Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,925
- 30,273
CASSIUS CLAY 1964
Hii picha ilikuwa maarufu sana miaka ya 1960. Ilipigwa siku Cassius Clay alipomshinda Sony Liston na kuchukua mkanda wa uzito wa juu wa masumbwi.
Kwangu mimi picha hii inaniletea kumbukumbu nyingi za miaka hiyo. Kwanza nakumbuka kupokea simu kanipigia baba yangu niko nyumbani ananifahamisha kuwa Cassius Clay amempiga Sony Liston.
Kwa nini baba anipigie simu kunipa taarifa hizi? Alikuwa anajua ni kwa kiasi gani nikimpenda Cassius Clay. Wakati huo bado hajawa Muhammad Ali. Nyakati hizi zilikuwa za kipekee sana kwangu na kwa hakika watoto wengi wa umri wangu.
Hizi zilikuwa nyakati za The Beatles, Elvis Presley, Cliff Richard, Helen Shapiro, Ray Charles, Sam Cooke na wengineo. Nyimbo za hawa wanamuziki zilituchukua sana. Lakini kadri umri ulivyozidi kusogea na fikra zangu za utoto zikawa naziacha nyuma pamoja na hawa watu maarufu.
Lakini mara moja moja ninaposikia miziki yao wa nyakati zao narejea udogoni inakuwa kama jana. Nakumbuka siku nilipoiona senema ya Elvis Presley, "Blue Hawaii," Empire Cinema. Ilikuwa siku ya Eid Fitr. Nyimbo zake hadi leo zinajaza moyo wangu kumbukumbu nyingi.
Nimemuona Helen Shapiro katika "Play it Cool," anaimba "I don't Care."
Katika senema hii alikuwapo Billy Fury. Kijana wa Kiingereza akipiga mitindo ya Rock and Roll.
Siku moja niko Liverpool Coach Station, London stesheni ya mabasi kwenda "bara" ya Uingereza ukipenda.
Natoka Cardiff nakwenda Glasgow. Cardiff ukifananisha na London ni shamba mfano unatoka Kilwa unakuja Dar-es-Salaam upande basi kwenda labda Arusha.
Ukifika Dar es Salaam kituo cha mabasi Mnazi Mmoja na wewe huijui Dar-es-Salaam bila shaka utanyoosha miguu kuangalia mji kabla ya kwenda Arusha angalau upate cha kuhadithia ukirejea Kilwa.
Basi nanyoosha miguu kuangalia mitaa jirani na hapo Liverpool Coach Station. Nikakuta tangazo limebandikwa nje kwenye kioo cha mgawa mmoja mdogo mfano wa AK Tea Room.
Tangazo lile linamtangaza Helen Shapiro kama Born Again Christian na kueleza wapi atahubiri Injili. Zaidi ya miaka 30 sasa imepita. Nilipangiwa kusomesha darasa moja la undergraduates University of Iowa.
Wamarekani wana utamaduni na mila za kipekee sana. Wanafunzi wamekaa darasani utadhani wako kijiweni wana barizi. Wenyeji wameniekeza kabla vipi naweza ku-connect na darasa langu siku ya kwanza wakanielewa. Nikaweka kwenye projector poster ya Blue Hawaii nikawauliza kama wanamjua huyo kwenye poster.
"That's Elvis..."
Nikawaeleza kwa kifupi historia yangu na Elvis Presley nikiwa na miaka 12. Nikaweka picha yangu nyuma yangu wanesimama vijana wa umri wangu. Hii iliwamaliza kabisa. Darasa lilichangamka na lecture ilimalizika vyema kabisa. Wamarekani wanaamini dunia yote iko kwao kwengine Afrika ni mwitu.
Muhammad Ali hakupata kuwa mbali na mimi hadi kifo chake.
Kitabu chake, "Muhammad Ali My Own Story," ni katika vitabu ninavyovipenda sana. Nilipofika New York nilifika Guy Madison Garden ambako Muhammad Ali alipigana na Joe Frazier 1971 katika pambano lililoitwa, "Fight of the Century." Nilifika pia Central Park kuangalia John Lennon Memorial. Lennon alikuwa mmoja wa The Beatles.
Katika wenyeji wangu New York alikuwa Spiegel ambaye alikuwa rafiki wa karibu sana wa John Lennon. Jana yake alikuwa nyumbani kwa Lennon jirani sana na Central Park na siku ya pili ndiyo Lennon akauliwa kwa kupigwa risasi nje ya nyumbani kwake.
Mimi nilishangaa aliponieleza hili na yeye alishangaa nilipomwimbia nyimbo ya The Beatles, "Things We Said Today," na nikamwambia nikiipiga nyimbo hii kwenye guitar langu Hoffner.
Wakati huo nilikuwa na miaka 16.
Cassius Clay v Sonny Liston, MIami Beach 1964
Muhammad Ali v Joe Frazier, Guy Madison Garden New York 1971
John Lennon Memorial, Central Park New York
Hii picha ilikuwa maarufu sana miaka ya 1960. Ilipigwa siku Cassius Clay alipomshinda Sony Liston na kuchukua mkanda wa uzito wa juu wa masumbwi.
Kwangu mimi picha hii inaniletea kumbukumbu nyingi za miaka hiyo. Kwanza nakumbuka kupokea simu kanipigia baba yangu niko nyumbani ananifahamisha kuwa Cassius Clay amempiga Sony Liston.
Kwa nini baba anipigie simu kunipa taarifa hizi? Alikuwa anajua ni kwa kiasi gani nikimpenda Cassius Clay. Wakati huo bado hajawa Muhammad Ali. Nyakati hizi zilikuwa za kipekee sana kwangu na kwa hakika watoto wengi wa umri wangu.
Hizi zilikuwa nyakati za The Beatles, Elvis Presley, Cliff Richard, Helen Shapiro, Ray Charles, Sam Cooke na wengineo. Nyimbo za hawa wanamuziki zilituchukua sana. Lakini kadri umri ulivyozidi kusogea na fikra zangu za utoto zikawa naziacha nyuma pamoja na hawa watu maarufu.
Lakini mara moja moja ninaposikia miziki yao wa nyakati zao narejea udogoni inakuwa kama jana. Nakumbuka siku nilipoiona senema ya Elvis Presley, "Blue Hawaii," Empire Cinema. Ilikuwa siku ya Eid Fitr. Nyimbo zake hadi leo zinajaza moyo wangu kumbukumbu nyingi.
Nimemuona Helen Shapiro katika "Play it Cool," anaimba "I don't Care."
Katika senema hii alikuwapo Billy Fury. Kijana wa Kiingereza akipiga mitindo ya Rock and Roll.
Siku moja niko Liverpool Coach Station, London stesheni ya mabasi kwenda "bara" ya Uingereza ukipenda.
Natoka Cardiff nakwenda Glasgow. Cardiff ukifananisha na London ni shamba mfano unatoka Kilwa unakuja Dar-es-Salaam upande basi kwenda labda Arusha.
Ukifika Dar es Salaam kituo cha mabasi Mnazi Mmoja na wewe huijui Dar-es-Salaam bila shaka utanyoosha miguu kuangalia mji kabla ya kwenda Arusha angalau upate cha kuhadithia ukirejea Kilwa.
Basi nanyoosha miguu kuangalia mitaa jirani na hapo Liverpool Coach Station. Nikakuta tangazo limebandikwa nje kwenye kioo cha mgawa mmoja mdogo mfano wa AK Tea Room.
Tangazo lile linamtangaza Helen Shapiro kama Born Again Christian na kueleza wapi atahubiri Injili. Zaidi ya miaka 30 sasa imepita. Nilipangiwa kusomesha darasa moja la undergraduates University of Iowa.
Wamarekani wana utamaduni na mila za kipekee sana. Wanafunzi wamekaa darasani utadhani wako kijiweni wana barizi. Wenyeji wameniekeza kabla vipi naweza ku-connect na darasa langu siku ya kwanza wakanielewa. Nikaweka kwenye projector poster ya Blue Hawaii nikawauliza kama wanamjua huyo kwenye poster.
"That's Elvis..."
Nikawaeleza kwa kifupi historia yangu na Elvis Presley nikiwa na miaka 12. Nikaweka picha yangu nyuma yangu wanesimama vijana wa umri wangu. Hii iliwamaliza kabisa. Darasa lilichangamka na lecture ilimalizika vyema kabisa. Wamarekani wanaamini dunia yote iko kwao kwengine Afrika ni mwitu.
Muhammad Ali hakupata kuwa mbali na mimi hadi kifo chake.
Kitabu chake, "Muhammad Ali My Own Story," ni katika vitabu ninavyovipenda sana. Nilipofika New York nilifika Guy Madison Garden ambako Muhammad Ali alipigana na Joe Frazier 1971 katika pambano lililoitwa, "Fight of the Century." Nilifika pia Central Park kuangalia John Lennon Memorial. Lennon alikuwa mmoja wa The Beatles.
Katika wenyeji wangu New York alikuwa Spiegel ambaye alikuwa rafiki wa karibu sana wa John Lennon. Jana yake alikuwa nyumbani kwa Lennon jirani sana na Central Park na siku ya pili ndiyo Lennon akauliwa kwa kupigwa risasi nje ya nyumbani kwake.
Mimi nilishangaa aliponieleza hili na yeye alishangaa nilipomwimbia nyimbo ya The Beatles, "Things We Said Today," na nikamwambia nikiipiga nyimbo hii kwenye guitar langu Hoffner.
Wakati huo nilikuwa na miaka 16.
Cassius Clay v Sonny Liston, MIami Beach 1964
Muhammad Ali v Joe Frazier, Guy Madison Garden New York 1971
John Lennon Memorial, Central Park New York