Kiba
JF-Expert Member
- Mar 23, 2012
- 459
- 62
Leo katika mji mdogo wa lamadi katika jimbo la Busega mkoani Simiyu FFU wametanda kila kona baada ya polisi kumkamata mwenyekiti wa vijana CHADEMA mkoa wa Simiyu na viongozi wengine wa chama hicho usiku wa kuamkia leo.
Chanzo cha kukamatwa viongozi hao ni baada ya CCM kuweka pingamizi kwa wagombea wote wa CDM katika kugombea nafasi katika uongozi wa kijiji hali ambayo ilichafua hewa na kufanya wananchi kuvunja ofisi ya kata ili wammalize mwanasheria wa wilaya aliyekua amerudisha majibu hayo mnamo tar 2 mwezi huu.
Kufuatia timbwilitimbwi hilo mwanasheria huyo aliwarudisha wagombea wote wa CDM chini ya masharti makali ya wananchi baada ya kuona kimenuka.
Hii leo asubuhi kufuatia viongozi hao kukamatwa wafuasi wa CDM walivamia kituo cha polisi ili kuwatoa ila viongozi hao hawakuwekwa katika kituo hicho cha polisi bali walipelekwa usiku huo huo mjini Bariadi katika kituo kikuu cha polisi.
Hadi kufikia majira ya mchana huu wananchi bado wanasubiri viongozi hao waletwe baada ya viongozi hao kuwashuhudia wananchi kwa njia ya simu kuwa wako salama na watapelekwa ktk mahakama ya Nyashimo ili kusomewa mashtaka na wakawaomba wananchi kwenda kuwawekea mdhamana kictendo ambacho kimeshafanyiwa kazi na viongozi wa CDM hivyo hapa wananchi wanasubiri kuwaona MAKAMANDA hao wakiwasili au LA.
Chanzo cha kukamatwa viongozi hao ni baada ya CCM kuweka pingamizi kwa wagombea wote wa CDM katika kugombea nafasi katika uongozi wa kijiji hali ambayo ilichafua hewa na kufanya wananchi kuvunja ofisi ya kata ili wammalize mwanasheria wa wilaya aliyekua amerudisha majibu hayo mnamo tar 2 mwezi huu.
Kufuatia timbwilitimbwi hilo mwanasheria huyo aliwarudisha wagombea wote wa CDM chini ya masharti makali ya wananchi baada ya kuona kimenuka.
Hii leo asubuhi kufuatia viongozi hao kukamatwa wafuasi wa CDM walivamia kituo cha polisi ili kuwatoa ila viongozi hao hawakuwekwa katika kituo hicho cha polisi bali walipelekwa usiku huo huo mjini Bariadi katika kituo kikuu cha polisi.
Hadi kufikia majira ya mchana huu wananchi bado wanasubiri viongozi hao waletwe baada ya viongozi hao kuwashuhudia wananchi kwa njia ya simu kuwa wako salama na watapelekwa ktk mahakama ya Nyashimo ili kusomewa mashtaka na wakawaomba wananchi kwenda kuwawekea mdhamana kictendo ambacho kimeshafanyiwa kazi na viongozi wa CDM hivyo hapa wananchi wanasubiri kuwaona MAKAMANDA hao wakiwasili au LA.