baraka boki
Senior Member
- Sep 20, 2010
- 181
- 80
na David Frank, Arusha
MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Arusha (UV-CCM), James Millya, ni miongoni mwa watakaohojiwa leo na Kamati ya Usalama na Maadili ya Mkoa kufuatia mgogoro unaofukuta kati ya makundi mawili ya vijana hao kuhusu falsafa mpya ya Kujivua Gamba kwa wanachama wa ngazi ya juu wa CCM.
Wakati kundi jingine likitaka wanachama hao ambao ni aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa; Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge; na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, wajivue gamba kundi jingine linapinga uamuzi huo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana ndani ya chama hicho mkoa na kuthibitishwa na Katibu wa CCM Mkoa, Mary Chatanda, zinaeleza kuwa mbali na mwenyekiti huyo pia wajumbe wa kamati ya utekelezaji ya UV-CCM mkoa nao watahojiwa sambamba na wanachama walioshiriki katika maandamano yaliyofanyika hivi karibuni.
Katika madai yao waandamanaji hao kutoka wilaya zote mkoani hapa ambazo ni pamoja na Arusha Mjini, Monduli, Arumeru, Longido, Ngorongoro na Karatu, walikuwa wakishinikiza katibu huyo aachie ngazi kwa madai ya kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kusababisha majimbo mawili ya uchaguzi ya Arusha Mjini na Karatu kuchukuliwa na wapinzani.
Mbali na majmbo hayo pia walidai kuwa kushindwa uchaguzi katika baadhi ya maeneo kulisababishwa na katibu huyo, wakimtuhumu kufanya kazi kibabe na zaidi ya hayo anaingilia kazi za jumuia hiyo.
Katika kikao hicho kitakachokuwa chini ya Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha, Onesmo Nangole, baadhi ya watakaohojiwa walidai kuwa kina lengo la kuwatisha kufukuzwa uanachama.
Wakizungumza na gazeti hili, miongoni mwa watakohojiwa leo walilalamika na kuhoji ni vipi wao wawekwe kiti moto huku kundi lingine la vijana hao waliofanya maandamano kama hayo likiachwa.
Nashindwa kuelewa ni vipi kundi lililoandamana na kutoa matamko mazito dhidi ya viongozi wa ngazi za juu liachwe bila kuwekwa kiti moto na kuwataka vijana wa upande mmoja kuhojiwa peke yao.
Tunajua lengo la kikao cha leo ni kututisha tuache dhamira yetu ambayo tutaendelea nayo hadi kieleweke, alisema mmoja wa vijana hao.
Katika siku za hivi karibuni makundi mawili ya vijana mkoani hapa yamekuwa yakisigana na kulumbana huku kila moja likielezea hisia zake juu ya mustakabali wa falsafa mpya ya Kuvua Gamba.
Wakati moja likipinga hatua hiyo na lingine linasisitiza watuhumiwa wote wanaodaiwa kuhusika na tuhuma za ufisadi wangolewa kwa lengo la kusafisha chama.
Kadhalika ilidaiwa kuwa watuhumiwa wa ufisadi walikifanya Chama cha Mapinduzi kukosa mvuto mbele ya Watanzania katika uchaguzi mkuu uliopita na kusababisha majimbo mengi nchini kunyakuliwa na wapinzani katika nafasi ya ubunge na udiwani.
MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Arusha (UV-CCM), James Millya, ni miongoni mwa watakaohojiwa leo na Kamati ya Usalama na Maadili ya Mkoa kufuatia mgogoro unaofukuta kati ya makundi mawili ya vijana hao kuhusu falsafa mpya ya Kujivua Gamba kwa wanachama wa ngazi ya juu wa CCM.
Wakati kundi jingine likitaka wanachama hao ambao ni aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa; Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge; na Mbunge wa Igunga, Rostam Aziz, wajivue gamba kundi jingine linapinga uamuzi huo.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana ndani ya chama hicho mkoa na kuthibitishwa na Katibu wa CCM Mkoa, Mary Chatanda, zinaeleza kuwa mbali na mwenyekiti huyo pia wajumbe wa kamati ya utekelezaji ya UV-CCM mkoa nao watahojiwa sambamba na wanachama walioshiriki katika maandamano yaliyofanyika hivi karibuni.
Katika madai yao waandamanaji hao kutoka wilaya zote mkoani hapa ambazo ni pamoja na Arusha Mjini, Monduli, Arumeru, Longido, Ngorongoro na Karatu, walikuwa wakishinikiza katibu huyo aachie ngazi kwa madai ya kushindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo na kusababisha majimbo mawili ya uchaguzi ya Arusha Mjini na Karatu kuchukuliwa na wapinzani.
Mbali na majmbo hayo pia walidai kuwa kushindwa uchaguzi katika baadhi ya maeneo kulisababishwa na katibu huyo, wakimtuhumu kufanya kazi kibabe na zaidi ya hayo anaingilia kazi za jumuia hiyo.
Katika kikao hicho kitakachokuwa chini ya Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha, Onesmo Nangole, baadhi ya watakaohojiwa walidai kuwa kina lengo la kuwatisha kufukuzwa uanachama.
Wakizungumza na gazeti hili, miongoni mwa watakohojiwa leo walilalamika na kuhoji ni vipi wao wawekwe kiti moto huku kundi lingine la vijana hao waliofanya maandamano kama hayo likiachwa.
Nashindwa kuelewa ni vipi kundi lililoandamana na kutoa matamko mazito dhidi ya viongozi wa ngazi za juu liachwe bila kuwekwa kiti moto na kuwataka vijana wa upande mmoja kuhojiwa peke yao.
Tunajua lengo la kikao cha leo ni kututisha tuache dhamira yetu ambayo tutaendelea nayo hadi kieleweke, alisema mmoja wa vijana hao.
Katika siku za hivi karibuni makundi mawili ya vijana mkoani hapa yamekuwa yakisigana na kulumbana huku kila moja likielezea hisia zake juu ya mustakabali wa falsafa mpya ya Kuvua Gamba.
Wakati moja likipinga hatua hiyo na lingine linasisitiza watuhumiwa wote wanaodaiwa kuhusika na tuhuma za ufisadi wangolewa kwa lengo la kusafisha chama.
Kadhalika ilidaiwa kuwa watuhumiwa wa ufisadi walikifanya Chama cha Mapinduzi kukosa mvuto mbele ya Watanzania katika uchaguzi mkuu uliopita na kusababisha majimbo mengi nchini kunyakuliwa na wapinzani katika nafasi ya ubunge na udiwani.