MJUMBE WA NCHI
Member
- Jan 2, 2015
- 53
- 23
Ikiwa mkoa wa mwanza unajiandaa kuanza zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kwa mfumo wa bvr baadhi ya wilaya maandalizi yanafanywa katika hali inayotiashaka.jana na leo nimepita katika wilaya za misungwi na kwimba,nimeshangaa kuona maandalizi ya zoezi hili yanavyoendelea bila wananchi kuwekwa wazi kwa mambo ya msingi yanayotakiwa kujulikana wazi.kwa mfano katika maeneo niliyopita wananchi hata hawajui wataandikishwa lini ilihali katika halmashauri maandalizi yanaendelea kwa kasi.leo lipo jambo lililoshangaza wengi kwa wale waliolifahamu katika wilaya ya kwimba,nalo si lingine bali ni la tangazo la kazi ya uandikishaji la bvr kit operator na mwandikishaji msaidizi lililobandikwa leo lenye dedline ya kesho.yaani watu walifanyie kazi ndani ya masaa 24 tu na tangazo liko makuu ya wilaya tu.mchakato huu unatia shaka kwa wale wanaoona mbali.iweje suala lenye maslahi kwa taifa zima liende kwa utaratibu wa kimyakimya huku suala la hamasa vikiachiwa vyama vya siasa vinavyofanya kwa maslahi yao ya vyama?