CCM Acheni Utoto Huu

CCM Acheni Utoto Huu

................... Labda wampe maswali ahead of time lakini ...............
....

NN, umenikumbusha last time alipokuwa akihojiwa na Tido Mhando (puppet) pale TBC. Inaelekea yeye mwenyewe ndiye aliyeandaa maswali halafu akaanda na majibu yaliyochapishwa kwenye karatasi. maswali akampa Tido ili (Tido) amuulize JK. wakati wa kujibu akawa anasoma kwenye karatasi lake!!!! halafu waliandaliwa watu mikoani waliouliza maswali yenye majibu tayari. Wenye maswali yanayoeleweka walipokuwa wakipiga simu zilizotolewa na TBC ama line zilikuwa hazipatikani ama swali lako linasikilizwa kwanza na wapambe halafu simu inakatikika haipatikani tena mpaka kipindi kikaisha!!!
 
Kama hawezi kuelezea analotaka kuifanyia nchi hii je atafanya nini akichaguliwa? Natamani sana CCM ifutike kama ambavyo UNIP na KANU zilivyofutika baada ya kulewa madaraka.


Tumenyanyaswa kiasi cha kutosha, tumedharauliwa kiasi cha kutosha na tumepuuzwa kiasi cha kutosha. Sasa ni wakati wa kuiondoa CCM. Sababu za kuin'goa tunazo, nia ya kuin'goa tunayo na uwezo wa kuin'goa tunao. Shime wapenda maendeleo tuizike CCM.
 
Marais wote wa Marekani hufanya midahalo ipatayo mitatu au zaidi kabla ya uchaguzi; iweje rais wa Tanzania asiweze kufanya mdahalo kabla ya uchaguzi. ??

Wamarekani wanachagua kiongozi kwa kupima uzito wa hoja zake anazozijenga kuomba kura za wananchi na rekodi yake ya utendaji kazi kutimiza ahadi za kampeni. Midahalo kwa wanasiasa wa Marekani ni fursa nzuri sana kwa wagombea kujiuza na kuongeza ushawishi wao kwa wapiga kura. Kule siyo rahisi kuiba kura labda uwe na umafia wa George Bush ambaye kwa kushirikiana na mdogo wake Jeb Bush walighushi matokeo ya Florida na hatimaye akawa rais wa Marekani.

Watanzania wanaangalia pesa au takrima kama ukipenda. Mtu akiwa na pesa nyingi za kugawa kwa wapiga kura hiyo inaweza kutosha kumpa ushindi. Lakini pia kuna mbinu mbadala za kushinda kama kuiba kura, kutangaza washindwa kuwa washindi kibabe na mengine yanayofanana na hayo. Hii inaweza kukueleza kwa nini hapa kwetu wanasiasa wengine hawaoni umuhimu wa midahalo. Wanajua kuna mbinu mbadala za kushinda uchaguzi kwa nini waumize vichwa na midahalo.
 
NN, umenikumbusha last time alipokuwa akihojiwa na Tido Mhando (puppet) pale TBC. Inaelekea yeye mwenyewe ndiye aliyeandaa maswali halafu akaanda na majibu yaliyochapishwa kwenye karatasi. maswali akampa Tido ili (Tido) amuulize JK. wakati wa kujibu akawa anasoma kwenye karatasi lake!!!! halafu waliandaliwa watu mikoani waliouliza maswali yenye majibu tayari. Wenye maswali yanayoeleweka walipokuwa wakipiga simu zilizotolewa na TBC ama line zilikuwa hazipatikani ama swali lako linasikilizwa kwanza na wapambe halafu simu inakatikika haipatikani tena mpaka kipindi kikaisha!!!

Jibaba hongera. Umegusa palipokuwa pameachwa au pamesahaulika. Kweli, JK aliulizwa maswali yaliyoandaliwa na wafanyakazi wa TBC1 walikiri na wanaendelea kukiri hilo. Serekali na Tido walisahau kuwa wafanyakazi wa TBC1 wengine ni CHADEMA, CUF etc wakadhani kuwa watakaa kimya. Poor plan.

Kama haitoshi, utakumbuka Tido aliuliza swali kuhusu shule za kata kama nakumbuka sawasawa, JK alishindwa kilijibu maana Tido alichomekea halikuwa kwenye agenda na ndio sababu ya Tido kutoswa Tbc1. Sasa hivi ameongezewa some months hadi december ili asirudi BBC amwage mboga wakati wa uchaguzi

Lol.....Tumshukuru Mungu kwa kutuletea Mkombozi. Malaria sugu na wengine ni wanachama na makada wa CCM lakini malaria sugu anatishet, kadi ni na simu yake anatumia mlio wa Chadema. See? Asante MAlaria sugu wetu. Kizuri ni kuwa madaktari wa Muhimbili wamesema malundo ya mbu walio Mh2 hawasababishi malaria, sijui ndio kumwambia JK kuwa Nchi bila Malaria inawezekana...?

Napenda nchi yangu, naipenda TBC kama mwajiri wangu lakini wafanyakazi tumezarauliwa vya kutosha....tukapige kura wote bila kusita
 
MWEZI OCTOBER NI MWEZI AMBAO MBIVU NA MBICHI ZITAJULIKANA........WAFUASI WA VYAMA MBALIMBALI KADRI WALIVYOJIANDAA WASITAFUTE VISINGIZIO PINDI MATOKEO YATAKAPOTANGAZWA............sababu za wizi wa kura,masanduku kuchelewa kufika,kura kuharibika n.k zitakuwa zimepita KAMA MMEJIANDAA VYEMA NAJUA MMETAFUTA MBINU ZA KUDHIBITI YOTE HAYO..........TUTAKUJA NA SABABU GANI TENA? PINDI MATOKEO YATANGAZWAPO?

You have a point Mahesabu.

Kama wapinzani hawataandaa mbinu hivi sasa za kudhibiti wizi wa kura na udanganyifu mwingineo ambao wote tunajua kuwa utakuwepo wakati wa uchaguzi mwezi October 2010, basi hawatakuwa na sababu za kulalama kuwa wameibiwa kura. Wakilalama kila mtu atajua kuwa ni maumivu ya kushindwa tu.

Inabidi maandalizi ya wapinzani yawe ni pamoja na jinsi ya kudhibiti wizi wa kura na udanganyifu mwingineo.
 
Mbona tumeiga kupiga kura?...niambie hii ni mila ya kabila gani kati ya 120 tulonayo?.......hata hicho cheo cha urais ni cha kabila gani?(neno lenyewe la kiarabu)
hahahaha!! gud answer! au katiba ni utamaduni wa wazaramo? atuambie!!
 
NN, umenikumbusha last time alipokuwa akihojiwa na Tido Mhando (puppet) pale TBC. Inaelekea yeye mwenyewe ndiye aliyeandaa maswali halafu akaanda na majibu yaliyochapishwa kwenye karatasi. maswali akampa Tido ili (Tido) amuulize JK. wakati wa kujibu akawa anasoma kwenye karatasi lake!!!! halafu waliandaliwa watu mikoani waliouliza maswali yenye majibu tayari. Wenye maswali yanayoeleweka walipokuwa wakipiga simu zilizotolewa na TBC ama line zilikuwa hazipatikani ama swali lako linasikilizwa kwanza na wapambe halafu simu inakatikika haipatikani tena mpaka kipindi kikaisha!!!

Wait a minute. Hatukumchagua rais kwa kigezo cha kuwa bingwa wa kujenga na kubomoa hoja kwenye midahalo. Wala hatukumchagua kwa sababu ana IQ kubwa sana kuliko washindani wenzake. Ukweli ni kwamba hata mdahalo wa wagombea aliukataa. Sababu kubwa ilikuwa ni kwamba anachagulika, mara ni kijana, na wengine wakadai ni chaguo la mungu kwa vigezo gani sijui na ni mungu yupi sijui pia. Na kweli alichagulika kwa kishindo. Hayo mengine mnamuonea bure.
 
Kama unakumbuka mwaka jana au mwaka juzi mwishoni kwenye ule mkutano wa TED uliofanyikia Arusha. Jamaa alishiriki majadiliano yaliyokuwa moderated na Isha Sessay....yaani alikuwa anahangaika kutafuta cha kujibu hadi nikamwonea huruma.
.

Mkuu NN naikumbuka ile siku yule dada wa CNN alipomtoa jasho mkulu wa kaya, huku Mkulo akitamani kuingia chini ya meza kujificha asiulizwe.
 
Mdahalo mara nyingi kwenye kipindi cha uchaguzi huwa ndio chombo muhimu cha kuwaelimisha wapiga kura tofauti za kisera baina ya vyama vyenye kuwania uongozi. Na Siasa zenye midahalo ni nchi ambazo zipo kwenye 'liberal democracies' ambazo serikali inawajibu kwenye almost every sector of the economy, welfare, health, education foreign policies na kadhalika.

Sisi sijui tunahitaji mdahalo wa nini kujua kwamba kuna utovu wa nidhammu wa hali ya juu katika serikali yetu. Kwanza amna maendeleo, mawaziri wasio heshimu katiba na kudhani wapo above the law, serikali isiyo heshimu 'bill of rights' kwa watu wake vitisho kila mara watu wanapotaka kutumia democrasia kudai haki zao. Jamani kuna haja ya mdahalo kuzungumzia mambo complicated wakati basics tuu za democracy ya nchi yeyote hapa kwetu zina kuwa violated day in day out. Si sawa mtoto kuto kwenda shule wala si sawa kuwatishia kifungo sijui bunduki waandamaji au wagoamaji hii tu tosha kusema kwamba CCM ni tambara bovu. Kama hivi ni vitu muhimu katika constitution ya nchi yeyote na vinakuwa avithaminiwi kabisa amna point ya mdahalo its obvious whats wrong.

Kwa mtaji huo kufanya mdahalo au kulilia mdahalo ni kujifanya wajuaji na kupenda kukopi kila kitu from the west when our political affairs are crystal clear. Upinzani uache uvivu nendeni mka kampeni huko watanzania waamke.
 
Kazi kweli kweli, cha zaidi ni pale CCM wanapoona baadhi ya wakongwe kama Shibuda kutishia kuhamia upinzani na jana wanachama kama 70 wamerudisha kadi za CCM na kujiunga na upinzani, kingine ni pale TUCTA walipokaa na kusema watatoa tamko kuwa ni rais gani wamchague mwaka huu, "POOR CCM NA SHAME ON YOU" Wametunyanyasa, wemetutesa na kutudhalililisha vya kutosha na sasa saa ya ukombozi imefika na na CHADEMA ndio mkombozi wetu, kilikuwepo KANU je mbona kiling'oka? na hao tume ya uchaguzi wakiwasikiliza CCM na kumzuia Slaa kugombea uraisi tutaanzisha maandamano ya amani kuhamasisha wananchi kugoma kupiga kura hapo Oktoba. CCM ACHENI UOGA. "PIGANENI KWA SERA SIO KWA SARE"

DITTO well said
 
Back
Top Bottom