Buriani Willson Kabwe

Bwana Mapesa

JF-Expert Member
Apr 28, 2011
2,551
1,777
Huyu alikuwa mlezi kwangu, ndiye aliyenitafutia shule wakati namaliza O level ili nianze safari ya kwenda advance level(alikuwa rafiki wa baba yangu mzazi na walishirikiana mengi pamoja na suala la elimu yangu) . Nilimjua kama msomi mwanasheria ambaye alikuwa mzoefu katika uongozi wa umma watu wa mbeya na kwingine alipopita wanaweza shuhudia hili (ingawa hakuna aliyekamilika mapungufu yanaweza kuwepo kwani ndo sifa ya kila mwanadamu). Niwe mkweli niliumia sana kusikia mkuu wa mkoa akimtaja kama mtu wa hovyo asiyeweza fanya nae Kazi pale kigamboni siku ya uzinduzi wa daraja la NYERERE. Niliumia zaidi sababu nilijua kuwa wakati ule marehemu alikuwa na hali mbaya kitandani nchini India. Siamini kama mkuu wa mkoa hakulitambua hili. Lakini katika kujiona msafi, mcha mungu akaamua kumpiga jiwe maiti, kwa hili nashindwa kuamini kama Makonda kweli ni mcha mungu, sababu kwa mtu yoyote mcha mungu asingeweza kuyafanya yale wakati anajua fika mzee Kabwe alikuwa kitandani. Hayo yamepita lakini imeniuma zaidi kuona mtu aliyepata sifuri O level na anayetumia vyeti sio vyake kumkataa mtu msomi, mwenye vyeti vyake na kufanikiwa kumtoa kwenye nafasi yake kwa aibu.
Makonda kama unataka ahueni katubu na muombe radhi marehemu Kabwe labda mizimu yake itaacha kukuandama. Umewakosea wengi ila hili la Kabwe litakutafuna milele.
Sasa nimeamini hakuna jiwe litakalo salia juu ya jiwe.
 
Wacha kelele wewe. Huyo Marehemu alitumbuliwa kwasababu ya vyeti vya Makonda au sababu ya wizi wake na mikataba ya figisu pale Ubungo?
Kutumbua mwizi wa mali ya umma haijalishi elimu ya kwenye makaratasi ya mtumbuaji. Hata angelikuwa kihiyo angelimdaka tu.
 
Wacha kelele wewe. Huyo Marehemu alitumbuliwa kwasababu ya vyeti vya Makonda au sababu ya wizi wake na mikataba ya figisu pale Ubungo?
Kutumbua mwizi wa mali ya umma haijalishi elimu ya kwenye makaratasi ya mtumbuaji. Hata angelikuwa kihiyo angelimdaka tu.
Punguza povu, halafu rudia kuandika
 
Wewe usituletee figisufigisu yeye apumzike kwa amani tu huko aliko ila ukweli ni kwamba alichotufanyia huku mwanza anajua mwenyewe na wahusika waliohusika na upigaji wa viwanja viwanja vya kliniki na jengo la makongoro
Kwa watu wa Kolomije lazima mje kwa style hii, hahaha viva Ngoshaz
 
Ninachojua kwenye Halmashauri zote anaye saini mikataba ni Mwenyekiti/Mayor wa Halimashauri husika. Sasa sijui kama Marehemu aliadhibiwa kwa yeye kusaini mikataba au kwa kuwa yeye akiwa nimtendaji mkuu wa halimashauri husika alishindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo kwenye mikataba. Ila haka kajamaa kameshiriki kikamilifu kudhalilisha taaluma za watu nahata mzee Kabwe kalimdhalilisha na hii nikwa sababu kalijiona kama kana zero nakakepewa ukuu wa mkoa kakajiona kanaweza kufanya lolote lile hata kama hakana utaalam wake!

Binafsi Bashite mwanzo nilimuona kama mchapakazi kumbe uchapakazi wake ulikuwa wa kujitutumua tu ili kaonekane kana jua kumbe kabwege tu! Hakuna kitu kinachouma kama kudhalilisha Professional ya mtu tena unadhalilishwa na mtu aliye ungaunga tu kama ndorobo
 
Wewe usituletee figisufigisu yeye apumzike kwa amani tu huko aliko ila ukweli ni kwamba alichotufanyia huku mwanza anajua mwenyewe na wahusika waliohusika na upigaji wa viwanja viwanja vya kliniki na jengo la makongoro

Alichowafanya Mwanza Kitu gani, wakati nyuma yake na mbele yake inasemekana kulikuwa na mkono mrefu wa serikali, kama Mwanza aliharibu yeye kama yeye mbona Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa haikumtia hatiani? Siasa ndo zinazotuharibu nchi hii!
 
Wacha kelele wewe. Huyo Marehemu alitumbuliwa kwasababu ya vyeti vya Makonda au sababu ya wizi wake na mikataba ya figisu pale Ubungo?
Kutumbua mwizi wa mali ya umma haijalishi elimu ya kwenye makaratasi ya mtumbuaji. Hata angelikuwa kihiyo angelimdaka tu.
Aliye mshutumu hakuwa na uhalali wa kufanya vile.. Alitakiwa awe dereva wa Kabwe na si boss wa Kabwe kwa mujibu wa Magufuli
 
Wacha kelele wewe. Huyo Marehemu alitumbuliwa kwasababu ya vyeti vya Makonda au sababu ya wizi wake na mikataba ya figisu pale Ubungo?
Kutumbua mwizi wa mali ya umma haijalishi elimu ya kwenye makaratasi ya mtumbuaji. Hata angelikuwa kihiyo angelimdaka tu.
Mlimpeleka mahakama ipi marehemu Kabwe akapatikana na hatia?

Halafu msomi wa div 0 na digrii ya kusaidiwa ana uwezo gani wa kufanya maamuzi?

Na Sizonge sasa aibu yake, wenye haki zao alizozikanyaga wamemwachia Mungu. Atapambana na kisasi cha Mungu
 
Ninachojua kwenye Halmashauri zote anaye saini mikataba ni Mwenyekiti/Mayor wa Halimashauri husika. Sasa sijui kama Marehemu aliadhibiwa kwa yeye kusaini mikataba au kwa kuwa yeye akiwa nimtendaji mkuu wa halimashauri husika alishindwa kutekeleza majukumu yake ipasavyo kwenye mikataba. Ila haka kajamaa kameshiriki kikamilifu kudhalilisha taaluma za watu nahata mzee Kabwe kalimdhalilisha na hii nikwa sababu kalijiona kama kana zero nakakepewa ukuu wa mkoa kakajiona kanaweza kufanya lolote lile hata kama hakana utaalam wake!

Binafsi Bashite mwanzo nilimuona kama mchapakazi kumbe uchapakazi wake ulikuwa wa kujitutumua tu ili kaonekane kana jua kumbe kabwege tu! Hakuna kitu kinachouma kama kudhalilisha Professional ya mtu tena unadhalilishwa na mtu aliye ungaunga tu kama ndorobo
Kama mzoefu kwenye ofisi za umma, watu wote ambao professionally ni incompetent huwa na hulka ya kujitutumua the likes of Bashite... Wanafunika mtego na majani.
 
Mkiwa mnafanya ufujaji na wizi wa mali za umma huwa hamna huruma ya kuwa pesa na raslimali mnazoiba kuna watu wanaumia na kukosa baadhi ya huduma mkitumbuliwa mnarudi kwa wananchi kulialia ya kuwa mnaonewa mara busara haikutumika wakati nyie mnaiba mbona huruma na busara hamkutumia
 
Alichowafanya Mwanza Kitu gani, wakati nyuma yake na mbele yake inasemekana kulikuwa na mkono mrefu wa serikali, kama Mwanza aliharibu yeye kama yeye mbona Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa haikumtia hatiani? Siasa ndo zinazotuharibu nchi hii!
Kabwe was a sacrificial lamb... (Kondoo wa kafara). Nahis kuna watu walitamani Kabwe afe haraka ili wafiche maovu yao, siamini hata kulikuwa na ufisadi eti Kabwe alihusika peke yake.. Watu waliona anachelewa kufa wakaona wa accelerate kifo chake kupitia bwana mdogo Bashite wakati marehemu yu kitandani.
Angalizo :Najaribu kuhisi baada ya hili sakati la ubaguzi wa wauza madawa na watumiaji madawa.
 
Uliwahi kukuona huo mkataba? Pale daraja la NYERERE? Mkataba alisaini peke yake... Think before you comment... Jamaa alikuwa mahututi kitandani was it fair to be treated in such a way, tena kwa tuhuma tuu.
Makonda alimuambia mh. Rais mbele ya kadamnasi kuwa jamaa kasign. Sasa wewe unabisha nini!!? Unataka kusema Makonda alimpa mh rais taarifa za uongo!!? Kwa hiyo unataka kusema ugonjwa ndo unamuondolea mtu makosa aliyoyafanya!!? Napata tabu kuhusu uelewa wako wa mambo
 
Makonda alimuambia mh. Rais mbele ya kadamnasi kuwa jamaa kasign. Sasa wewe unabisha nini!!? Unataka kusema Makonda alimpa mh rais taarifa za uongo!!? Kwa hiyo unataka kusema ugonjwa ndo unamuondolea mtu makosa aliyoyafanya!!? Napata tabu kuhusu uelewa wako wa mambo


Makonda yawezakuwa alimdanganya Rais, fuatilia issue nyingi kipindi akiwa Mkuu wa Wilaya Kinondoni, aliwahiwafukuwza wahandisi kazi kuwa walitengeneza barabara kwa gharama kubwa je wale wahandisi wapo wapi mbona wote wamerudishwa kazini japo kwenye kurudi hawakutangazwa hadharani kama alivyowasimamisha, tatizo bashite alibase kwenye uongo na majungu kuliko kufanya kazi na hasa alitaka kupandisha chati yake juu kwa haraka
 
yatasemwa mengi juu yake
lakini huyu ndio shujaa wa vita dhidi ya madawa ya kulevya
Ushujaa kumtaja Mbowe na Gwajima au? Wema Sepetu, TID, Mr. Blue hivi hawa wanafanana na kina El Chapo kweli?
images-1.jpeg

yatasemwa mengi juu yake
lakini huyu ndio shujaa wa vita dhidi ya madawa ya kulevya
Ushujaa kumtaja Mbowe na Gwajima au? Wema Sepetu, TID, Mr. Blue hivi hawa wanafanana na kina El Chapo kweli
Ndomana wakatajwa kina Manji wakaachwa kina Gharib
 
Back
Top Bottom