CAG ni Mkaguzi tu, si MDHIBITI

CAG ni Mkaguzi tu, si MDHIBITI

Kwa ripoti yako kila mwaka kugubikwa na madudu huko Halmashauri na taasisi za Serikali na hakuna kinachofanyika baada ya hapo mpaka uje na ripoti nyingine (mwaka unaofuata) ya madudu yale yale ama kuzidi! Ni sahihi kukuita wewe ni MDHIBITI? kwa lipi? Nafikiri ungebaki na AUDITOR GENERAL (AG) tu ingekuwa poa mno.
Hapo ndipo Kafulila anasema CAG anapaswa kujua fedha zinapotelea wapi??!
 
Hivi wale internal auditors wako idara gani?
 
Kabla ya kudai katiba mpya tuwe na hoja kama hizi vinginevyo tutaletewa katiba isiyojibu kiu yetu.
 
Basi kama unaona CAG hafanyi kazi yake,basi nenda kaombe uwe wewe mkuu maana inaonekana wewe ni mtaalamu kumzidi yeye.
 
Kwa ripoti yako kila mwaka kugubikwa na madudu huko Halmashauri na taasisi za Serikali na hakuna kinachofanyika baada ya hapo mpaka uje na ripoti nyingine (mwaka unaofuata) ya madudu yale yale ama kuzidi! Ni sahihi kukuita wewe ni MDHIBITI? kwa lipi? Nafikiri ungebaki na AUDITOR GENERAL (AG) tu ingekuwa poa mno.
Kweli kabisa na hata hiyo nafasi ya Auditor General imepata meno kiasi fulani baada ya mashinikizo toka kwa mashirika ya fedha ya kimataifa na nchi wafadhiri, vinginevyo nafasi ya Auditor General ktk nchi za kiafrika ni kama OBSERVERS tu.
 
Hivi wale internal auditors wako idara gani?
Internal auditor general, ni ofisi mpya Una mda kidogo ila haijulikani sana,
Ma internal auditor wote wanatakiwa waondolewe Kwa waajiri wao, yaani unakuta internal auditor wa wizarani yupo chini ya katibu mkuu, halafu anamkagua bosi wake , wanapata shida Sana hawa watu kufanya kazi zao, hivyo Kwa sasa wanajua wanajitegemea Chini ya ofisi ya internal auditor general, Kwa mtazamo wangu naona ni kama duplication ya kazi ya CAG.
 
nakubaliana na mtoa mada, CAG ni Auditor tu hadhibiti chochote madudu yale yale ya miaka yoooote, hatua sifurii. Pengine iwepo CONTROLLER of BUDGET (independent office/institution) ili twende sawa.
kwa serikali ya sasa kuweka UVCCM ndo wakurugenzi wa halmashauri lazima iwe shida kila mwaka
 
Kwa ripoti yako kila mwaka kugubikwa na madudu huko Halmashauri na taasisi za Serikali na hakuna kinachofanyika baada ya hapo mpaka uje na ripoti nyingine (mwaka unaofuata) ya madudu yale yale ama kuzidi! Ni sahihi kukuita wewe ni MDHIBITI? kwa lipi? Nafikiri ungebaki na AUDITOR GENERAL (AG) tu ingekuwa poa mno.

Kabisa ninakubaliana na hoja yako mkuu CAG anafanya post-mortem (audit) tu hakuna cha ziada. Kwenye abbreviation CAG kama ulivyosema C (Controller) iko dormant au imekufa kabisa hakuna inachofanya vinginevyo watu wasingemisbehave kiasi hiki kwenye nidhamu ya fedha. Tunakuwaje na Controller na bado serikali ikope 500 billion Zaidi ya sheria ya budget? Malipo ya madeni hewa ya mabillion yanafanyika na utumbo mwingine wa kumwaga na bado tunasema tuna Controller General???. Ipo haja ya kuiangalia upya hii sheria kama tunataka kutoka hapa tulipo.
 
Back
Top Bottom