cameraphone bora zaidi duniani

cameraphone bora zaidi duniani

Chief-Mkwawa

Platinum Member
Joined
May 25, 2011
Posts
32,062
Reaction score
43,480
siku hizi camera za simu ndio kila kitu watu wameacha kununua digital camera za kawaida na watu wanatumia camera za simu kila wakati. ni vigumu kujua uzuri wa camera ya simu hadi upate maelekezo kidogo. hapa nimejaribu kuchambua simu zenye camera bora zaidi duniani na nimezigawanya katika makundi matatu
1. kundi la kwanza- simu zilizotoka muda mrefu
nimezigawanya kama simu zilizotoka muda mrefu sababu simu hizi sasa hv zimeshuka bei, unaweza ukazipata mkononi kwa bei rahisi na zinapatikana maeneo mengi, hapa tunapata cameraphone 2.


NOKIA 808 pureview
nokia 808 ndio simu ya kwanza duniani kuwa na camera yenye lens ya 41 megapixel, hadi leo inaaaminika ndio camera phone bora duniani. simu hii inatumia symbian specification zake sio za kutisha sana na ina processor mbili moja ya simu na nyengine kwa ajili ya camera tu. nokia 808 ina camera yenye akili ambayo unaweza kubadilisha vitu vingi vya profesional photographer kama iso, white balance na vyenginevyo.


silaha kubwa ya hii camera ya simu au unaweza kuita engineering trick inaitwa pixel oversampling. yani hii nokia 808 ina megapixel 41 lakini inatoa picha hadi za megapixel tano, inachofanya inapiga picha nyingi (kama 7) halafu inaunganisha zile picha kwa kushibisha pixel (pixel 7 zinaunganishwa kutoa super pixel yenye quality nzuri) hii inafanya picha za hii simu kuwa zina quality kubwa sana.


watu wanaotakiwa kumiliki simu hii ni wale wanaopenda camera nzuri kwa bei rahisi, wanaopenda symbian, wasiojali kuzoom sana, wanaopenda quality ya picha za kushare kwenye social site kama facebook, instagram. bei yake kwa sasa unaweza pata rahisi hadi 600,000


GALAXY CAMERA
hii ilikua ni karata ya kwanza ya samsung kwenye soko la camera phone. simu hii inatumia android na ina specification kubwa kushinda nokia 808. galaxy camera yenyewe ina lens ya 16 megapixel. simu hii haitoi picha zenye quality kubwa kama 808 na haina akili kama 808 lakini ina silaha yake yakipekee ambayo 808 haifikii nayo ni zoom. ina lens ambayo inazoom kitu kilicho mbali kije karibu

hii simu ni nzuri kwa waandishi wa habari, na watu wanaopenda kupiga picha kutokea mbali bei ni around 800,000 kama unaweza kutoa hela zaidi ya hiyo na umeipenda aina hii ya camera ya simu ni vizuri ukaenda kununua galaxy s4 zoom ambayo ntaielezea hapo chini.


2.kundi la pili simu zilizotoka sasa
hapa sasa hakuna kulia lia bei hizi ni brandnew camera phone ambazo zimetoka siku si nyingi ndio nzuri zaidi kimuonekano na pia zinakuja na latest features za smartphone.


LUMIA 1020
imetoka juzi july 11 mwaka huu ikiwashangaza wengi sana baada ya nokia kuweza kuunganisha technolojia zake mbili za pureview za mwanga mdogo na pixel oversampling ina maana hapa unapata uwezo wa camera ya lumia 920 na nokia 808 pureview kwenye camera moja. ni nyembamba imeekwa kifashion zaidi pengine hii ndo camera ya simu ianyovutia zaidi

masista duu, mabitozi, mnaopenda fb na social network, wandishi wa habari na wapenda camera wooote hiii ndio camera phone bora zaidi kwa sasa. bei ni around 1,300,000. imeanza kuuzwa marekani sasa mwez wa 9 itasambaa duniani.


GALAXY S4 ZOOM
wote tunaijua samsung galaxy s4, flagship ya samsung sasa hii ni version yake ya camera. usitegemee specs za s4 humu hii imepitwa specification na hata galaxy camera lakini ndio latest camera phone ya samsung. kama alivo mdogo wake silaha kubwa ya hii camera ni zooming ikiwa na lens kubwa kabisa


kama hujali specs sana unaweza ku upgrade toka galaxy camera kuja huku maana camera hii ni nzuri zaidi. watu wanaotakiwa kununua ni wale wale kama wa galaxy camera na bei ni around 900,000 au 1m


3. kundi la tatu ni kamera tunayoisubiria
galaxy camera zimeshindwa kuonesha ubavu kwa nokia lakini yupo ambaye watu wanamsubiria kuja kumpa upinzani nokia ambaye si mwengine bali ni sony honami. hii simu itatoka muda si mrefu na itakua na megapixel 20.

kama kuna camera ya simu unataka kuielewa zaidi inavyofanya kazi usisite kuuliza hapo chini
 
hakuna chakuongeza hapo , umemaliza kila kitu CHIF-mkwawa
 
Last edited by a moderator:
tusubiri hiyo honami nadhani itakuwa ya cc wazee ambao hatuoni vizuri megapixels 20!
 
vipi kamera ya huwei p6?

mkuu unajua hizi flagship zina camera ambazo ni za kawaida tu kwa ajili ya matumizi ya kawaida. huawei hawajatoa simu specific kabisa ya camera ndio maana sijaweka hapa.

camera ya p6 unaweza fananisha na simu kama s4. htc one, xperia z, lumia 920 hizo ndo level zake.
 
asante kwa somo
tufanye informed choice ya simu sasa thanx to chief-mkwawa
 
Last edited by a moderator:
Naona HTC umeichinjia baharini.

mkuu kama nilivojibu juu htc one kafocus kwa lumia inatoa picha nzuri low light ila picha mbaya mchana camera haina iq, same to lumia 920 same to gs4 hizi ni camera za kawaida na sio dedicated camera phone.

ona ui ya htc one ya camera
HTC-One-Camera-UI-5.png


ona ui ya lumia 920 ya camera
lumia920ui_091609175734.jpg


ona ui ya lumia 1020 ya camera
nokia-lumia-1020-camera.jpg


angalia hizo picha tatu hapo juu then skia point yangu. ukitaka kuchange iso au white balance kwenye htc one au lumia 920
1. huoni camera unaingia kwenye menu
2. unaeka namba tu bila kujua effect namba inazotoa
3. ngumu kwa mtu asie proffesional

angalia ya lumia 1020 ni mistari na button una adjust huku unaona hii inamfanya kila mtu awe pro camera hata mimi na wewe, so hapa unaona kuna cameraphone na simu zenye camera ya kawaida
 
mkuu kama nilivojibu juu htc one kafocus kwa lumia inatoa picha nzuri low light ila picha mbaya mchana camera haina iq, same to lumia 920 same to gs4 hizi ni camera za kawaida na sio dedicated camera phone.

ona ui ya htc one ya camera
HTC-One-Camera-UI-5.png


ona ui ya lumia 920 ya camera
lumia920ui_091609175734.jpg


ona ui ya lumia 1020 ya camera
nokia-lumia-1020-camera.jpg


angalia hizo picha tatu hapo juu then skia point yangu. ukitaka kuchange iso au white balance kwenye htc one au lumia 920
1. huoni camera unaingia kwenye menu
2. unaeka namba tu bila kujua effect namba inazotoa
3. ngumu kwa mtu asie proffesional

angalia ya lumia 1020 ni mistari na button una adjust huku unaona hii inamfanya kila mtu awe pro camera hata mimi na wewe, so hapa unaona kuna cameraphone na simu zenye camera ya kawaida
nimeppenda ufafanuzi wako,ila mimi bado concern yangu ileile nina hamu sana kuona nani atapata likes yako ya kwanza as mpk sasa una likes given 0
 
Back
Top Bottom