CAF yaamuru mechi ya fainali Simba Vs Berkane ichezwe New Amaan, Zanzibar Mei 25, 2025

CAF yaamuru mechi ya fainali Simba Vs Berkane ichezwe New Amaan, Zanzibar Mei 25, 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Wakuu!

CAF kupitia barua yao imewaambia TFF na Simba SC kuwa mchezo wa fainali ya pili ya CAFCC kati ya Simba dhidi ya Berkane ipigwe New Amaan Complex visiwani Zanzibar.

Pia, Soma: Mwana FA: Fainali ya Simba dhidi ya RS Berkane itachezwa Benjamin Mkapa

CAF imesema uamuzi huo ni baada ya kujiridhisha na ukaguzi wa uwanja wa Benjamin Mkapa katika vipindi vya mvua.

1747297192673.png
 
Taarifa za uzushi hizi, CAF siku zote wakiona kiwanja ulichochagua hakina vigezo wanakuambia uchague kiwanja kingine ili kucheza mechi yako. Iweje leo iwe tofauti na kuamuru mechi ichezwe sehemu fulani. Mm nakataa kabisa na nitakuwa mtu wa mwisho kuamini hili.
 
Madhara ya kuleta uchawa kwenye mambo ya msingi ndio haya.

Binafsi baada ya Simba kutinga fainali nikauliza fainali ya CAF ni jambo kubwa ni mojawapo ya vitu tunavyoweza kuvitumia kujitangaza kama nchi nikauliza mechi itachezwa wapi na uwanja wenyewe wa mkapa ndio kama vile tulivyoona ukigeuka kuwa shamba la mpunga? Nikajibiwa na Naibu waziri Mwana FA kuwa mkapa unakarabatiwa eti mkandarasi mbobevu kaajiriwa kufunga mabomba yanayotoa maji uwanjani nikajisemea muda utaongea

Mamia Samia alitumia mabilion kutengeneza royal tour Ili kuitangaza nchi Ina maana hii issue ya Simba kuingia fainali hawakuona kama ni mojawapo ya vitu vinavyoweza kuitangaza nchi?
 
➡️ CAF imewataarifu TFF kuwa mechi ya Fainali ya CAFCC kati ya Simba dhidi ya Berkane ipigwe New Amaan Complex Zanzibar

➡️ CAF imeeleza kuwa maamuzi hayo ni baada ya kujiridhisha na ukaguzi wa mara kwa mara wa hali ya uwanja wa Benjamin Mkapa katika kipindi cha mvua

IMG_3155.jpeg
 
Back
Top Bottom