MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 20,707
- 42,793
Jili jibu lako ni la kishenzi mno. Hii nchi haina mitaa ya waislamu wala wakristo. Hata huko unapopataja kunaweza kufunguliwa mabucha ya kitimoto na usifanye lolote. Ni vile tu kuheshimiana ila hakuna sheria inayokataza. Ficha upumbavu wako wewe mzee.Mashine...
Kila jamii ina maeneo yake ya asili.
Dar es Salaam ambako ndiyo kwetu nilikozaliwa naifahamu vyema kabisa.
Nimezaliwa Gerezani mwaka wa 1952.
Sasa anza hapo na tembea kote Kariakoo, Buguruni, Kinondoni, Temeke, Manzese, Ilala huna haja ya kuuliza hayo maeneo wenyewe ni nani?
Haya yote ni maeneo ya asili Mtaa wa Kipata nilipozaliwa mimi hadi leo kuna nyumba zina miaka 100.
Kote huko nilikotaja hapo juu hali ni hii.
Jibu hili naamini linajibu maswali yako mengine ya Wahindi nk.
Dar es Salaam Wakristo walitengewa Mission Quarter na ndiyo sehemu Dar es Salaam kulikuwa na kanisa Mtaa wa Masasi.
Mama...Mzee wetu ungeandika bila kuleta udini wako tungekuheshimu mno. Wewe mwenyewe ndo unalazimisha tukudharau. Kiukweli heshima yako hapa JF imeshuka mno. Halafu huwa najiuliza kwanini ukizidiwa hoja unaanza kuleta historia za nyumbani kwenu? Kwa mfano mtu aliuliza kwamba je Manzese ni eneo teule la kiislamu wewe ukajibu kuna ndugu zako walishaishi hapo.
Jili jibu lako ni la kishenzi mno. Hii nchi haina mitaa ya waislamu wala wakristo. Hata huko unapopataja kunaweza kufunguliwa mabucha ya kitimoto na usifanye lolote. Ni vile tu kuheshimiana ila hakuna sheria inayokataza. Ficha upumbavu wako wewe mzee.
Kwanini wakristo walitengwa eneo lao..kwanini waislamu hawataki kuchanganyika na wakristo.?''Mji wa Dar es Salaam katika miaka ya 1920 ulikuwa umegawanyika katika sehemu nne: Kariakoo, Gerezani, Kisutu na Misheni Kota.
Sehemu ya ukazi wa asili ilikuwa Kisutu. Kisutu ina msikiti wa zamani kuliko yote katika Dar es Salaam - Msikiti wa Mwinyikheri Akida, unaokaribia takriban miaka mia moja hivi.
Vilembwe wa Sheikh Mwinyikheri hadi leo wangali wakiuhudumia msikiti wa mzee wao na msikiti huo bado uko chini ya uangalizi wao.
Kariakoo ilikuwa sehemu ya kuandikisha wapagazi wakati wa Vita Kuu Vya Kwanza.
Jina lenyewe ëKarikaooí linatokana na jina la Kizungu, ''Carrier Corps.''
Misheni Kota ilikuwa sehemu iliyotengwa makhsusi na Waingereza kwa ajili ya Wakristo.
Wakati ule Wakristo hawakuwa wengi Dar es Salaam, kwa ajili hii walitengewa sehemu yao maalum ya kuishi ili wasichanganyike na Waislam.
Misheni Kota ilikawa sehemu ya kuishi Wakristo kiasi ambacho hata mitaa yake ilipewa majina ya sehemu katika Tanganyika ambako Wamishionari walikuwa wamejipenyeza na kuweka maskani.
Majina ya mitaa kama Masasi, Likoma, Ndanda, Muhonda, Muheza na Magila imedumu hadi sasa.
Hizi ni sehemu ambazo Ukristo ulishamiri.
Misheni Kota ndiyo sehemu pekee katika Dar es Salaam ambapo Wamisionari walifanikiwa kujenga kanisa.
Wakristo walitengewa katika sehemu hii kuwa makazi yao.''
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes).
View attachment 2307398
Wakoloni katika hila zao waliwagawa wananchi ili wapate kuwatawala vyema.Kwanini wakristo walitengwa eneo lao..kwanini waislamu hawataki kuchanganyika na wakristo.?
#MaendeleoHayanaChama
Sheikh,Mabucha yanayouza nguruwe sasa hivi iwe kavu o roast yapo au hakuna?BURIANI HASSAN CHIKUSA MSOMI MKIMYA
Naamini si wengi wanamfahamu Hassan Chikusa na yote yaliyomsibu katika maisha yake.
Mimi nilimjua Hassan Chikusa kwa kuwa alikua jirani yangu akiishi kwa ndugu yake Masaki jirani na nyumba niliyokuwa naishi mimi na familia yangu.
Wakati ule alikuwa kijana mdogo ndiyo kwanza amemaliza masomo yake na anafanya kazi Makao Makuu National Bank of Commerce (NBC), Sokoine Drive.
Tulizoeana sana na wakati mwingine akija nyumbani kwa mazungumzo na akipenda mazungumzo yangu katika vitabu, historia na muziki kama ilivyo kawaida ya vijana.
Hassan alikuwa akiweka shajara yaani akiandika, ''diary.''
Hassan alikuwa kijana akiipenda dini yake sana kwa mapenzi makubwa.
Mwaka wa 1993 pakawa na sakata la uvunjaji mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe Wilaya ya Kinondoni baada ya sala ya Ijumaa.
Kilichotokea ni kuwa kijana alitumwa nyama na muuza nyama pengine kwa kutokujua akamuuzia huyu kijana nyama ya nguruwe.
Palikuwa na malalamiko kuhusu haya mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe lakini walioshika madaraka hawakujali wala kutia maanani malalamiko ya Waislam.
Mjini Dar es Salaam kulikuwa na mabucha 29 ya kuuza nyama ya nguruwe kwenye sehemu wanazoishi Waislam na hii ilikuwa kinyume cha sheria.
Tatizo hili Waislam wakalifikisha kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mustafa Nyang;anyi lakini hakuna kilichofanyika na likafikishwa pia kwa Waziri Mkuu, John Samuel Malacela.
Waswahili wanamsemo wanasema yale yalikuwa sawa na kutwanga maji katika kinu.
Hili tatizo la mabucha likashushwa chini hadi kwa Mkuu wa Wilaya, Wilson Mkama na yeye akawaita ofisini kwake maimamu wa misikiti mitano ya Wilaya ya Kinondoni kwa mazungumzo.
Serikali haikuwa tayari kufunga mabucha hayo kwa kile walichokiona ni shinikizo kutoka kwa Waislam wenye, ''siasa kali.''
Bwana Mkama akawaeleza maimam kuwa hayo mabucha yapo kihalali na wana leseni walizopewa na serikali kufanya biashara hiyo kwa ajili hii serikali ina dhima ya kuzilinda hizo bucha.
Mkutano ukamalizika na maimamu wakarejea misikitini kwao kuwaeleza Waislam kauli ya serikali kuhusu mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe.
Waingereza wana msemo, ''The straw which broke the camel's back,'' yaani ujani uliowekwa juu ya mgongo wa ngamia ukauvunja.
Waislam walighadhibika sana kwa uamuzi wa serikali kuwapuuza.
Siku ya pili ilikuwa Ijumaa Kuu.
Baada ya sala ya Ijumaa vijana wa Kiislam walipomaliza sala waliziendea zile bucha zilizokuwa Wilaya ya Kinondoni wakazivunja zote kwa mpigo.
Dar es Salaam ilizizima.
Haya hayakupata kutokea katika kipindi chote cha uhuru.
Rais Ali Hassan Mwinyi akiwa Zanzibar akasema katika kulani kuvunjwa mabucha ya nguruwe kuwa nguvu za dola ziwaangukie wale waliovunja mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe.
Jioni yake BBC hwakuchelewa wakafanya mahojiano na Waziri Mkuu John Samuel Malecela.
Malecela akasema kuwa waliovunja mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe ni wahuni wanotaka kuchukua serikali kupitia dini.
Waziri wa Mambo ya Ndani na Naibu Waziri Mkuu Augustine Mrema yeye akasema mabucha yamevunjwa kutokana na nguvu kutoka nchi ya Kiislam ili kuivuruga Tanzania.
Katibu Mkuu wa CCM Horace Kolimba yeye akahitimisha kwa kusema kuwa waliovunja mabucha si Waislam ila ni wahuni wanaotaka kupindua serikali.
Kufika asubuhi siku ya Jumamosi masheikh 40 wakawa wamekamatwa usiku wa manane kwa taadhira kubwa majumbani kwao mfano wa majambazi na kutiwa korokoroni.
Wahariri wa magazeti asubuhi yake siku ya Jumamosi wakawa katika burdani kubwa ya kuandika kuvunjwa kwa mabucha ya kuuza nguruwe na kukamatwa kwa masheikh.
Asubuhi ile ya Jumamosi kundi dogo la Waislam wakaenda Kituo Cha Kati cha Polisi kufuatilia masheikh waliokamatwa usiku na kuwekwa korokoroni hapo.
Hawa nao wakakamatwa na kuwekwa ndani.
Haukupita muda baada ya habari kuenea kuwa Waislam waliokwenda kuwauliza masheikh na wao wamekamatwa Waislam wakaja kwa wingi kituoni siku ya pili yake Jumapili iliyokuwa Easter Sunday.
Siku hiyo Waislam wakakusanyika pale kituoni ikawa kama vile kituo kimezingirwa na sala ya L'Asr ilipoingia ikapigwa adhana pale nje ya ya kituo watu wakasali barabarani.
Polisi wakataka kuwapiga mabomu ya machozi lakini pakawa na kutokubaliana baina ya askari wenyewe.
Hawakupendezewa na kitendo kile.
Askari Waislam wakawaambia wenzao hilo haliwezi kufanyika kuwapiga mabomu Waislam wanaosali kwani ni kufuru kubwa Waislam hawajafanya fujo wamekuja kituoni kufuatilia masheikh wao walioko korokoroni.
Jua lilipotua Waislam wakaondoka pale kituoni wakaamua wakutane siku ya pili Msikiti wa Mtoro washauriane.
Siku hii ya Jumapili yaani Easter Sunday mimi ndiyo niliingia Dar es Salaam nikitokea Le Havre, Ufaransa nikaja Paris kwa muda wa siku mbili kisha nikaenda London kisha Cardiff na kurejea London kupanda ndege kurudi Dar es Salaam.
Nilipofika nyumbani ndipo nilipopata taarifa ya masheikh kukamatwa na kati ya masheikh hao alikuwa mjomba wangu Sheikh Pazi wa Manzese.
Sikusubiri nikaenda kwa Hassan Chikusa wakati huo akiishi Mwananyamala kwani nilijua pamoja na kupita kwa jamaa wengine yeye ndiye ataweza kunipa taarifa ya mkasa mzima pamoja na tathmini.
Hayo niliyoandika hapo juu ni baadhi ya mambo aliyonifahamisha kuwa yametokea kuanzia siku ile ya Ijumaa yalipovunjwa mabucha hadi siku ya pii yake Jumamosi.
Hili ninalosema sasa ni jambo ambalo kwa miaka yote kila nilipokutana na Hassan moyo uliniuma sana nikiishia kumuombea dua.
Hassan siku ile nilipokwenda kwake ilikuwa Jumapili usiku na hakuwa na taarifa kuwa siku ya Jumatatu, yaani Easter Monday Waislam wameamua kufanya shura ndani ya Msikiti wa Mtoro ambao Imam Mkuu, Sheikh Kassim Juma alikuwa kakamatwa Arusha akielekea Nairobi kwenye matibabu na kurudishwa Dar es Salaam na yuko rumande.
Mimi ndiye nliyemfahamisha kuwa kesho Easter Monday kuna shura ya Waislam wote wa Dar es Salaam kujadili kwa pamoja nini kifanyike kurejesha heshima ya masheikh wetu.
Hassan aliniuliza kama mimi nitakuwepo.
Nikamwambia In Shaa Allah nitakuwapo.
Hassan Chikusa na yeye akaniambia atakuwapo pia.
Kwa ufupi siku ile ndani ya Msikti wa Sheikh Mtoro Mwinyi Mangara iliamriwa baada ya mjadala mkali sana Waislam watoke kwa maandamano hadi Kituo Cha Kati Cha Polisi kwenda kuwatoa masheikh wao korokoroni.
Katika maandamano yale Waislam walipambana na polisi na mabomu ya machozi yalipigwa.
Mapambano haya yalifanyika kati ya kituo cha polisi na Clock Tower.
Haya ndiyo yalikuwa maandamano ya kwanza ya Waislam Tanzania Bara.
Zanzibar maandamano yao yalikuwa mwaka wa 1988.
Maandamano haya yote tatizo ni Uislam.
Hassan Chikusa akakamatwa pamoja na vijana wengi wa Kiislam.
Wakawekwa rumande wakashtakiwa na kuhukumiwa vifungo jela.
Hassan Chikusa akapoteza kazi yake NBC.
Huyu ndiye Hassan Chikusa msomi mkimya ambae baada ya kutoka jela akiwa hana kazi masahibu mengi ya maisha yalimfika.
Lakini siku zote akisema yaliyomfika ni madogo sana na yote ameyakadiria Allah na na yeye bado yu hai.
Kwangu mimi maadamano yale na wale walioshiriki katika yale maandamano kile kilikuwa kipimo.
Tunamuomba Allah amsamehe makosa yake mja wake huyu na amtie Firdaws.
Amin.
View attachment 2305229
Hassan Chikusa
Luku...Sheikh,Mabucha yanayouza nguruwe sasa hivi iwe kavu o roast yapo au hakuna?
Myahudi...Utaendaje kuharibu biashara ya watu kisa nguruwe.
Kuna watu wanahitaji kuelimishwa, kwani hii ni nchi ya kiarabu
Kwa hiyo tuendelee kuishi kwa mpangilio wa kikoloni kwenye nchi huru?''Mji wa Dar es Salaam katika miaka ya 1920 ulikuwa umegawanyika katika sehemu nne: Kariakoo, Gerezani, Kisutu na Misheni Kota.
Sehemu ya ukazi wa asili ilikuwa Kisutu. Kisutu ina msikiti wa zamani kuliko yote katika Dar es Salaam - Msikiti wa Mwinyikheri Akida, unaokaribia takriban miaka mia moja hivi.
Vilembwe wa Sheikh Mwinyikheri hadi leo wangali wakiuhudumia msikiti wa mzee wao na msikiti huo bado uko chini ya uangalizi wao.
Kariakoo ilikuwa sehemu ya kuandikisha wapagazi wakati wa Vita Kuu Vya Kwanza.
Jina lenyewe ëKarikaooí linatokana na jina la Kizungu, ''Carrier Corps.''
Misheni Kota ilikuwa sehemu iliyotengwa makhsusi na Waingereza kwa ajili ya Wakristo.
Wakati ule Wakristo hawakuwa wengi Dar es Salaam, kwa ajili hii walitengewa sehemu yao maalum ya kuishi ili wasichanganyike na Waislam.
Misheni Kota ilikawa sehemu ya kuishi Wakristo kiasi ambacho hata mitaa yake ilipewa majina ya sehemu katika Tanganyika ambako Wamishionari walikuwa wamejipenyeza na kuweka maskani.
Majina ya mitaa kama Masasi, Likoma, Ndanda, Muhonda, Muheza na Magila imedumu hadi sasa.
Hizi ni sehemu ambazo Ukristo ulishamiri.
Misheni Kota ndiyo sehemu pekee katika Dar es Salaam ambapo Wamisionari walifanikiwa kujenga kanisa.
Wakristo walitengewa katika sehemu hii kuwa makazi yao.''
(Kutoka kitabu cha Abdul Sykes).
View attachment 2307398
Wewe mzee ipo siku lazima nikulishe kitimoto rost na ndizi mbili ili uache huu udini wako.Myahudi...
Ninaposoma kama hivi najifunza mengi na kukubali ukweli kuwa nyakati zimebadilika sana.
Wakati tunakua Dar es Salaam Wakristo walikuwa wakitaka kuchinja kuku wanampa Muislam kwa kuchelea kuwa Muislam asishindwe kula nyumba ya Mkristo.
Leo mtu anauliza kwani Tanzania ni nchi ya Kiarabu?
Mikutano ya TANU wakati wa kupigania uhuru ilikuwa ikifunguliwa kwa dua na msomaji alikuwa Sheikh Suleiman Takadir.
Dagii,Huyo polisi mstaafu ali ishia wapi?malizia story.
Ubarikiwe sana mzee wangu,vitu unavyo tupa hapa ni adimu kwakweliDagii,
Sina habari zake zaidi.
Hata mm nakubaliana na wewe swala la kuchinja kuku, tilikua tunawapa waislam wachinje ila kwakua umekubalina na mabadiliko basi tusonge mbele pamoja kwa amaniMyahudi...
Ninaposoma kama hivi najifunza mengi na kukubali ukweli kuwa nyakati zimebadilika sana.
Wakati tunakua Dar es Salaam Wakristo walikuwa wakitaka kuchinja kuku wanampa Muislam kwa kuchelea kuwa Muislam asishindwe kula nyumba ya Mkristo.
Leo mtu anauliza kwani Tanzania ni nchi ya Kiarabu?
Mikutano ya TANU wakati wa kupigania uhuru ilikuwa ikifunguliwa kwa dua na msomaji alikuwa Sheikh Suleiman Takadir.
Na mleta mada alikuwa smart. Hakuwa mstari wa mbele katika sakata hilo na hivyo akasalimika.Huyo Hassan Chikusa kwanini alihatarisha kazi yake kisa Mabucha ya kitimoto?
Amin.Ubarikiwe sana mzee wangu,vitu unavyo tupa hapa ni adimu kwakweli
Kuta...Na mleta mada alikuwa smart. Hakuwa mstari wa mbele katika sakata hilo na hivyo akasalimika.
Assnte. Tunaisubiri kwa hamu hiyo historia ili tuelewe vipi nchi yetu ilifikia pale ilipofika.Amin.
Kuta...
Haikuwa kuwa uwe mbele ndiyo ukamatwe.
Wala hakuna katika waliokamatwa ambao mimi nilikuja kuzungumzanao waliojuta kwa kukamatwa na kufungwa si katika sakata hili au la Mwembechai.
Kuna historia kubwa sana ambavyo yapaswa kufahamika kwa nini nchi ilifikia pale ilipofika.
BURIANI. KWA HAKIKA NI PIGO KUBWA KWA SISI TULIOMFAHAMU KUPITIA MITANDAO NA MAANDIKO YAKE JAPO KWA UCHACHE. NISEME ALIKUWA MTU MUUNGWANA ALIYEHESHIMU KILA MTU. PIA ALIIJUA HISTORIA NA MATUKIO MBALIMBALI YA NCHI HII VYEMA.BURIANI HASSAN CHIKUSA MSOMI MKIMYA
Naamini si wengi wanamfahamu Hassan Chikusa na yote yaliyomsibu katika maisha yake.
Mimi nilimjua Hassan Chikusa kwa kuwa alikua jirani yangu akiishi kwa ndugu yake Masaki jirani na nyumba niliyokuwa naishi mimi na familia yangu.
Wakati ule alikuwa kijana mdogo ndiyo kwanza amemaliza masomo yake na anafanya kazi Makao Makuu National Bank of Commerce (NBC), Sokoine Drive.
Tulizoeana sana na wakati mwingine akija nyumbani kwa mazungumzo na akipenda mazungumzo yangu katika vitabu, historia na muziki kama ilivyo kawaida ya vijana.
Hassan alikuwa akiweka shajara yaani akiandika, ''diary.''
Hassan alikuwa kijana akiipenda dini yake sana kwa mapenzi makubwa.
Mwaka wa 1993 pakawa na sakata la uvunjaji mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe Wilaya ya Kinondoni baada ya sala ya Ijumaa.
Kilichotokea ni kuwa kijana alitumwa nyama na muuza nyama pengine kwa kutokujua akamuuzia huyu kijana nyama ya nguruwe.
Palikuwa na malalamiko kuhusu haya mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe lakini walioshika madaraka hawakujali wala kutia maanani malalamiko ya Waislam.
Mjini Dar es Salaam kulikuwa na mabucha 29 ya kuuza nyama ya nguruwe kwenye sehemu wanazoishi Waislam na hii ilikuwa kinyume cha sheria.
Tatizo hili Waislam wakalifikisha kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mustafa Nyang;anyi lakini hakuna kilichofanyika na likafikishwa pia kwa Waziri Mkuu, John Samuel Malacela.
Waswahili wanamsemo wanasema yale yalikuwa sawa na kutwanga maji katika kinu.
Hili tatizo la mabucha likashushwa chini hadi kwa Mkuu wa Wilaya, Wilson Mkama na yeye akawaita ofisini kwake maimamu wa misikiti mitano ya Wilaya ya Kinondoni kwa mazungumzo.
Serikali haikuwa tayari kufunga mabucha hayo kwa kile walichokiona ni shinikizo kutoka kwa Waislam wenye, ''siasa kali.''
Bwana Mkama akawaeleza maimam kuwa hayo mabucha yapo kihalali na wana leseni walizopewa na serikali kufanya biashara hiyo kwa ajili hii serikali ina dhima ya kuzilinda hizo bucha.
Mkutano ukamalizika na maimamu wakarejea misikitini kwao kuwaeleza Waislam kauli ya serikali kuhusu mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe.
Waingereza wana msemo, ''The straw which broke the camel's back,'' yaani ujani uliowekwa juu ya mgongo wa ngamia ukauvunja.
Waislam walighadhibika sana kwa uamuzi wa serikali kuwapuuza.
Siku ya pili ilikuwa Ijumaa Kuu.
Baada ya sala ya Ijumaa vijana wa Kiislam walipomaliza sala waliziendea zile bucha zilizokuwa Wilaya ya Kinondoni wakazivunja zote kwa mpigo.
Dar es Salaam ilizizima.
Haya hayakupata kutokea katika kipindi chote cha uhuru.
Rais Ali Hassan Mwinyi akiwa Zanzibar akasema katika kulani kuvunjwa mabucha ya nguruwe kuwa nguvu za dola ziwaangukie wale waliovunja mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe.
Jioni yake BBC hwakuchelewa wakafanya mahojiano na Waziri Mkuu John Samuel Malecela.
Malecela akasema kuwa waliovunja mabucha ya kuuza nyama ya nguruwe ni wahuni wanotaka kuchukua serikali kupitia dini.
Waziri wa Mambo ya Ndani na Naibu Waziri Mkuu Augustine Mrema yeye akasema mabucha yamevunjwa kutokana na nguvu kutoka nchi ya Kiislam ili kuivuruga Tanzania.
Katibu Mkuu wa CCM Horace Kolimba yeye akahitimisha kwa kusema kuwa waliovunja mabucha si Waislam ila ni wahuni wanaotaka kupindua serikali.
Kufika asubuhi siku ya Jumamosi masheikh 40 wakawa wamekamatwa usiku wa manane kwa taadhira kubwa majumbani kwao mfano wa majambazi na kutiwa korokoroni.
Wahariri wa magazeti asubuhi yake siku ya Jumamosi wakawa katika burdani kubwa ya kuandika kuvunjwa kwa mabucha ya kuuza nguruwe na kukamatwa kwa masheikh.
Asubuhi ile ya Jumamosi kundi dogo la Waislam wakaenda Kituo Cha Kati cha Polisi kufuatilia masheikh waliokamatwa usiku na kuwekwa korokoroni hapo.
Hawa nao wakakamatwa na kuwekwa ndani.
Haukupita muda baada ya habari kuenea kuwa Waislam waliokwenda kuwauliza masheikh na wao wamekamatwa Waislam wakaja kwa wingi kituoni siku ya pili yake Jumapili iliyokuwa Easter Sunday.
Siku hiyo Waislam wakakusanyika pale kituoni ikawa kama vile kituo kimezingirwa na sala ya L'Asr ilipoingia ikapigwa adhana pale nje ya ya kituo watu wakasali barabarani.
Polisi wakataka kuwapiga mabomu ya machozi lakini pakawa na kutokubaliana baina ya askari wenyewe.
Hawakupendezewa na kitendo kile.
Askari Waislam wakawaambia wenzao hilo haliwezi kufanyika kuwapiga mabomu Waislam wanaosali kwani ni kufuru kubwa Waislam hawajafanya fujo wamekuja kituoni kufuatilia masheikh wao walioko korokoroni.
Jua lilipotua Waislam wakaondoka pale kituoni wakaamua wakutane siku ya pili Msikiti wa Mtoro washauriane.
Siku hii ya Jumapili yaani Easter Sunday mimi ndiyo niliingia Dar es Salaam nikitokea Le Havre, Ufaransa nikaja Paris kwa muda wa siku mbili kisha nikaenda London kisha Cardiff na kurejea London kupanda ndege kurudi Dar es Salaam.
Nilipofika nyumbani ndipo nilipopata taarifa ya masheikh kukamatwa na kati ya masheikh hao alikuwa mjomba wangu Sheikh Pazi wa Manzese.
Sikusubiri nikaenda kwa Hassan Chikusa wakati huo akiishi Mwananyamala kwani nilijua pamoja na kupita kwa jamaa wengine yeye ndiye ataweza kunipa taarifa ya mkasa mzima pamoja na tathmini.
Hayo niliyoandika hapo juu ni baadhi ya mambo aliyonifahamisha kuwa yametokea kuanzia siku ile ya Ijumaa yalipovunjwa mabucha hadi siku ya pii yake Jumamosi.
Hili ninalosema sasa ni jambo ambalo kwa miaka yote kila nilipokutana na Hassan moyo uliniuma sana nikiishia kumuombea dua.
Hassan siku ile nilipokwenda kwake ilikuwa Jumapili usiku na hakuwa na taarifa kuwa siku ya Jumatatu, yaani Easter Monday Waislam wameamua kufanya shura ndani ya Msikiti wa Mtoro ambao Imam Mkuu, Sheikh Kassim Juma alikuwa kakamatwa Arusha akielekea Nairobi kwenye matibabu na kurudishwa Dar es Salaam na yuko rumande.
Mimi ndiye nliyemfahamisha kuwa kesho Easter Monday kuna shura ya Waislam wote wa Dar es Salaam kujadili kwa pamoja nini kifanyike kurejesha heshima ya masheikh wetu.
Hassan aliniuliza kama mimi nitakuwepo.
Nikamwambia In Shaa Allah nitakuwapo.
Hassan Chikusa na yeye akaniambia atakuwapo pia.
Kwa ufupi siku ile ndani ya Msikti wa Sheikh Mtoro Mwinyi Mangara iliamriwa baada ya mjadala mkali sana Waislam watoke kwa maandamano hadi Kituo Cha Kati Cha Polisi kwenda kuwatoa masheikh wao korokoroni.
Katika maandamano yale Waislam walipambana na polisi na mabomu ya machozi yalipigwa.
Mapambano haya yalifanyika kati ya kituo cha polisi na Clock Tower.
Haya ndiyo yalikuwa maandamano ya kwanza ya Waislam Tanzania Bara.
Zanzibar maandamano yao yalikuwa mwaka wa 1988.
Maandamano haya yote tatizo ni Uislam.
Hassan Chikusa akakamatwa pamoja na vijana wengi wa Kiislam.
Wakawekwa rumande wakashtakiwa na kuhukumiwa vifungo jela.
Hassan Chikusa akapoteza kazi yake NBC.
Huyu ndiye Hassan Chikusa msomi mkimya ambae baada ya kutoka jela akiwa hana kazi masahibu mengi ya maisha yalimfika.
Lakini siku zote akisema yaliyomfika ni madogo sana na yote ameyakadiria Allah na na yeye bado yu hai.
Kwangu mimi maadamano yale na wale walioshiriki katika yale maandamano kile kilikuwa kipimo.
Tunamuomba Allah amsamehe makosa yake mja wake huyu na amtie Firdaws.
Amin.
View attachment 2305229
Hassan Chikusa