Burundi President says third term will be his last


Well said.
 
Kama Ameweza Kupindua Katiba Atashindwa Kupindua Matokeo Ya Kura?

Mkuu Nkurunzinza hajapindua katiba, kwani kapigiwa kura na Wananchi mara ngapi? Si mara moja tu - sasa akiwania Urais kwa mara ya pili kuna tatizo gani - si katiba inaruhusu mihula miwili na yeye anakubaliana na hilo. Watu wanataka kumsingizia kwamba kavunja katiba, wanajifanya kusahau kwamba aliteuliwa na Bunge kuongoza Nchi kabla katiba haijakamilika - hicho kilikuwa ni kipindi cha mpito hakuteuliwa na Wananchi kwani Warundi hawalijui hilo?

Raia walimpigia kura kwa mara ya kwanza miaka mitano/minne iliyopita hivyo katiba unamuruhusu agombee kwa mara ya pili ambayo itakuwa ndio mara yake ya mwisho. Mimi nawashauri raia wa Burundi wasikubali kutumiwa na watu wa nje kutaka kuleta vurugu ndani ya Taifa lao - Warundi washikamane wawe kitu kimoja - wasiruhusu wageni ku-instigate vurungu ndani ya Taifa lao, wageni wanataka mvurugane msielewane ili wao wapate nafasi ya kutekeleza ajenda zao za siri za muda mrefu.
 
Bwana Nkuruzinza..angeweka kwanza uroho wa madaraka pembeni na kuthamini nafsi za wasio na hatia zikiteketea....hata kabla ya kwenda kwenye box la kura hali halisi yenyewe inajidhihiri kuwa wananchi hawakutaki...sasa kwani unang'ang'ania....kwani kuna nini humo madarakani....anataka amuongoze nani kama waongozwa hawamtaki kiongozi....??
Kwa aina ya viongozi kama NKURUZINZA ndio ninapoona umuhimu wa THE HAGUE....
 
...bukya kweli uko sahihi! Na hao raia wasubiri kumtimua kwa kura kama hawataki kumpa 'ekisanja 'kingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…