Bungeni: Wabunge wadai Kauli ya Prof Mkenda haina Uhalisia, mwenyewe akana kauli hiyo

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,031
1,648
Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii imewasilisha taarifa yake kuhusu mahojiano iliyofanya na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) baada ya Waziri Wa Elimu, Prof. Adolf Mkenda, Novemba 2, 2022, kudai Bungeni kuwa Bodi hiyo inamkwamisha

Akiwasilisha taarifa hiyo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati, Mbunge wa Singida Mjini (CCM), Mussa Sima amesema kikubwa walichobaini ni mawasiliano hafifu kati ya Wizara ya Elimu na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu

Akichangia ndani ya Bunge, Profesa Mkenda amekanusha hajawahi kulalamika ndani ya Bunge kwa kuwa anaimudu kamati hiyo, pia hajawahi kusema kama bodi inamkwamisha, kauli ambayo iliwaibua baadhi ya Wabunge kumuombea mwongozo kwa madai alitoa kauli hiyo na ndiyo sababu ya Spika kuteua Moja ya Kamati ikapate uhakika


Chanzo: Mwananchi
 
Kamati ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii imewasilisha taarifa yake kuhusu mahojiano iliyofanya na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) baada ya Waziri Wa Elimu, Prof. Adolf Mkenda, Novemba 2, 2022, kudai Bungeni kuwa Bodi hiyo inamkwamisha

Akiwasilisha taarifa hiyo kwa niaba ya Mwenyekiti wa Kamati, Mbunge wa Singida Mjini (CCM), Mussa Sima amesema kikubwa walichobaini ni mawasiliano hafifu kati ya Wizara ya Elimu na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu

Akichangia ndani ya Bunge, Profesa Mkenda amekanusha hajawahi kulalamika ndani ya Bunge kwa kuwa anaimudu kamati hiyo, pia hajawahi kusema kama bodi inamkwamisha, kauli ambayo iliwaibua baadhi ya Wabunge kumuombea mwongozo kwa madai alitoa kauli hiyo na ndiyo sababu ya Spika kuteua Moja ya Kamati ikapate uhakika


Chanzo: Mwananchi
Tatizo la viongozi wengi wenye shahada za uzamivu huwa hawajiandai vyema pale wapotakiwa kujibu maswali ama kuwasilisha ujumbe fulani kwa walengwa fulani. Tabia hii mbaya inatokana na uzoefu wao kitaaluma wakiwa wahadhiri katika kuwafundisha wanafunzi wa vyuo.

Jumuia ya wasomi hawa huamini wao ndiyo wenye ujuzi wa kujua mambo, na watu wengine hawajui vitu kwa kina. Wakati mwingine hutoa majibu "perfunctorily" ili kitimiza tu wajibu. Wao wanaamini ukishajibu kwa kutamka tu TRAB na TRAT, basi umefunga mjadala na kuwaziba midomo watu wengine vimbelembele wasiokuwa na uelewa wa mambo kama wao.
 
Back
Top Bottom