CCM Arusha: Lema amelipotosha bunge kuhusu Arusha

CCM Arusha: Lema amelipotosha bunge kuhusu Arusha

aminangalo

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2013
Posts
974
Reaction score
190
CCM Arusha Leo wahitimisha ziara ya kutembelea kata zote za Arusha Mjini kukagua ilani ya uchaguzi ambapo pia wamefanya mikutano ya hadhara

Mikutano hiyo iliyoongozwa na MWENYEKITI Wa CCM wilaya DK SOILELI imekuwa namwitikio mkubwa haswa baada ya kupokea wanachama wengi Wa CHADEMA Kama Kata ya UNGA LTD MWENYEKITI na katibu Wa CHADEMA na kurudi CCM

Leo katika kata ya Ngarenaro mwenyekiti Wa vijana Wa CCM wilaya ya Arusha Mjini amemwinya LEMA kuacha kuwaongopea wajumbe Wa bunge LA katiba kuwa msimamo Wa wana Arusha ni serikali mbili na siyo tatu tatu ni za kwake yeye siyo za wanaarusha

Yeyote atakaye dhubutu kuichezea amani yetu watanzania Uvccm tutamshughulikia kikamilifu

Alimalizia kwa kuwaomba wana Arusha kuikataa CHADEMA maana wameharibu Mjini na kuwafanya watalii wasije Arusha uchumi kuporomoka kisa maandamano na mabomu ya CHADEMA

Mkataeni lema na chadema yake alimalizia mwenyekit huyo
 
Wana ARUSHA tumeshaikataa CHADEMA na mambo yake yote! Huyu LEMA tunasubiria uchaguzi tu ili tumrudishe kwao Machame.
 
mbona unaandika mwenyewe kila kitu? unajiuliza swali na kujipa majibu.
kama lema aliyechaguliwa kwa kura nyingi na watu unasema msimamo wake si wa wana arusha, ww unapata wapi mamlaka ya kusema kuwa arusha wanataka serikali 3.
 
...

.....Arusha ya zizima Hotuba ya G LEMA yatikisa jiji la Arusha !!!


Hapa chini UKAWA inachanja mbuga huko IRINGA...

attachment.php


attachment.php

attachment.php
 
mbona unaandika mwenyewe kila kitu? unajiuliza swali na kujipa majibu.
kama lema aliyechaguliwa kwa kura nyingi na watu unasema msimamo wake si wa wana arusha, ww unapata wapi mamlaka ya kusema kuwa arusha wanataka serikali 3.

Naona umeshaa piga kitu ya karatasi amko tatu ni za lema labda na wifi yetu ila Arusha ni mbili tuuu basi
 
na wewe unalipotosha jukwaa. Arusha na Lema wetu msituambie lolote.. wameshndwa akina mwigulu, mkapa, kinana na makamu wa rais. Watakuwa hao vifaranga uvccm ndo uwaweke washndane na lema?

Walishindwa lini hao viongozi wetu???
 
Na huyo Soileli ni nani kamwambia Arusha wanataka Serikali 2?

Maoni ya wananchi ni Serikali 3,so Lema anatuwakilisha vyema.

Ziara ya kutembelea kata zipi? Mbona Kimandolu na Baraa hatujawaona?

Hiyo ziara itakuwa iliishia ktk Mirungi mtaa wa Makaburi ya Baniani Unga ltd kwa diwani wa Magamba Issa.
 
CCM Arusha Leo wahitimisha ziara ya kutembelea kata zote za Arusha Mjini kukagua ilani ya uchaguzi ambapo pia wamefanya mikutano ya hadhara

Mikutano hiyo iliyoongozwa na MWENYEKITI Wa CCM wilaya DK SOILELI imekuwa namwitikio mkubwa haswa baada ya kupokea wanachama wengi Wa CHADEMA Kama Kata ya UNGA LTD MWENYEKITI na katibu Wa CHADEMA na kurudi CCM

Leo katika kata ya Ngarenaro mwenyekiti Wa vijana Wa CCM wilaya ya Arusha Mjini amemwinya LEMA kuacha kuwaongopea wajumbe Wa bunge LA katiba kuwa msimamo Wa wana Arusha ni serikali mbili na siyo tatu tatu ni za kwake yeye siyo za wanaarusha

Yeyote atakaye dhubutu kuichezea amani yetu watanzania Uvccm tutamshughulikia kikamilifu

Alimalizia kwa kuwaomba wana Arusha kuikataa CHADEMA maana wameharibu Mjini na kuwafanya watalii wasije Arusha uchumi kuporomoka kisa maandamano na mabomu ya CHADEMA

Mkataeni lema na chadema yake alimalizia mwenyekit huyo


Kwa hiyo, kwa kutumia akili ndogo tu, nani hapo ndiyo wa maana na mkweli? Ni Godblee Lema ambaye amechaguliwa kwa kura za kutosha kuwa mbunge wa Arusha Mjini au Mwenyekiti wa vijana wa chama kilichoshindwa uchaguzi? Au mnaonaje kwamba hata hao wananchi walioichagua CHADEMA na kuipa viti karibu vyote vya udiwani siyo sehemu ya Arusha? Au UVCCM Arusha nayo ina mamlaka ya kuwasemea na hao, tofauti na kura zinavyosema?

Ni kweli kuwa CCM ni mpaka uwe na kasoro kichwani! Hivi kati ya CCM na CHADEMA nani ndiyo chanzo cha mabomu ya Arusha? Kama siyo upuuzi wa serikali ya CCM kulazimisha ushindi na kunyanyasa upinzani nani angekufa Arusha? Acheni kulazimisha maoni hata pale mnapojua wananchi wana maoni tofauti. Lema kwa sasa ni sauti ya Wana Arusha. Mpaka atakapopewa ubunge mtu mwingine, ni busara mkamheshimu na kushirikiana naye kufanya maendeleo ya Arusha.

Nadhani pia kunatakiwa kuwe na muda wa kampeni na muda wa kujenga nchi. Kwa ninavyokumbuka, muda wa kampeni umepita. Hebu waacheni wana Arusha wajenge Arusha yao.
 
Back
Top Bottom