Habari kwenu wataalamu, katika kujifunza C++
Nimejaribu kufanya mfano huu, lengo likiwa ni kuonesha maneno yanayojirudia knye sentensi, lakini sipati matokeo nnayoyahitaji.
Nnakosea wapi?
View attachment 2147837
Mkuu inamaana unataka kutafuta maneno yanayojirudia kwenye sentensi na si herufi kama ni maneno.
Kama kawaida unapoanza kutatua tatizo kupitia code kuna vitu inakubidi kuvibainisha kabla ya kuanza kuiandika code yenye.
Step 1:
What are the input to your program?
Hapa inakubidi kuangalia jee ni data gani unahitaji kuingia kama input ambapo kwenye Case yetu ni sentensi.
Mfano tutumie sentensi hii kama input
"Baba na mama wanakwenda dukani kununua vifaa vya shamba pamoja na chakula"
Step 2:
What are the output of the program?
Hapa tutaangalia tunategemea kupata nini kama output baada ya kuingiza input.
Kwa case yetu tunahitaji maneno yanayojirudia kwenye sentensi.
Kulingana na mfano wetu neno linalojirudia ni
"na"
Baada ya kuvitambua vitu hivyo ndipo sasa tuanze kudadavua namna tutavyoandika program yetu na itoe majibu tunayohitaji.
Kwanza kabisa kwa kuwa sentensi ina maneno mengi basi njia rahisi ya kuitunza sentensi ili tuifanyie kazi ni kwa kutumia array. Kwa hivyo tutapikea sentensi na kuitunza kwenye array.
Kisha baada ya kuwa na sentensi nzima sasa hapo ndipo tutaanza ku compare neno moja moja lilopo kwenye Kila index na index zingine na pale tutakapo baini kuwa neno limejirudia basi tutalitunza kwenye array nyingine ili baada ya hapo tutoe jibu Kwa pamoja ni neno gani limejirudia.
Sasa kutokana na hayo maelezo nikipata muda nitaandika code Kisha ntaipost hapa.