CAG Mfano wa Kuigwa kwa Wasomi

CAG Mfano wa Kuigwa kwa Wasomi

‘...Tatizo la Ma Profesa wanaona wote wasio ma Profesa kama Mbuzi...’-Job Ayoub ndugai

‘...Kule Duniani kama sio kwenye Mdahalo hatukuiti Dr au Profesa...’ -Ndugai

‘... Namshauri aende akamuombe Radhi mh. Rais DOCTOR John Pombe Magufuli...’ -Yule Yule Ndugai
 
Mwakajana mbunge Msukuma aliwahi kueleza Bungeni kuwa mambo makubwa katika nchi hii yamefanywa na watu wasio wasomi, watu walioshia darasa la 7 ukilinganisha ba wanaojiita wasomi. Aliyaongea hayo wakati akipigania watendaji wa vijiji walioishia darasa la saba warudishwe kazini.

Pamoja na ukweli kuwa Mbunge Musukuma mara nyingi kauli zake hukosa weledi lakini katika hili kwa kiwango fulani alikuwa sahihi.

Kati ya watu ambao hawana mchango mkubwa katika Taifa hili ni hawa wanaoitwa 'wasomi', hapa ndiyo tunawapata wale wenye titles za Dr. na Prof.

Tumeshuhudia, mara kadhaa, hawa wanaoitwa wasomi, wakiteuliwa kwenye nafasi za uongozi katika serikali. Wengi wao walipoingia huko waliishia kuwa walamba viatu vya wale waliowateua na hakuna chochote kipya walichokipeleka badala ya baadhi yao kwenda kudhihirisha unafiki, woga, ukigeugeu na kukosa misimamo hata katika mambo ambayo waliwahi kuyanena kwa vinywa vyao wenyewe.

Sifa kubwa ya msomi wa kweli ni kujitambua, kujiamini na kusimama katika yale unayoyaamini.

Leo hii tujiulize, ni Doctor (PhD) na Professor (ukimwacha Musa Assad) gani ambaye daima amewahi kusimama katika yale anayoyaamini bila kugeuka na kuyakana yale aliyokuwa akiyanena kabla ya kuteuliwa kwenye nafasi za uongozi? Ni msomi gani ambaye alipoteuliwa, utendaji wake ulidhihirisha utofauti wa yeye aliye msomi na viongozi wengine wenye elimu ya kawaida? Je, ni Bashiru au Kabudi?

Sidhani kama kuna awamu ya utawala iliyojaza madokta na maprofesa kama awamu ya 5. Lakini ni awamu hii ndiyo imekuwa na sera mbaya za uchumi zinazofukuza uwekezaji, kupalilia umaskini, kuongeza shida ya ajira, kupunguza mauzo ya ndani na nje, na kuua mzunguko wa fedha.

Ni awamu hii ndiyo yenye mfumo wa utawala holela. Mkuu wa wilaya, Mkoa au Waziri anaweza kusimamisha uzalishaji wa kiwanda au mgodi wakati hana mamlaka ya kisheria, anaweza kumweka ndani mtu yeyote hata kwa masuala ambayo yangeweza kufikishwa mahakamani kwa mfumo wa kisheria wa kawaida.

Ni awamu hii, watawala wanaamini kuwa wananchi ni kama wanyama, wanaweza kuwaswaga kadiri wao wanavyotaka bila ya kuzingatia sheria na katiba.

Ni awamu hii matamko ya Rais yanageuzwa kuwa ni sheria hata kama yapo kinyume na katiba. Lakini ndani ya serikali kuna madokta na maprofesa kibao ambao badala ya kumshauri, kumrekebisha na hata kumuonya Rais na viongozi wengine pale ambapo utendaji wao ni kinyume na katiba, ni kinyume na kanuni za uchumi au kinyume na utawala bora, wao ndio wamekuwa vinara wa kushangilia kila linalonenwa na watawala.

Watanzania, yawezekana kwa mara ya kwanza, wanaoneshwa na Prof. Musa Assad, namna wasomi wanavyotakiwa kuwa.

Prof. Musa Assad, tunampongeza kwa mambo yafuatayo:

1) Kuzingatia mamlaka ya kazi yake kwa mujibu wa katiba na siyo matakwa ya mtu au kikundi fulani

2) Kujiamini kwake katika yale ambayo yupo sahihi

3) Kuongea ukweli kwa kile anachokiamini

4) Kutokuwa na papara na kuwa mropokaji

5) Kuwa mwadilifu na mkweli kwa nafsi yake na Mungu anayemwamini

Tunahitaji wasomi wa namna hii. Wanaofanya kazi kwa mujibu wa sheria na katiba lakini walio jasiri kuyanena yaliyo sahihi hata kama kuna watu hayawapendezi.

Kwa upande mwingine, tuna aibu ya Taifa. Mheshimiwa Ndugai na Bunge ni aibu ya Taifa letu. Mtu asiyejua kuwa kila mtu na kila taasisi yoyote ina weaknesses na strengths zake, na ndiyo maana kunakuwa na improvements programs. Ndugai hajui hayo. Bunge halijui hayo. Kama kweli Bunge letu na speaker, hawayajui haya, basi wana udhaifu wa hali ya juu, au sasa wameanza kuwa zaidi ya DHAIFU.
Yaani baada ya tukio la kuzozana na ofisi ya Bunge Assad amekuwa ni mfano mwema? Kwani ameanzia kazi ofisi ya CAG? Je, umezipitia kazi zingine alizowahi kufanya na kuridhika kwamba huyu ni mfano wa kuigwa?

Ni tatizo letu wa-TZ. Hata wacheza mpira, wakifanya vizuri mechi moja tu, kelele nyiiingi na kuamini kiwango cha mchezo kimepanda, kumbe hoi.

Assad ni mdhaifu kama wengine tu. Huko NSSF tulishasikia alifanya madudu kama vichaa wengine tu!
 
Mbona alipotaka kubomoa jengo la Tanesco pale Ubungo makutano alizuiwa, ilikuwaje katika uuzwaji nyumba za serikali ambazo zilikuwa zimeisha depreciate mpaka negative value kiasi cha serikali kutumia gharama kubwa kuzitunza, Mh. Waziri mwenye zamana wakati huo kwa nini hakuzuiwa?
Majibu mnayo huko huko. Sisi walipa kodi tunachojua ni kwamba, nyumba ziliuzwa na jengo la Tanesco halikubomolewa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumeshuhudia, mara kadhaa, hawa wanaoitwa wasomi, wakiteuliwa kwenye nafasi za uongozi katika serikali. Wengi wao walipoingia huko waliishia kuwa walamba viatu vya wale waliowateua na hakuna chochote kipya walichokipeleka badala ya baadhi yao kwenda kudhihirisha unafiki, woga, ukigeugeu na kukosa misimamo hata katika mambo ambayo waliwahi kuyanena kwa vinywa vyao wenyewe.
Tuwe waangalifu kwenye hili. Assad anastahili sifa anazopata nami kuna uzi nilimpongeza, lakini ni kweli pia kuwa Assad ana ofisi inayolindwa kikatiba na kisheria hivyo ni rahisi zaidi kwake kuwa na msimamo na kulinda ajira yake na offisi ya CAG. Hao wengine ni vigumu sana kumtumikia kafiri na usufuate mambo yake. Bahati mbaya hawana ulinzi wowote kwa hiyo wengi hukubali tu kufunika kombe mwanaharamu apite.
 
"Sipo ccm,chadema,act wazalendo n.k lakini ni mpiga kura ninayejitambua"CAG Ni msomi anayeitendea haki taaluma yake. Ndugai DHAIFU
Hakuna haja ya kujieleza sana sentensi ya msingi ni hii "CAG Ni msomi anayeitendea haki taaluma yake." toshaa!
 
Tuwe waangalifu kwenye hili. Assad anastahili sifa anazopata nami kuna uzi nilimpongeza, lakini ni kweli pia kuwa Assad ana ofisi inayolindwa kikatiba na kisheria hivyo ni rahisi zaidi kwake kuwa na msimamo na kulinda ajira yake na offisi ya CAG. Hao wengine ni vigumu sana kumtumikia kafiri na usufuate mambo yake. Bahati mbaya hawana ulinzi wowote kwa hiyo wengi hukubali tu kufunika kombe mwanaharamu apite.
Majaji Vipi Mkuu?
 
Majaji Vipi Mkuu?
Majaji nafikiri wako relatively better off (ukilinganisha na wakina sisi ) kwa upande wa protection kama kuna tatizo liko pale kwenye kulipa fadhila. Yaani anachaguliwa mtu ambaye ana matatizo hivyo akikaa kwenye kiti ajuacho ni kulipa fadhila, lakini akitaka kufanya kazi yake kwa weledi si rahisi kumtoa.
 
Yaani baada ya tukio la kuzozana na ofisi ya Bunge Assad amekuwa ni mfano mwema? Kwani ameanzia kazi ofisi ya CAG? Je, umezipitia kazi zingine alizowahi kufanya na kuridhika kwamba huyu ni mfano wa kuigwa?

Ni tatizo letu wa-TZ. Hata wacheza mpira, wakifanya vizuri mechi moja tu, kelele nyiiingi na kuamini kiwango cha mchezo kimepanda, kumbe hoi.

Assad ni mdhaifu kama wengine tu. Huko NSSF tulishasikia alifanya madudu kama vichaa wengine tu!
Weka hapa hadharani hayo madudu yake badala ya kukatatika mauno tu.

Kwanza hakuna sehemu Proffesa amesema yeye hana udhaifu wowote, yule ni Alhaj anajuwa ni Mungu tu ndio aliyemkamirifu.

You're listening too slowly son.
 
Assad, atunukiwe tuzo ya Msomi BORA WA KARNE 21, najua JKN alikuzaliwa na kufa KARNE YA 20, Assad ni wa karne ya 21.
 
‘...Tatizo la Ma Profesa wanaona wote wasio ma Profesa kama Mbuzi...’-Job Ayoub ndugai

‘...Kule Duniani kama sio kwenye Mdahalo hatukuiti Dr au Profesa...’ -Ndugai

‘... Namshauri aende akamuombe Radhi mh. Rais DOCTOR John Pombe Magufuli...’ -Yule Yule Ndugai
Hizi kauli zinaakisi umaskini wa mtu flani. Na sisemei umaskin wa mali. Naamini umaskini ni state of mind. Hupend kuona wenzio wamekuzi.. wakikuzid unalalamika.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani baada ya tukio la kuzozana na ofisi ya Bunge Assad amekuwa ni mfano mwema? Kwani ameanzia kazi ofisi ya CAG? Je, umezipitia kazi zingine alizowahi kufanya na kuridhika kwamba huyu ni mfano wa kuigwa?

Ni tatizo letu wa-TZ. Hata wacheza mpira, wakifanya vizuri mechi moja tu, kelele nyiiingi na kuamini kiwango cha mchezo kimepanda, kumbe hoi.

Assad ni mdhaifu kama wengine tu. Huko NSSF tulishasikia alifanya madudu kama vichaa wengine tu!
Huko NSSF kwann msimshtaki? Assad hajakataa kuitws dhaifu. Hata waziri wabiashara na viwanda amesema leo kuna udhaifu kwenye wizara yake.. ndio kusema dhaifu ni dhambi?
alichoonyesha CAG ni msimamo.. kwamba dispite of all odd hajapanick.. ametekeleza majukum yake huku akiwa underpressure. Tofauti na yule bwana mwingine.
Cha pili anatuufundisha wasomi kuwa wakweli.. wasomi wengi wasasa wakiwa nje ya siasa wanasema kweli..wanakosoa wanahoji.. subiri wapate vyeo.. ni kusifu kuabudu serikal

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuwe waangalifu kwenye hili. Assad anastahili sifa anazopata nami kuna uzi nilimpongeza, lakini ni kweli pia kuwa Assad ana ofisi inayolindwa kikatiba na kisheria hivyo ni rahisi zaidi kwake kuwa na msimamo na kulinda ajira yake na offisi ya CAG. Hao wengine ni vigumu sana kumtumikia kafiri na usufuate mambo yake. Bahati mbaya hawana ulinzi wowote kwa hiyo wengi hukubali tu kufunika kombe mwanaharamu apite.

Jaji mkuu naye tatizo ni nini?
 
1. Ukichunguza vizuri, kuna uwezekano CAG alili 'provoke' Bunge na Spika kwa ujumla. Kwa nini nasema hivyo? Ni kwa sababu CAG alitoa kauli ya udhaufu wa Bunge muda kitambo kidogo, kabla Spika Ndungai hajaamua kutangaza kumuita CAG kwenye kamati ya maadili tena kwa maneno makali. Kwa maneno mengine, kuna uwezekano zilitumika juhudi za kidiplomasia kati ya Bunge na Ofisi ya CAG ili kumaliza tatizo hili lakini kwa tabia ambayo nimeielezea hapo awali ya CAG basi sieji akataka kuonyesha msuli tena sijui kwa mnaufaa ya nani. Ki urahisi ilitakiwa mbinu ya kushuka kwa upande mmoja ili ulingane na upande mwingine (CAG alikosa mbinu hii).

2. Katika suala lingine ningependa kujua ni utaratibu upi utumika kujiridhisha kuwa ripoti inayoandaliwa na CAG haina mapungufu na hakuna hila dhidi ya mkaguliwa?

3. Kwa nini majumuhisho ya ripoti ya CAG hayaanishi extreme best performance na extreme worst perfomance za wakaguliwa badala yake CAG anaonyesha worst performance za wakaguliwa tu. Baada ya ukaguzi, Ofisi ya CAG uchukua jukumu gani ili kuwasaidia wale waliopata hati chafu...ili waboreshe usimamizi wa fedha?

4. Je. tunaweza kuanza kufikiria kuwa CAG mara nyingi kwenye summary ya repoti yake husisitiza zaidi worst performance scenario ili kuifitinisha serikali iliyoko madarakani kwa wananchi ama huwa ana lengo gani hasa?
Wewe unazungumzia hisia. Lakini ukweli wa mambo ni tofauti na unavyodhania.

Baada ya ile taarifa kuwa cg amelitukana baraza letu tukufu, cg aliamua kuwasiliana moja kwa moja na ndugui, na yeye ndugui alimjibu, tena kwa lugha ya kirafiki kabisa kuwa hilo suala ni dogo, watalimaliza akirudi. Alimjibu kwa mesaage, na bado zipo. Wakati huo cg alikuwa nje ya nchi.

Baada ya cg kurudi toka nje, aliwasiliana moja kwa moja na ndugui. Na ndugui akamwalika nyumbani kwake saa 5 usiku pale jiji letu kuu jipya, tena cg alisafiri usiku, akafika jijini saa 4.30 usiki.. Wakaongea, na mwisho ndugui alimhakikishia cg kuwa suala hilo lilikuwa limekwisha.

Lakini kwa mshangao, baada ya kuambiwa jambo hilo limekwisha, baada ya siku chache kupita, akaambiwa wito wa kamati ya baraza upo pale pale. Cg akaitikia wito. Akahojiwa, naye akajibu kwa kueleza kuwa haikuwa nia yake kulidharau baraza tukufu kuwa ni nyoronyoro bali alijibu kufuatana na swali aliloulizwa, 'Kila mwaka unaandaa ripoti na kuonesha mapungufu yale yale, na mapungufu hayo hayafanyiwi kazi. Wewe utafanya nini kuhakikisha mapungufu unayoyagundua yanafanyiwa kazi? Naye akajibu kuwa, yeye anaandaa ripoti, akishaandaa anakuwa ametimiza wajibu wake. Ripoti inapelekwa barazani ambako yeye hana uwezo wa kuamrisha baraza lifanye nini. Kama baraza halifanyii kazi ripoti yake, basi huo ni unyoronyoro wa baraza na siyo ofisi ya cg'.

Na akafafanua kuwa unyoronyotlro ni neno ambalo lipo kwenye ripoti zake na za watangulizi wake, na ataendelea kulitumia neno hilo pale anapotakiwa kuulelezea upungufu. Kwenye maelezo hayo, kosa la cg ni nini?

Lakini baadaye ndugui amesema kuwa eti cg alisema kuwa ataendelea kuliita baraza ni nyoronyoro! Kwa nini ageuze maneno?

Jambo la pili, siyo kweli kuwa cg huwa haelezi maeneo ambayo yamefanyika vizuri. Soma ripoti yote utaona kuna maeneo anaonesha kuwa mwaka uliotangulia kulikuwa na hali fulani na sasa kuna ubora wa kiwango fulani.

Halafu jambo la tatu, taasisi zote zinazokaguliwa, huwa zinaelezwa mapumgufu yao, na namna ambavyo walistahili kufanya. Lakini taasisi iliyokaguliwa, ina nafasi ya kuomba msaada wa kitaalam kutoka ofisi ya cg hata baada ya ripoti ili kupata mafunzo namna ya kuweka mahesabu yao vizuri lakini otisi ya cg haiwezi kujipeleka mahali ambapo haijaombwa.
 
Yaani baada ya tukio la kuzozana na ofisi ya Bunge Assad amekuwa ni mfano mwema? Kwani ameanzia kazi ofisi ya CAG? Je, umezipitia kazi zingine alizowahi kufanya na kuridhika kwamba huyu ni mfano wa kuigwa?

Ni tatizo letu wa-TZ. Hata wacheza mpira, wakifanya vizuri mechi moja tu, kelele nyiiingi na kuamini kiwango cha mchezo kimepanda, kumbe hoi.

Assad ni mdhaifu kama wengine tu. Huko NSSF tulishasikia alifanya madudu kama vichaa wengine tu!
Usisikilize majungu. Namfahamu Musa Assad tangu akiwa Tutorial Assistant pale UDSM.

Huko NSSF hakuwahi kuwa mwajiriwa. Alikuwa mjumbe tu board. Maneno ambayo wajinga fulani wanadai eti alinunua nyumba ya NSSF ni upuuzi mtupu! Hivi kununua nyumba kwa kufuata utaratibu uliowekwa bila kukiuka shartinlolote, ni kosa? Watu wanatengeneza kashfa hewa ili kukidhi matakwa yao.

Kama kuna jinai yoyote dhidi ya Assad, si apelekwe mahakamani? Maana hana kinga yoyote dhidi ya jinai. Tena ingekuwa njia sahihi ya kuuthibitishia umma kuwa CAG amekosa uadilifu, na angeweza kuondolewa hata kwenye nafasi yake.
 
Tuwe waangalifu kwenye hili. Assad anastahili sifa anazopata nami kuna uzi nilimpongeza, lakini ni kweli pia kuwa Assad ana ofisi inayolindwa kikatiba na kisheria hivyo ni rahisi zaidi kwake kuwa na msimamo na kulinda ajira yake na offisi ya CAG. Hao wengine ni vigumu sana kumtumikia kafiri na usufuate mambo yake. Bahati mbaya hawana ulinzi wowote kwa hiyo wengi hukubali tu kufunika kombe mwanaharamu apite.
Una hoja ya msingi. Lakini wasomi kuna wakati wakati wanatakiwa kuchagua kati ya kutunza taaluma zao au kuwa watumwa wa matumbo yao.

Tijiulize, ni yeye tu ndiye mwenye kinga? Vipi kuhusu jaji mkuu? Vipi kuhusu majaji?
 
Inaonekana wengi mmechelewa kumfahamu Proffesa Assad, mwaka 2014 alishamuita jiwe political enterprenuer kwa kuuza nyumba za serikali.
Pamoja na kuwa mjasilia siasa lakini ccm wakakosa mtu wa kumpa nchi wakaona wampe mjasilia siasa .
 
Mwakajana mbunge Msukuma aliwahi kueleza Bungeni kuwa mambo makubwa katika nchi hii yamefanywa na watu wasio wasomi, watu walioshia darasa la 7 ukilinganisha ba wanaojiita wasomi. Aliyaongea hayo wakati akipigania watendaji wa vijiji walioishia darasa la saba warudishwe kazini.

Pamoja na ukweli kuwa Mbunge Musukuma mara nyingi kauli zake hukosa weledi lakini katika hili kwa kiwango fulani alikuwa sahihi.

Kati ya watu ambao hawana mchango mkubwa katika Taifa hili ni hawa wanaoitwa 'wasomi', hapa ndiyo tunawapata wale wenye titles za Dr. na Prof.

Tumeshuhudia, mara kadhaa, hawa wanaoitwa wasomi, wakiteuliwa kwenye nafasi za uongozi katika serikali. Wengi wao walipoingia huko waliishia kuwa walamba viatu vya wale waliowateua na hakuna chochote kipya walichokipeleka badala ya baadhi yao kwenda kudhihirisha unafiki, woga, ukigeugeu na kukosa misimamo hata katika mambo ambayo waliwahi kuyanena kwa vinywa vyao wenyewe.

Sifa kubwa ya msomi wa kweli ni kujitambua, kujiamini na kusimama katika yale unayoyaamini.

Leo hii tujiulize, ni Doctor (PhD) na Professor (ukimwacha Musa Assad) gani ambaye daima amewahi kusimama katika yale anayoyaamini bila kugeuka na kuyakana yale aliyokuwa akiyanena kabla ya kuteuliwa kwenye nafasi za uongozi? Ni msomi gani ambaye alipoteuliwa, utendaji wake ulidhihirisha utofauti wa yeye aliye msomi na viongozi wengine wenye elimu ya kawaida? Je, ni Bashiru au Kabudi?

Sidhani kama kuna awamu ya utawala iliyojaza madokta na maprofesa kama awamu ya 5. Lakini ni awamu hii ndiyo imekuwa na sera mbaya za uchumi zinazofukuza uwekezaji, kupalilia umaskini, kuongeza shida ya ajira, kupunguza mauzo ya ndani na nje, na kuua mzunguko wa fedha.

Ni awamu hii ndiyo yenye mfumo wa utawala holela. Mkuu wa wilaya, Mkoa au Waziri anaweza kusimamisha uzalishaji wa kiwanda au mgodi wakati hana mamlaka ya kisheria, anaweza kumweka ndani mtu yeyote hata kwa masuala ambayo yangeweza kufikishwa mahakamani kwa mfumo wa kisheria wa kawaida.

Ni awamu hii, watawala wanaamini kuwa wananchi ni kama wanyama, wanaweza kuwaswaga kadiri wao wanavyotaka bila ya kuzingatia sheria na katiba.

Ni awamu hii matamko ya Rais yanageuzwa kuwa ni sheria hata kama yapo kinyume na katiba. Lakini ndani ya serikali kuna madokta na maprofesa kibao ambao badala ya kumshauri, kumrekebisha na hata kumuonya Rais na viongozi wengine pale ambapo utendaji wao ni kinyume na katiba, ni kinyume na kanuni za uchumi au kinyume na utawala bora, wao ndio wamekuwa vinara wa kushangilia kila linalonenwa na watawala.

Watanzania, yawezekana kwa mara ya kwanza, wanaoneshwa na Prof. Musa Assad, namna wasomi wanavyotakiwa kuwa.

Prof. Musa Assad, tunampongeza kwa mambo yafuatayo:

1) Kuzingatia mamlaka ya kazi yake kwa mujibu wa katiba na siyo matakwa ya mtu au kikundi fulani

2) Kujiamini kwake katika yale ambayo yupo sahihi

3) Kuongea ukweli kwa kile anachokiamini

4) Kutokuwa na papara na kuwa mropokaji

5) Kuwa mwadilifu na mkweli kwa nafsi yake na Mungu anayemwamini

Tunahitaji wasomi wa namna hii. Wanaofanya kazi kwa mujibu wa sheria na katiba lakini walio jasiri kuyanena yaliyo sahihi hata kama kuna watu hayawapendezi.

Kwa upande mwingine, tuna aibu ya Taifa. Mheshimiwa Ndugai na Bunge ni aibu ya Taifa letu. Mtu asiyejua kuwa kila mtu na kila taasisi yoyote ina weaknesses na strengths zake, na ndiyo maana kunakuwa na improvements programs. Ndugai hajui hayo. Bunge halijui hayo. Kama kweli Bunge letu na speaker, hawayajui haya, basi wana udhaifu wa hali ya juu, au sasa wameanza kuwa zaidi ya DHAIFU.
Yap.
 
Back
Top Bottom