CBS yamlipa Oprah Winfrey $8M kwa kuwahoji Harry na Meghan

Ikaria

Member
Jul 17, 2019
74
205
Kituo cha habari CBS kilimlipa Oprah Winfrey takriban dola za Marekani Milioni 8 ili kupewa leseni ya mahojiano yake na mtoto wa Mfalme Harry na mkewe Meghan.

Mahojiano hayo yalifanikishwa na kampuni ya Harpo Production inayomilikiwa na Oprah
Mahojiano hayo ya takriban masaa mawili yalipeperushwa Marekani usiku wa jana na kuoneshwa kwenye vyombo vya habari vya Uingereza Jumatatu ya tarehe 8 usiku kwa ushirikiano na CBS.

Ni mahojiano yaliyovutia hisia mseto kote ulimwenguni baada ya Meghan kufichua uchungu aliopitia ndani ya kasri ya kifalme Uingereza kutokana na kuwa yeye ni mwanamke Mwafrika.

Meghan anasema hata kabla ya kumzaa mtoto wake Archie, tayari alikuwa ameambiwa kwamba itifaki (protocol) hazingeruhusu Archie kupewa hadhi ya Mwanamfalme kwa sababu sio mzungu kamili.

Aliendelea kusema alitamani hata kujitoa uhai kwani alikuwa ameanza kujiona hafai kabisa.

“Kuna muda niliwaza hata ni bora nife kutokana na jinsi walivyokuwa wakinibagua” alisema Meghan huku machozi yakimtoka.

Kwa upande wake Harry pia alisema alikuwa akipata maswali mengi ya kibaguzi kutoka kwa familia yake jambo ambalo lilimshtua sana.

“Niliulizwa natarajia mwanangu atakuwa mweusi kiasi gani” amesema Harry.

Ni baada ya kushindwa kuvumilia masaibu haya ambapo sasa waliamua kuondoka kwenye Kasri Uingereza kwenda kuishi Marekani maisha ya kawaida.

Aidha pia Harry amesema familia yake iliacha kumsaidia kifedha na kwamba hata baba yake aligoma kupokea simu zake.

images (1).jpeg
 
Halafu eti wanatupenda saaana!!!

Huyo kaolewa na mtoto wao ninyi je ambao hamna hata uhusiano wowote!? Na hii inafanyika kwenye kasri la Malkia, familia inayosemwa imestaarabika kiasi cha kupewa heshima ya kuwa 'nuru' ya Uingereza;Je. Huko mitaani ambapo raia hawajastaarabika hali ikoje?
 
Ingawa ubaguzi upo sana Ulaya lakini haina ubishi kada za sayansi zimeshikiliwa na ethnic minorities. Inatia raha sana unafiki hospitali daktari bingwa wa kitengo ni Mghana, Mhindi au Mwarabu. Hata kama wafagiaji hawampendi kwa rangi au dini yake lakini inabidi wampe heshima.
 
Halafu eti wanatupenda saaana!!!

Huyo kaolewa na mtoto wao ninyi je ambao hamna hata uhusiano wowote!? Na hii inafanyika kwenye kasri la Malkia, familia inayosemwa imestaarabika kiasi cha kupewa heshima ya kuwa 'nuru' ya Uingereza;Je. Huko mitaani ambapo raia hawajastaarabika hali ikoje?
Nyie mtakubali kuwa na rais mzungu hapa Tanzania?

Waafrica ni wabaguzi kuliko wanadamu wote wa aina nyingine.

CCM kila siku inahubiri ubaguzi kwa wapinzani sembuse wazungu?
 
Daah inafikirisha sana, wazungu hawatupendi
Kuna nyakati tunawalaumu bure wazungu, hii kitu ipo popote dunuani. Ni ndoa ngapi hapa tanzania hazijafungwa kisa wazazi hawataki mtoto wao aoe au aolewe na mtu wa kabila au dini tofauti?
Hivi tuchukue picha kuwa wewe ni mfalme, je ungeweza kuruhusu ufalme wako awepo mtoto wa kizungu?
 
Halafu eti wanatupenda saaana!!!
===
Huyo kaolewa na mtoto wao ninyi je ambao hamna hata uhusiano wowote!? Na hii inafanyika kwenye kasri la Malkia, familia inayosemwa imestaarabika kiasi cha kupewa heshima ya kuwa 'nuru' ya Uingereza;Je. Huko mitaani ambapo raia hawajastaarabika hali ikoje?
Tundu lisu
 
Kuna nyakati tunawalaumu bure wazungu, hii kitu ipo popote dunuani. Ni ndoa ngapi hapa tanzania hazijafungwa kisa wazazi hawataki mtoto wao aoe au aolewe na mtu wa kabila au dini tofauti?
Hivi tuchukue picha kuwa wewe ni mfalme, je ungeweza kuruhusu ufalme wako awepo mtoto wa kizungu?

Waafrika especially watanzania ndio wabaguzi numero uno. Kutwa kucha kuwakataza watoto wao wasioe wachaga mara wasioe wanyakyusa au wahaya . Kuna nyuzi kibao humu ndani za watanzania kuwakataza watoto wao wasioe au kuolewa na baadhi ya makabila, je huo sio ubaguzi? Kama tunaweza kubaguana wenyewe kwa wenyewe kwa nini tuwashangae Buckingham palace wanapombagua mtu mweusi? Tusiwe wanafiki, tutoe kwanza boriti kwenye macho yetu, ndipo tutaona vibanzi kwenye macho ya wenzetu. Fix your own issues first before you consider fixing another person’s issues
 
Weusi wanapiga kitabu cha kufa mtu. Marekani sasa hivi kundi linaloongoza kupiga kitabu ni wanawake weusi wanakipiga hasa na wengi hawa wanafikiria kujiajiri. Wanaume nao wanajitahidi ingawaje bado wanasua sua. Waafrika Trump alipiga marufuku kusoma zaidi ya miaka miwili maana yake kwa Waafrika ilikuwa ni kusoma diploma tu lakini Biden kafuta huo upuuzi.
Ingawa ubaguzi upo sana Ulaya lakini haina ubishi kada za sayansi zimeshikiliwa na ethnic minorities. Inatia raha sana unafiki hospitali daktari bingwa wa kitengo ni Mghana, Mhindi au Mwarabu. Hata kama wafagiaji hawampendi kwa rangi au dini yake lakini inabidi wampe heshima.
 
Maisha hayaa.yaani interview tu.mama kalipwa dola million 8.
haikuwa rahisi kuwa convince Harry na Meghan kutoa ukweli wote ,kumbuka hii ni kashfa nzito Sana kwa utawala wa malkia.impact ya kutoa ukweli wa Mambo wa jumba la kifalme hasa huu wa ubaguz wa rangi ni kwamba utachochea mijadara kwa waingereza kuanza kulipinga na kulitupia kisogo jumba Hilo,na hii itachochea hisia za waingereza kuanza kufikilia/kutaka ukomo wa mfumo wa uwepo wa ufalme ndani ya UK.kumbuka waingereza walishaanza kitambo kuhoji nn umuhimu wa ufalme ndani ya Uk,sema walikuwa wanakosa hoja yenye mashiko kuung'oa utawala wa ufalme nchini UK.Hivyo mahojiano haya yamekuwa ni pigo kubwa Sana kwa malkia pengine yaka tabiri mwisho wa ufalme Uk.
 
Back
Top Bottom