buhange
JF-Expert Member
- Oct 23, 2011
- 505
- 110
Ni sekunde, dakika, masaa, siku, miezi na miaka kadhaa sasa tangu mpendwa wetu Hayati Moringe Sokoine, Waziri mkuu wa zamani atutoke kwa ajali mbaya ya gari akiwa safarini kuelekea Dar es Salaam kutokea Dodoma, hatimaye leo tunaazimisha miaka kadhaa ya kifo chake, Kwa tuliokuwepo na ambao hatukuwepo kipindi cha utendaji wake, lakini tukiwa tumepata fursa ya kusikia aina ya uchapa kazi wake enzi zake!, Nini wito wako kwa viongozi wetu wa sasa ktk kumuenzi Mpigania haki huyu na maendeleo ya wanyonge ktk enzi hizo? Atakumbukwa daima.