CC ya CCM haikuwa na jipya

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Nilipowasili tu jana usiku kutoka Arusha-kwa-Lema nikatamani kujua yaliyoendelea Kisiwandui, Zanzibar. Huko kulifanyika kikao cha Kamati Kuu ya CCM kilichofanya tathmini ya mambo kadha wa kadha yahusuyo chama.

Iliripotiwa kuwa ajenda ya wagombea urais ilikuwa moto na kumeafikiwa mambo magumu na mazito juu ya baadhi yao au wote. Nikataka kujua ukweli. Nikawasiliana na Mjumbe mmoja wa CC aliyekuwepo Kisiwandui.

Alichosema ni kuwa hakukuwa na jipya. Yamejadiliwa mambo ya kawaida sana ya kichama. Hata Ripoti ya Kamati ya Komredi Mangula iliwafagilia wagombea watarajiwa kwa kusema wamerekebishika na sasa wako safi.

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na maandalizi ya uchaguzi ujao yaliteka sana kikao husika. Wakati wa kuwajadili wagombea mbalimbali chamani,wajumbe waligawanyika na kila mchangiaji alimfagilia wa kwake.

"Hakukuwa na jipya ndugu yangu. Nikirudi tutaongea vizuri"nikaambiwa na kuahidiwa na mjumbe huyo wa CC.

Mambo yanakaribia patamu!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 

Huwa ninaamin taarifa yako cku zote asante
 
Kwani kulitegemewa nini dakika ya 88. . . . . . .
 
Daima CCM hawana jipya! Ulitegemea waongelee issue ya ESCROW wakati wote ni wezi? Walikutana kupongezana tu na kulipana mamilioni ya pesa za walipa kodi na kuondoka!
 

Jipya utalipata mwezi wa tano.
 
Kijana,hujui ninayoyajua.Unayajua ninayoyajua. Tusubiri tuone

Mzee Tupatupa

Najua usiyoyajua, sitaki kujua unayoyajua, yananitosha ninayoyajua, sitaki kujua kupitia unayoyajua, jua ya ufipa ya lumumba yatakufanya utoke jasho kwenye jua.
 

Unachanganya watu maana taarifa kwa mujibu wa Kubenea humu humu JF kikao ni leo 13/01/2015 hicho cha jana ni kipi wakati viongozi walikuwa kwenye sikukuu za Mapinduzi?
 
Sasa mlitaka lipi litokee, Yale maneno yenye eti lowasa atafukuzwa, nk , yameishia wapi. Waongo na wanafiki
 
Unachanganya watu maana taarifa kwa mujibu wa Kubenea humu humu JF kikao ni leo 13/01/2015 hicho cha jana ni kipi wakati viongozi walikuwa kwenye sikukuu za Mapinduzi?
Huyu jamaa mpuuzi na muongo wa kutupwa kazi yake kutunga uongo tu cc wanakaa leo hicho anachosema kimekaa jana labda aliitisha petro mselewa ila siyo jk
 
Unachanganya watu maana taarifa kwa mujibu wa Kubenea humu humu JF kikao ni leo 13/01/2015 hicho cha jana ni kipi wakati viongozi walikuwa kwenye sikukuu za Mapinduzi?

Jana kulikuwa na kikao Kisiwandui Zanzibar

Mzee Tupatupa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…