?

2 - Ni kosa la kisheria kwa raia mmoja kumpiga raia mwingine au raia kupigana. Kwa nini aliyepelekwa kituoni ni kijana aliyepigwa na si waliompiga?

3 - Ukiangalia utaona kuwa hata waziri hafahamu utawala wa sheria; badala ya kuamuru wote waliohusika wakamatwe kwa mujibu wa sheria anabakia "kuomba" polisi waimarishe ulinzi haraka. Sheria inapovunjwa hakuna maombi, ni amri tu, ndiyo maana polisi wanaitwa law enforcers.

4 - Yaleyale ya kila siku, ziara ya kiserikali halafu wananchi wanaipaka rangi ya siasa na kiongozi mhusika anaangalia tu, bila ya kujua nini cha kufanya.
 
Huyo kijana wa CDM hana kosa. Hao mabaunsa wa magamba ndio walioanzisha hizo vururgu.
 
huyo waziri atakua anafanya kazi za ccm sio za watanzania. hajui kama chadema ni chama cha siasa kama ilivyo ccm? kwanini abague? wazanzibar wana matatizo sana.
 
Matatizo ya uvunjifu wa amani huanzishwa na mawaziri wenyewe kama waziri yupo kikazi kwanini misafara yao inapabwa na magari yenye bendera za ccm pia mabaunsa wenye mavazi ya ccm. Kama ni waziri wa JMT kwanini kwa nini msafara wake hauwi na ulinzi wa polisi? Ccm wanajua kabisa tunduma chadema wanawafuasi wengi na ni vijana kwahiyo waziri kwenda kwenye shughuri za kiserikali na vijana wengi wa ccm ambao si wakazi wa tunduma haikuwa sahihi.
 
Ccm na magamba wapo kupima kina cha maji ya mbeya " nawaambia mbeya maji marefu wachezee wadalisalama basi"
 
Nadhani Masisiem wote wana upungufu wa ufahamu mwilini mwao! kwa nini hawawezi kutofautisha shughuli za kiserikali na za kichama? unaweza kukuta huyo nahodha alikuwa amevalia kijani!!!!
 
wajiandae wasio mabaunsa, tukio hilo litazaa uhasama mkubwa kwani limewaudhi vijana.
 
Nadhani Masisiem wote wana upungufu wa ufahamu mwilini mwao! kwa nini hawawezi kutofautisha shughuli za kiserikali na za kichama? unaweza kukuta huyo nahodha alikuwa amevalia kijani!!!!

Siyo kuvaa tu kijani bali alikuwa akitumia magari ya serikali kwenye shughuli za chama
 
Akili ya panzi kabisa,siku hizi waziri yuko kwenye ziara za kiserikali anatembea na mabaunsa wa CCM,hapo kilichofanyika ni kupandikiza chuki,hata mm nimechukizwa na kitendo cha huyo dogo kupigwa pasipo sababu,ni uonevu huo,ni hali ya kujidai kuwa CCM wako juu ya sheria,ole wenu nyie CCM na ufisadi wenu,hakika Mungu hajala,na siku zenu zinahesabika
 
Mara kadhaa nimeongolea jambo la viongozi wa serikali na vyama vya siasa kutofautisha shughuli za kichama na kiserikali zinazohusu watanzania wote. Mlinirushia madongo na hasa wapenzi wa Chadema kwa kutoangalia athari zake. Lisemwalo lipo na kama halipo laja. Leo tunaanza kushuhudia athari zake. Ziara ya waziri huyo ni ya kiserikali au ya kichama? Iweje watu waendekeze uchama katika ziara hiyo? Je waziri ametambu kasiro na yaliyosababisha vurugu hizo?
 
Mara kadhaa nimeongolea jambo la viongozi wa serikali na vyama vya siasa kutofautisha shughuli za kichama na kiserikali zinazohusu watanzania wote. Mlinirushia madongo na hasa wapenzi wa Chadema kwa kutoangalia athari zake. Lisemwalo lipo na kama halipo laja. Leo tunaanza kushuhudia athari zake. Ziara ya waziri huyo ni ya kiserikali au ya kichama? Iweje watu waendekeze uchama katika ziara hiyo? Je waziri ametambu kasiro na yaliyosababisha vurugu hizo?

Mkuu, nani alikurushia madongo mbona point hiyo iko wazi kabisa? Chaguzi nyingi zinahojiwa kwa sababu viongozi ama walitumia madaraka ya au walitumia mali ya umma (magari ya serikali) kwa shughuli za uchaguzi.
 
Kwa mujibu wa habari hii:

1 - Kwa nini mabaunsa wafanye kazi ya ulinzi wakati polisi walikuwepo?

2 - Ni kosa la kisheria kwa raia mmoja kumpiga raia mwingine au raia kupigana. Kwa nini aliyepelekwa kituoni ni kijana aliyepigwa na si waliompiga?

3 - Ukiangalia utaona kuwa hata waziri hafahamu utawala wa sheria; badala ya kuamuru wote waliohusika wakamatwe kwa mujibu wa sheria anabakia "kuomba" polisi waimarishe ulinzi haraka. Sheria inapovunjwa hakuna maombi, ni amri tu, ndiyo maana polisi wanaitwa law enforcers.

4 - Yaleyale ya kila siku, ziara ya kiserikali halafu wananchi wanaipaka rangi ya siasa na kiongozi mhusika anaangalia tu, bila ya kujua nini cha kufanya.

Nilivyoelewa hapo ni kwamba. Polisi walimchukua huyo jamaa kwa ajili ya kuokoa maisha yake kutoka kwa wapigaji na si kama mtuhumiwa.
 
chadema ni chama cha wahuni,kwa nini wamzomee kiongozi?ustaarabu ni muhimu,ona sasa yaliyompata.
 
Back
Top Bottom