Bungeni Leo: Juni 29, 2012

Bungeni Leo: Juni 29, 2012

Naona viti vingi vipo wazi...inaniuma sana kutowaona tulikowatuma...!afadhari angekua mmoja..ila duh mpaka haibu..bora tulivunje tu bunge lenyewe..tunawapa bure tu kodi zetu...!
Namuona Mh Pinda...sioni kama anatoa majibu...!
"Vox populi,Vox dei"

Sioni umuhimu wa bunge kukaa miezi yote wakati ukiangalia viti vipo wazi na hata kama watajaa wabunge wengi watalalamika kwa 70% kuhusu budget kutokidhi haja lakini kisha anamalizia anaunga mkono hoja kwa 100%. Kama utaratibu ni huu kuna haja gani ya kukaa muda wote huu, mawaziri wanasoma budget mwisho hoja inaungwa mkono kwa asilimia mia (inakuwa kama mchezo wa kuigiza)
 
Halafu kwenye mambo ya anasa za wabunge huwa hakuna upinzani bungeni,wote wanakuwa chama kimoja.Kwaweli nguvu ya hoja ya ziada inahitajika kunishawishi nirudishe imani na Siasa uchwara ya bongo.

SWALI:Samahani mkuu,hao wabunge 357 nadhani 102 ni viti maalum ambao hawana majimbo so sidhani kama hao wafanyakazi wa4 wanawahusu wao lakini bahati mbaya sikusikiliza bunge leo wamesema hadi viti maalumu(a.k.a wapiga vigeregere) wanapewa wasaidizi wa4?

Alichotamka ni kwamba mbunge ni taasisi kama vile mkuu wa wilaya hivyo anahitaji wasaidizi wanne tena akanichosha alivyosema wanaajiriwa kwa matakwa ya mbunge hapo ndio nikachoka kabisa. Kwa kauli hiyo hata viti maalumu ukute akawekewa wasaidizi wake
 
Ni kweli kabisa.

Hivi ni wapi kunaweza kupatikana idadi ya wabunge wanaohudhuria kikaoa ikawekwa wazi magazetini walau tukaanzia hapo. Ikiwa hivyo watashtuka na kuikwepa hii absence kwa execuuse mbalimbali.

Hiyo itakuwa safi maana tutapata ushahidi wa michango yao bungeni maana hata kuwepo bungeni bila kuchangia nao ni ushiriki maana unaonyesha upo interested na kile kinachojadiliwa
 
Alichotamka ni kwamba mbunge ni taasisi kama vile mkuu wa wilaya hivyo anahitaji wasaidizi wanne tena akanichosha alivyosema wanaajiriwa kwa matakwa ya mbunge hapo ndio nikachoka kabisa. Kwa kauli hiyo hata viti maalumu ukute akawekewa wasaidizi wake

Dah!Haya bana,halafu tunajiita nchi masikini.
 
Aliyeiloga nchi hii alishughulika na uwezo wwetu wa kupanga matumizi. Na nadhani hii nchi haitakiwi kuwa na pato kubwa maaana pato likiongezeka tutaona vituko zaidi. Mfano tujaliwe mafuta, mamaa! naota kuwa kata zote nchini zitakuwa majimbo ya uchaguzi, tarafa zote zitakuwa mikoa, kila jimbo la uchaguzi litatoa wabunge wawili wawili mwanake na mwamme ili kuleta uwiano wa jinsia,baraza la mawazili lita kuwa na mawaziri miamoja, tutajenga majumba ya bunge kila kanda ili kuleta usawa kwa kuendesha vikao vya bunge mara moja kila kanda hapa tutaambiwa tunakuza utaifa na umoja wetu. Heli tubaki tulivyo maaana vitu vya maaana havitafanyika tuwe au tusiwe na hela.
 
Wasaidizi wenyewe ni hawa:

  1. Dereva
  2. Mpiga chapa
  3. Karani
  4. Mhudumu wa ofisi

wakuu naomba kuuliza, hivi mpiga chapa na karani wana tofauti gani ktk majukumu yao? serikali inadaiwa pesa nyingi sana na mifuko ya pensheni nssf wakiongoza kwa kukopwa pesa kugharamia miradi yake eg jengo hilo wanalojambia, udom etc. leo unaongeza na mradi wa ofisi za kina maji marefu na lusinde. nimeamini hii nchi inathamini wanasiasa kuliko maendeleo ya wananchi. mfyuuuu. your days are numbered. mene mene tekeli na peresi.
 
Msingi wa Umasikini waTanzania upo katika kuyapa kipaumbele mambo yasiyo na umuhimu kwa wakati husika.
Kwa sasa tunahitaji wazalishaji wa moja kwa moja ili tuwe na maendeleo ya haraka na wala siyo walaji.
Migogoro mingi inayojitokeza kwa sasa inasababishwa na kuboresha maslahi ya wanasiasa zaidi kuliko wafanyakazi wataalam wanaotoa huduma na kuzalisha mali katika taifa hili.
Ni muhimu ifahamike kwamba kuongeza ofisi za kisiasa ni kuongeza matumizi (walaji).
Bunge lenyewe limekosa tija na hivyo uwepo wa wabunge walio wengi ni mzigo tu kwa taifa, bora tuwe na bunge lenye wabunge 50 wenye ubora kuliko sasa hivi zaidi ya 60% ni wababaishaji wasiojua taifa linahitaji nini.
 
Back
Top Bottom