Jamani wadau nisaidieni, nahitaji car security system zile ambazo kuna hidden switch kama mtu hajui ilipo hawezi kuwasha gari pamoja na alarm yake, zinapatikana wapi hapa Dar na kwa sh ngapi roughly? aina gani za alarm ndio nzuri zaidi? ahsanteni!
sasa kuna vifaa unaweza kuweka simcard ndani na badala ya kutoa alarm unapata msg au unaweza kutuma command kupitia cm yako kuzima gari ikiwa unahisi limeibiwa, n.k
nadhani auto watch ni nzuri, bei max ni 180000 (pamoja na kufunga). Kariakoo ule mtaa wanapouza speaker na radio za magari (mtaa unaoenda kukutana straight na barabara ya umoja wa mataifa) kuna maustaadh fulani hufunga. Pata fundi mzuri unapoweka alarm, maana ukimpata kilaza anaweza kukuunguzia gari, hasa umeme wa gari ukiwa coplicated.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.