Call for interview Erolink

mundu mkongwe

Member
Joined
Feb 26, 2015
Posts
45
Reaction score
16
Nilipeleka CV erolink week iliyopita leo nimepigiwa sim nikafanye interview ya vodacom customer care.

Najua wapo wadau humu waliowahi kufanya interview pale.naomba dondoo muhimu kama mshahara wa vodacom customer care, majukumu ya customer care!
 
Kwa kuanza nenda upate experience but sio watu wa kuaminika.
 
mshahara ni laki tatu hadi mbili na nusu ,training ya bil malipo wala chakula ya mwezi na nusu ,karibu.
 
Nenda ukapasuke masikio huko
Bora ukalime vitunguu ruvu ndg yangu utatusua.
 
Hao jamaa huwa wanaita tu kufanya interview na mara nyingi si kwamba kazi zinakuwepo moja kwa moja, unaenda na kufanya writen interview, ukishinda unaweza kaa hata miezi 3 au zaidi tena ukaitwa na kufanywa oral ukishinda unaweza kaa hata miezi 6 tena au zaidi ndo ukajaitwa kwa kazi, huwa wanawaweka reserve hadi voda wawe na uhitaji wa watu. Nenda kafanye kila lakheri.

NB: Pia unaweza ukafanya na moja kwa moja ukaingia kazini.
 
asante mkuu Tamalisa ndio nasubiri paper sasahivi nitaleta report baadae.
 
hongera sana , kuliko kukaa home ni bora kutoka tu ukanyooshe miguu
 
Kafanye tu, lakini ndio ujue customer care ukilipwa 500,000 basi jua 270,000 wanakula erolink iliyobaki ndio yako.....
 
nibora ya hawa ya erolink wanaita kwenye interview recruitment agency nyingine ukipeleka cv sahau kabisa kuitwa kwenye interview ingawa wanabana kwenye payment ila bora kukomaanao huku unaangalia michongo mingine kuliko kushinda kijiweni na watu wasionda shule yaaan huambulii kitu siku nzima
 
Nimefanya interview ya erolink hapo moroco na nilipata kazi customer care voda m. City nikafanya miezi 11 nikapata serikalini so nikaacha voda.

Kama una shida ya kazi nenda kafanye interview hawana ubaguzi na yupo dada niliesoma nae chuo yuko hapo ndie anaentervier watu wa customer care. Kuhusu maswali yao ww pitia products na services wanazotia voda hakika hutashindwa kwwnye interview.
 
Jamani mm nimefanya nao kazi wanayokukata hawakati direct kwenye mshahara na ukifika kabla ya interview watakuambia kazi na mshahara kama utaridhia utafanya interview usipotaka basi.

Na pia wanalipa kwa masaaa uliyofanya kazi nakumbuka kuna wakati nililipwa hadi 570,000 kama ukipata bonus na overtime mshahara unaongezeka cha msingi uwe punctual hakikisha calls zako ni nzuri na muda wa kuingea na mteja ni dk ngapi na adherence kiujumla
 
asante mkuu lufuo nimeshafanya interview na nimefaulu training inaanza leo ijumaa
 
kupeleka cv erolink ni lazima uwe umesomea customer care tu au hata mtu wa course yoyote anaweza kwenda?
 
course yoyote unaweza kupeleka. ila inabidi uwe tayari kufanya kazi yoyote itakayolewa sio lazima iwe customer care
 
panda gari linalokwenda mwenge shika moroco airtel chukua bodaboda hadi office zao zilipo ni 1000 tu ukitumia bodaboda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…