Bungeni leo: Martha Mlata; Kanumba alitakiwa awe na Bodigadi na hakustaili kuishi Sinza

Mbunge huyu alipokuwa anachangia hoja kuhusiana na sheria juu ya haki za wasanii na kazi zao. Alsema maeneo aliyokuwa anaish marehemu kanumba ni uswahilin hatari kwa Jk pamoja na Pm na wengneo.

Aidha aliongeza kuwa msanii huyo alpaswa kua na bodgad wa kumlnda.

Kwa hiyo Tanzania siku hizi wabunge wanasema tuna raia wa daraja moja na wengine wa madaraja mengine?

Kwa nini Kanumba hastahili kukaa Sinza? Kuna watumishi wa umma wastaafu waliofanya kazi Ikulu ya Nyerere wamejenga na wanakaa Sinza, Kanumba ni muhimu kuliko hawa?
 
Mzee Morris Nyunynusa hakustahili kukaa Buguruni na Dr. Remmy pia hakustahili kakaa Sinza! Pia Mzee Kipara na YombaYomba hawakustahili kufa maskini!
 
mmh,jamani kwani rais au pm wapo kwa kuwatembelea watu wanaoishi masaki peke yao? Basi kama hvyo tunaoishi kwa mtogole sisi sio binadamu wa kukutana na rais..ikumbukwe rais,pm hata huyowapo hapo kwaajili ya wananchi wote na si kwaajili ya watu wa masaki au watu wenye hadhi fulani.martha anapaswa kujua kwamba kanumba japokuwa alikuwa na fans wengi na maarufu sana lakini alijaribu kujishusha na kuishi na jamii ya kawaida sana hakuangalia usupastaa wake,hii inaonesha kwa kiasi gani wabunge wetu wanavyopenda kuishi masaki,oysterbay n.k badala ya kuishi karibu na wananchi waliowachagua huko uswahilini..kumbe mnaogopa hadhi zenu zitashuks.?.mwanmke mwenzetu kateleza kiukweli...
 
Huyu Mbunge sijawahi kumsikia akiongea la maana, Ona leo tena ameropoka..

Kuna uhusiano gani kati ya kifo cha kanumba na kuishi uswahilini na kutokuwa na Bodigadi?
Ina maana yeye aligombea ubunge ili ajiwezeshe na asiishi uswahilini?
Je hawa wengine wanaoishi uswahilini hawana haki ya kuishi pengine?
Kwamba Kanumba alitakiwa asiishi uswahilini na awe na Bodigadi, kwa hiyo nini kifanyike?
kwamba tumfufue ili tumuondoe uswahilini kisha tumpatie mabodigadi? Halafu?

Hiki Kibibi sijui niaje aisee!! Yaani hapa kina entertain matabaka wazi wazi!!
Danm!!!

Magamba in action.....elimu anayo kweli?
 
Umesikia mchango wake wote aliochangia
unajua alikuwa anamaanisha nini kusema alichosema?

Na kama mwanamke unaweza kuelewa ugumu na changamoto wanazopitia mpaka wanafika hapo bungeni,na kiukweli hamna pumba yoyote aliyeongea Martha Mlata na mbona hata Sugu ameongea mambo ambayo
almost yanafanana mbona yeye mnaona yuko sahihi?

mamii

kujua alikuwa anongea nini ni jambo jingine na uwasilishwaji wa alichokuwa anamaanisha ni kitu kingine pia.
kwangu mimi hata mwanamume akiongea pumba sitasita kumsema endapo nitaona anakosea,
sugu nae si wale wale tu, hapa jambo la msingi ni umuhimu wa matumizi ya kauli tulitoazo tukiwa katika umati au vikundi vikubwa vya watu hata kama uliona amemaanisha vizuri hoja yake aliiwasilisha vibaya na haya ni makosa wafanyayo watu wengi. sipendi kupendelea bila sababu za msingi uzi huu ungekuwa unamuhusu sugu pia ningesema.
mwanamke aliye imara hukubali changamoto anazokutana nazo katika kutimiza ndoto zake ikiwa unasema changamoto zile zingine hayo ni yakujitakia.
kama ni changamoto za kawaida basi sote tujue hakuna kitu rahisi success does not come easy.
sasa kwa sababu kapitia changamoto ndio tumtetee hata kama anaongea pumba?
sote tumepitia changamoto mbalimbali kufika hapa tulipofika.
let us avoid pity and emotional judgement. let us be strong everyday and accept challenges and critics.
 
sijui inakuwaje mbunge mzima anaamua asichambe kinywa!

viti maalumu magamba kweli hili nalo zuzu kanumba anakampuni kwa nini hakuajiri mabody guard wake km alikuwa anahitaji hilo,kwa hiyo tutumie hela za walipa kodi kuwalipia wasanii mabody guard siyo hana point kabisa na je watu wa sinza hawahitaji usalama kweli mazuzu wako wengi lkn eti sisi tulolome yeye keshaingiza allowance ya tsh 200000 kwa upuuzi aliozungumza nawasilisha
 
Mbunge huyu alipokuwa anachangia hoja kuhusiana na sheria juu ya haki za wasanii na kazi zao. Alsema maeneo aliyokuwa anaish marehemu kanumba ni uswahilin hatari kwa Jk pamoja na Pm na wengneo.

Aidha aliongeza kuwa msanii huyo alpaswa kua na bodgad wa kumlnda.

Yaaani, ina maana mpaka mtu afe ndo umuhimu au mchango wake uonekane na hawa wanasiasa uchwara pamoja na serikali yao?! Huu sio unafiki tu bali ni uhuni na uzandiki mkubwa!
 
mmh,jamani kwani rais au pm wapo kwa kuwatembelea watu wanaoishi masaki peke yao? Basi kama hvyo tunaoishi kwa mtogole sisi sio binadamu wa kukutana na rais..ikumbukwe rais,pm hata huyowapo hapo kwaajili ya wananchi wote na si kwaajili ya watu wa masaki au watu wenye hadhi fulani.martha anapaswa kujua kwamba kanumba japokuwa alikuwa na fans wengi na maarufu sana lakini alijaribu kujishusha na kuishi na jamii ya kawaida sana hakuangalia usupastaa wake,hii inaonesha kwa kiasi gani wabunge wetu wanavyopenda kuishi masaki,oysterbay n.k badala ya kuishi karibu na wananchi waliowachagua huko uswahilini..kumbe mnaogopa hadhi zenu zitashuks.?.mwanmke mwenzetu kateleza

...

Big up.
 
Mbunge huyu alipokuwa anachangia hoja kuhusiana na sheria juu ya haki za wasanii na kazi zao. Alsema maeneo aliyokuwa anaish marehemu kanumba ni uswahilin hatari kwa Jk pamoja na Pm na wengneo.

Aidha aliongeza kuwa msanii huyo alpaswa kua na bodgad wa kumlnda.

Hawa ndio wabunge wetu. Wameanza hivyo basi muda si mrefu watataka nao wawe na walinzi kwa gharama za serikali.
 
Back
Top Bottom