CCM Arusha yampigia magoti mfanyabiashara Thomasi Munis, Mbio za Ubunge

Arusha Leo

Senior Member
Mar 12, 2012
122
72
CHAMA cha Mapinduzi ccm jimbo la Arusha mjini ,kimeanza mchakato wa kusaka
mgombea ubunge kijana mwenye uwezo wa kuchuana na mbunge wa sasa Godbles Lema,,baada ya kubainika kuwa
kuwa walioonyesha nia hadi sasa hakuna mwenye mvuto wa kumng'oa
waliooneysha nia hadi sasa niwazee.

Taarifa zilizothibitishwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho jijini
hapa,baada ya kufanyika kikao cha siri kujadili wagombea wa chama
hicho walioonyesha nia,zimedai kuwa ni lazima chama kishawishi ili
kupata mgombea aliyebora.

''Ni kweli viongozi wamepeana mkakati wa kusaka mgombea kijana
,machachari mwenye mvuto kwa wananchi ambaye ataweza kupambana na Lema
''alisema kada maarufu ambaye alidai si msemeji wa chama.

Katibu wa wilaya ,Feruzi Benno alisema alikiri kuwepo kwa mkakati wa
kumng'oa Lema nafasi ya ubunge,ila alisema chama kinataratibu zake na
ni mapema sana kuianika hadharani kwani kwa sasa.

''Nikweli lazima tuwe na mgombea mwenye sifa anayekubalika na wananchi
na tunaangalia mahitaji ya wananchi wa Arusha ni nini ,kwa sasa tuna
taratibu zetu na si lazima kila mtu azijue ,tulieni wakati ukifika
mtaona''alisema Benno.

Habari za kuaminika zinadai kuwa tayari chama hicho kimeanza ushawishi
kwa mfanyabiashara maarufu wa madini jijini hapa,Thomas Munis
kikimtaka achukue fomu ya kuwania ubunge wakati ukifika.

Hata hivyo Munisi alikiri kufanya mazungumzo na makada wa chama hicho
na kuwaahidi kuwajibu baada ya kukaa chini na kufikiria.

''Nikweli baadhi ya viongozi walikuja na kiniomba nigombee ubunge
Arusha mjini ,ila kwa sasa nafikiria kwanza sikuweza kuwajibu moja kwa
moja si unajua mambo ya siasa yalivyo kuwa magumu ila nitawajibu
soon''alisema Munisi

Hadi sasa walionyesha nia ya kuwania nafasi ya ubunge kupitia chama
hicho jimbo la Arusha mjini wamefika 9,akiwemo mfanyabiashara Philemon
Mollel , wakili wa kujitengemea Vicktas Njau,dkta Anold Andason ,Deo
Mtui na mtanzania mwenye asili ya kiasia aliyefanamika kwa jina la
Panju.
 
CHADEMA will run Arusha Town forever,we believe in UKAWA,and CHADEMA,Arusha bila LEMA haiwezekani,endeleeni kuota ndoto za mchana,maCCM mtamaliza pesa zenu bure!
 
Duu siasa ngumu hivi ni kweli Leo hii ccm imeanza kutafuta wagombea kwa tochi.?Ni hatari lakini Salama.
 
Haaa haaa yaani ni shedaaa mwaka huu.Munis mwenye utadhani anauzika hana lolote zaidi ya kujaza makaratasi kwenye pochi,kuvaa suruali chini ya makalio.........
 
Mmh Mbona Munis Na Kim Ni Ndugu Na Lema Ccm Ipo Mashakani Kupotea Arusha Kabisa Machale Kundesa
 
ni vigumu kupenya katika tundu la sindano awe munis au nani ,siasa za arusha zimebadilika sana ,ukitaja ccm umetonesha kidonda .
 
Alafu kuna mafara wanapita wakichafua kuta na ma spray eti "Raisi Mwigulu, Mbunge Lema"
Wamechora hadi na karibu na central Police kwenye ukuta wa Meru primary.
Hawa jamaa ni wa kushika na kuchapa viboko kisha wapige kuta zote rangi.
 
CHAMA cha Mapinduzi ccm jimbo la Arusha,,kimeanza mchakato wa kusaka mgombea ubunge kijana atakayechuana na mbunge wa sasa godbless Lema.

Aidha tayari mfanyabiashara wa madini ya Tanzanite Thomas Munis, anatajwa katika kinyang'anyiro hicho baada kuonekana walioonyesha nia hadi sasa ni wazee na hawana mvutoka kwa siasa za Arusha

Taarifa zilizothibitishwa na baadhi ya viongozi wa chama hicho jijini hapa,baada ya kufanyika kikao cha siri kujadili wagombea wa chama hicho walioonyesha nia,zimedai kuwa ni lazima chama kishawishi ili kupata mgombea aliyebora.

‘’Ni kweli viongozi wamepeana mkakati wa kusaka mgombea kijana ,machachari mwenye mvuto kwa wananchi ambaye ataweza kupambana na Lema ‘’alisema kada maarufu ambaye alidai si msemeji wa chama.

Katibu wa wilaya ,Feruzi Benno alisema alikiri kuwepo kwa mkakati wa kumng’oa Lema nafasi ya ubunge,ila alisema chama kinataratibu zake na ni mapema sana kuianika hadharani kwani kwa sasa.

‘’Nikweli lazima tuwe na mgombea mwenye sifa anayekubalika na wananchi na tunaangalia mahitaji ya wananchi wa Arusha ni nini ,kwa sasa tuna taratibu zetu na si lazima kila mtu azijue ,tulieni wakati ukifika mtaona’’alisema Benno.

Habari za kuaminika zinadai kuwa tayari chama hicho kimeanza ushawishi kwa mfanyabiashara maarufu wa madini jijini hapa,Thomas Munis,kikimtaka achukue fomu ya kuwania ubunge wakati ukifika.

Hata hivyo Munisi alikiri kufanya mazungumzo na makada wa chama hicho na kuwaahidi kuwajibu baada ya kukaa chini na kufikiria.

‘’Nikweli baadhi ya viongozi walikuja na kiniomba nigombee ubunge Arusha mjini ,ila kwa sasa nafikiria kwanza sikuweza kuwajibu moja kwa moja si unajua mambo ya siasa yalivyo kuwa magumu ila nitawajibu soon’’alisema Munisi

Hadi sasa walionyesha nia ya kuwania nafasi ya ubunge kupitia chama hicho jimbo la Arusha mjini wamefika 9,akiwemo mfanyabiashara Philemon Mollel , wakili wa kujitengemea Vicktas Njau,dkta Anold Andason ,Deo
Mtui na mtanzania mwenye asili ya kiasia aliyefanamika kwa jina la Mohamed Panju.
 
ubaya wa ccm badala ya kuangalia mtu mwenye uwezo wa kuongoza na kusimamia na kutetea wananchi wao wanaangalia mtu mwenye fedha. ndio maana wanaanza na kusema mfanyabiashara wa madini,ccm bado wana siasa za zamani sana kuona kwamba kuwa na fedha ndio dili ya kuchaguliwa, wameshindwa kabisa kujiuliza kwa nini Nasari alichaguliwa na kwa nini Lema alichaguliwa
 
ubaya wa ccm badala ya kuangalia mtu mwenye uwezo wa kuongoza na kusimamia na kutetea wananchi wao wanaangalia mtu mwenye fedha. ndio maana wanaanza na kusema mfanyabiashara wa madini,ccm bado wana siasa za zamani sana kuona kwamba kuwa na fedha ndio dili ya kuchaguliwa, wameshindwa kabisa kujiuliza kwa nini Nasari alichaguliwa na kwa nini Lema alichaguliwa

Kugombea uongozi ccm lazima uwe na fweza.
 
ccm watamlia pesa zake zote na hata back na sent cheza na ccm wewe.

swissme
 
Munis hawezi kupambana na Lema... Mizimu itamrudi ... CCM kurudi Arusha ni Ndoto za Mchana wa Jua kali ...
 
Back
Top Bottom