Canal mstaafu Fabiani Massawe

Canal mstaafu Fabiani Massawe

mtu kakosea maelezo mnamuambia alafu mnamjibu swali lake sio kila mtu anaponda tu. Yani kila mtu anajiona anajua sana m nadhani mtu wa kwanza ku comment kamuambia kakosea nyie wengine kama mnajua mnajibu swali sio tena kurudia yaleyale.
 
ni mtoto wa kwanza wa mzee Ignas au Inyasi Mark Massawe na alizaliwa kijiji cha Kifuni kata ya Kibosho magharibi. Elimu ya msingi alisoma Umbwe na sekondar alisoma Umbwe sec. Zidi ya hapo tulipoteana na kuja kukutana Dar akiwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni. Kwetu alikuwa role modal kwani alitutia moyo wa kupenda kusoma hasa wakati tulipokuwa tunamtembelea pale Umbwe sec. Alitugawia karanga na ugali wa shule. Ni mmoja wa viongozi waliolelewa katika maadili yaliyotukuka na uchapaji kazi wake upo kwenye damu kwani familia atokayo ni ya wale hardworkers na wenye hofu na mungu. Anao nduguze aliowahamasisha sana kusoma na alijitahidi kuijenga familia ya kisomi. Hata wazee wetu waliiga kutusomesha kupitia familia yao. Mungu ampe maisha marefu aweze kutuongoza katika maendeleo kwani ni kati ya viongozi wachache wabunifu. Mfano jitegemee sec na mgulani ni moja ya ubunifu wake.

amen mkuu Mnasihi hata mimi natokea kule kijiji cha manushi sinde
 
Last edited by a moderator:
mtu kakosea maelezo mnamuambia alafu mnamjibu swali lake sio kila mtu anaponda tu. Yani kila mtu anajiona anajua sana m nadhani mtu wa kwanza ku comment kamuambia kakosea nyie wengine kama mnajua mnajibu swali sio tena kurudia yaleyale.

mkuu Kivule ndivyo watanzania wengi walivyo kufuata MKUMBO ndio hawa wamefikisha taifa hili hapa lilipo na wala si wanasiasa.
 
Last edited by a moderator:
A

alafu we Pdidy, acha viroba mkuu, kwanza umejua kuandika? Mbona siku hizi hutupi tena habari za airport JNA?


Niko hapa jf toka 2007 nikitumia Id tofauti.

Acha ujinga.

analamba viroba nani mpwa hapo

aisee nipo naona mizigo umenza peleka via.cargo

vijana wa mwakyembe wanabaki kukenua tuuu unatisha uppo
 
Last edited by a moderator:
Kila mtu ana habari zake za ajabu ambazo watu wakizisikia kila wamwonapo usoni,hupatwa na mitazamo fulani kumhusu mtu huyo.Binafsi kila nimwonapo mtu huyu nacheka sana na kusema hao walio chini yake huko aliko "kazi wanayo".

Bila shaka wale wakimbizi wa Kagera wanayo ya kusimulia kuhusu huyu bwana.

Sitasahau siku alipomfuata headmaster wa Azania na kumlalamikia kuwa wanafunzi wa Azania wakiwa vituo vya mabasi na barabarani,wanawapiga sana wanafunzi wa kike wa Jitegemee baada ya kutokea ugomvi baina ya wanafunzi wa shule hizo mbili,ugomvi uliodumu takriban wiki nzima hadi serikali ilipoingilia kati.

Mnaamka asubuhi vituo vya Posta,kkoo na fire vimerembwa kwa chupi,madaftari,mabegi,sidiria za wadada wa Jitegemee waliokuwa wakienda shule asubuhi.Azania walikuwa na fujo sana kwa kweli!

Headmaster wa Azania akamjibu kuwa hawezi kufanya lolote kwa kuwa mambo hayo yanatokea nje ya shule,yeye hana uwezo nayo.

Massawe akamjibu "nashukuru bwana".

Akaitisha assemble ya wanafunzi wote wa Jite(walikuwa wengi sana),wote wakaondoka shift moja ya jioni.Jana yake aliwaambia waende shule wamejizatiti kivita,akawaamuru wabebe kila wanachoweza kubeba,panga,rungu,sime,nondo n.k
Kabla wanafunzi hawajatoka jioni,alituma kundi la askari waliovaa kiraia,wakaenda kukaa vituo vyote ambavyo wanafunzi wa Azania walipenda kukaa na kuvizia wadada wa Jitegemee na kuwapiga,kuwanyanyasa .
Ilikuwa rahisi kwa Azania kufanya hujuma maana walikuwa wakitoka mapema zaidi ya Jite na hivyo kujiandaa na kuweka mitego vituoni,wengine wakiwa wamevua uniform.

Halafu akawavisha askari wengine wa kike Jkt uniform za A level,wakatoka mapema na kufika vituo vya mjini wakionekana ni wanafunzi,Azania si wakaanzisha mambo yao,wasijue vituo vimejaa wajeda na sio abiria au wanafunzi pekee,mtitu ukalipuka,wakati ukiendelea madenti woote wa Jite wakaondoka kwa pamoja,wa kiume na kike wakitembea pamoja kuelekea destination zilizopangwa kiusalama kulingana na eneo mwanafunzi analokwenda,ambapo wengi walikuwa wakipita kkoo na posta,kama walivyoamrishwa na baba yao Massawe(huyu mtu alikuwa akisema neno tu,wanafunzi,walimu,askari wote wanalibeba zima zima,alikuwa kama mungu mtu pale Mgulani),wakazisimamisha daladala zinazopita nje ya shule yao,na kushusha abiria wote kwa nguvu,wakapanda na kuwapa makonda hela nyingi za nauli ya mtu mzima na zaidi,daladala kustukia mchongo zikawa zinaenda tupu hadi Jitegemee na kubeba wanafunzi,wakapelekwa mjini kwa makundi,wakakuta wajeda tayari wamemaliza kazi,wakakosa cha kufanya na kuanza kufanya fujo mjini,balaa likawa zito hadi shule zikafungiwa na wizara kwa muda.
Headmasters wote wakaitwa kujieleza,ndipo Massawe akatoa ya moyoni.

Tangu wakati huo sijasikia tena ugomvi mkubwa wa wanafunzi Dar kama enzi zile.

Serikali ikapata somo,nadhani na UMISETA ikapigwa stop manake inasemekana ugomvi ulianzia huko.

Ni mtu ambae ukimkabidhi kazi hakubali kushindwa,atatafuta namna ya kupata matokeo chanya kwa namna yoyote ile,jambo linalomfanya wengine wamuone jembe,wengine wamuone mjanja mjanja kupitiliza,wengine wamuone mpenda sifa,wengine wamuone opportunist,haijalishi unamwonaje,wewe jua tu kazi itafanyika kwa namna yoyote.

Pale Jitegemee alibuni miradi na kuwalipa walimu vizuri tu,hata wakati mwingine watu walijiuliza sana anatoa wapi uwezo wa kulipa walimu vizuri vile,wakawa suspicious nae ila angle moja tu aliwashinda mahasimu wake,kazi zilifanyika kwa mafanikio,aliendesha shule kwa mafanikio,na kila aliyekuwa chini yake alimfurahia na kumheshimu sana na kufanya kazi kwa bidii,hata wanafunzi na wajeda waliowahi kupishana nae na kukiona cha moto,leo ukiwauliza,watakwambia wanamheshimu na kumkumbuka sana.

Baadae alipandishwa cheo na kupelekwa makao makuu,huko nako akafanya vema tu,na kuanza safari ya kikazi iliyomfikisha hapa alipo.

Binafsi nilimjua zaidi akiwa Jitegemee na makao makuu kidogo.Sifahamu profile yake maeneo mengine nje ya hapo.

Tuliomjua huyu mtu,tulihisi mapema tu kuwa atafika mbali kikazi na kimaisha.

Ni mtoto wa mjini kweli,kamanda haswa,labda abadilike sasa,manake siasa hizi ngumu kweli.
 
kanali mstaafu fabian massawe amezaliwa mkoni kilimanjaro, kijiji cha mkomongo, kibosho. Ametuikia jeshi la wananchi tangu miaka ya 1970 katika nafasi mbalimbali ikiwa ni pamoja na mkuu kituo cha elimu ya sekondari ya jioni mgulani dar es salaam (sasa jitegemee sec). Baadae alikuwa mkuu wa kwanza wa shule ya jitegemee kwa miaka zaidi ya 15 kabla ya kuteuliwa mkuu wa wilaya ya kinondoni, baadae muleba na karagwe. Kwa sasa kanali massawe ni mkuu wa mkoa wa kagera.

bosco kama unaijua unakuja na jina.la esam
 
Kuhusu kazi wako waliosema hapo juu. Kweli ni mchapakazi sana. Ndio watu wanaohitajika nchi hii. Sio watu wa kuonaona huruma zisizo na msingi...

Btw.... ana mabinti warembo sana kwa kweli. Natumaini na hii ni sehemu ya wasifu.
 
Kila mtu ana habari zake za ajabu ambazo watu wakizisikia kila wamwonapo usoni,hupatwa na mitazamo fulani kumhusu mtu huyo.Binafsi kila nimwonapo mtu huyu nacheka sana na kusema hao walio chini yake huko aliko "kazi wanayo".

Bila shaka wale wakimbizi wa Kagera wanayo ya kusimulia kuhusu huyu bwana.

Sitasahau siku alipomfuata headmaster wa Azania na kumlalamikia kuwa wanafunzi wa Azania wakiwa vituo vya mabasi na barabarani,wanawapiga sana wanafunzi wa kike wa Jitegemee baada ya kutokea ugomvi baina ya wanafunzi wa shule hizo mbili,ugomvi uliodumu takriban wiki nzima hadi serikali ilipoingilia kati.

Mnaamka asubuhi vituo vya Posta,kkoo na fire vimerembwa kwa chupi,madaftari,mabegi,sidiria za wadada wa Jitegemee waliokuwa wakienda shule asubuhi.Azania walikuwa na fujo sana kwa kweli!

Headmaster wa Azania akamjibu kuwa hawezi kufanya lolote kwa kuwa mambo hayo yanatokea nje ya shule,yeye hana uwezo nayo.

Massawe akamjibu "nashukuru bwana".

Akaitisha assemble ya wanafunzi wote wa Jite(walikuwa wengi sana),wote wakaondoka shift moja ya jioni.Jana yake aliwaambia waende shule wamejizatiti kivita,akawaamuru wabebe kila wanachoweza kubeba,panga,rungu,sime,nondo n.k
Kabla wanafunzi hawajatoka jioni,alituma kundi la askari waliovaa kiraia,wakaenda kukaa vituo vyote ambavyo wanafunzi wa Azania walipenda kukaa na kuvizia wadada wa Jitegemee na kuwapiga,kuwanyanyasa .
Ilikuwa rahisi kwa Azania kufanya hujuma maana walikuwa wakitoka mapema zaidi ya Jite na hivyo kujiandaa na kuweka mitego vituoni,wengine wakiwa wamevua uniform.

Halafu akawavisha askari wengine wa kike Jkt uniform za A level,wakatoka mapema na kufika vituo vya mjini wakionekana ni wanafunzi,Azania si wakaanzisha mambo yao,wasijue vituo vimejaa wajeda na sio abiria au wanafunzi pekee,mtitu ukalipuka,wakati ukiendelea madenti woote wa Jite wakaondoka kwa pamoja,wa kiume na kike wakitembea pamoja kuelekea destination zilizopangwa kiusalama kulingana na eneo mwanafunzi analokwenda,ambapo wengi walikuwa wakipita kkoo na posta,kama walivyoamrishwa na baba yao Massawe(huyu mtu alikuwa akisema neno tu,wanafunzi,walimu,askari wote wanalibeba zima zima,alikuwa kama mungu mtu pale Mgulani),wakazisimamisha daladala zinazopita nje ya shule yao,na kushusha abiria wote kwa nguvu,wakapanda na kuwapa makonda hela nyingi za nauli ya mtu mzima na zaidi,daladala kustukia mchongo zikawa zinaenda tupu hadi Jitegemee na kubeba wanafunzi,wakapelekwa mjini kwa makundi,wakakuta wajeda tayari wamemaliza kazi,wakakosa cha kufanya na kuanza kufanya fujo mjini,balaa likawa zito hadi shule zikafungiwa na wizara kwa muda.
Headmasters wote wakaitwa kujieleza,ndipo Massawe akatoa ya moyoni.

Tangu wakati huo sijasikia tena ugomvi mkubwa wa wanafunzi Dar kama enzi zile.

Serikali ikapata somo,nadhani na UMISETA ikapigwa stop manake inasemekana ugomvi ulianzia huko.

Ni mtu ambae ukimkabidhi kazi hakubali kushindwa,atatafuta namna ya kupata matokeo chanya kwa namna yoyote ile,jambo linalomfanya wengine wamuone jembe,wengine wamuone mjanja mjanja kupitiliza,wengine wamuone mpenda sifa,wengine wamuone opportunist,haijalishi unamwonaje,wewe jua tu kazi itafanyika kwa namna yoyote.

Pale Jitegemee alibuni miradi na kuwalipa walimu vizuri tu,hata wakati mwingine watu walijiuliza sana anatoa wapi uwezo wa kulipa walimu vizuri vile,wakawa suspicious nae ila angle moja tu aliwashinda mahasimu wake,kazi zilifanyika kwa mafanikio,aliendesha shule kwa mafanikio,na kila aliyekuwa chini yake alimfurahia na kumheshimu sana na kufanya kazi kwa bidii,hata wanafunzi na wajeda waliowahi kupishana nae na kukiona cha moto,leo ukiwauliza,watakwambia wanamheshimu na kumkumbuka sana.

Baadae alipandishwa cheo na kupelekwa makao makuu,huko nako akafanya vema tu,na kuanza safari ya kikazi iliyomfikisha hapa alipo.

Binafsi nilimjua zaidi akiwa Jitegemee na makao makuu kidogo.Sifahamu profile yake maeneo mengine nje ya hapo.

Tuliomjua huyu mtu,tulihisi mapema tu kuwa atafika mbali kikazi na kimaisha.

Ni mtoto wa mjini kweli,kamanda haswa,labda abadilike sasa,manake siasa hizi ngumu kweli.

Daaaaah hii issue ya azania na jiteute, umenikumbusha mbali sana, maana nilikuwa mhanga wa mafujo hayo.
 
Jamani naomba kumjua huyu canal

historia yake amezaliwa wapi ametumikia taifa muda gani. ni makini sana huyu jamaa kama sikosei ni mkuu wa mkoa wa kagera.
Karibuni wakuu tumjue.

Hiyo Canal unamaanisha nini?
 
Mh Jf raha...Jitegemee Sec na Jkt Mgulani kwa vipindi tofauti...shule mbili hizooo enheee...stress free ndani ya JF...
 
Wanajf kuna masahihisho kidogo kwa wasifu wa huyu rt canal Fanian.Yeye ni uzao wa pili ktk familia ya Ignace na ni kijiji cha KIFUNI.Kweli yule ni jembe,baba yetu mdogo!
 
nimejichanganya wapi?

Mungu wangu!! hata huoni ulipojichanganya? hii mpya! ntakusaidia, 1. huwezi kumfagilia mtu halafu hujui sawasawa ni nani, yuko wapi na anafanya nini, mara unadhani yuko Kagera, mara polisi Tabora 2. Umeandika Canal si ungesema tu Kanali? Canal ni mrefreji, na katika lugha zetu zile za faragha ni tusi kubwa. Kama ulitaka kuandika in english ungesema Colonel 3. Post yako imekaa kama vile unatuuliza tukuambie wewe ni nani.
 
Mungu wangu!! hata huoni ulipojichanganya? hii mpya! ntakusaidia, 1. huwezi kumfagilia mtu halafu hujui sawasawa ni nani, yuko wapi na anafanya nini, mara unadhani yuko Kagera, mara polisi Tabora 2. Umeandika Canal si ungesema tu Kanali? Canal ni mrefreji, na katika lugha zetu zile za faragha ni tusi kubwa. Kama ulitaka kuandika in english ungesema Colonel 3. Post yako imekaa kama vile unatuuliza tukuambie wewe ni nani.

Ni usalama wa taifa.
 
Huyu mheshimiwa ni mpambanji mzuri sana ila alijitia doa tu pale alipochakachua matokea ya mbunge jimbo la Karagwe wakati huo akiwa Mkuu wa Wilaya. Na kwa dhambi hiyo akateuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa.
 
Kuhusu kazi wako waliosema hapo juu. Kweli ni mchapakazi sana. Ndio watu wanaohitajika nchi hii. Sio watu wa kuonaona huruma zisizo na msingi...

Btw.... ana mabinti warembo sana kwa kweli. Natumaini na hii ni sehemu ya wasifu.

imebidi nicheke tu
 
Akiwa MKUU WA wilaya KARAGWE alisimamia suala LA usafi mpaka wrote tukafurahi sana pia mji WA Kayanga ulikuwa no WA mfano kwa wilaya yingine
 
Back
Top Bottom