Bunge, TRA wote Wezi. Angalia Tunavyoibiwa

Bunge, TRA wote Wezi. Angalia Tunavyoibiwa

Muke Ya Muzungu

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2009
Posts
3,444
Reaction score
265
Bunge ilipitisha kwamba wale wote wanaorenew road licence lazima walipie huduma ya moto. Hapo mwanzoni hii huduma ya moto ilikuwa Tsh 3,000/ leo hii hiyo huduma imepanda kuanzia Tsh 40,000/ kwenda juu.

Sasa hii huduma ya moto iliyopitishwa na bunge ni la nini wakati hatuna hata zima moto moja kwenye maeneo nyeti kama airport. huu mrani ni wa nani na kwa nini. TRA inatumaliza na kodi zinazowanufaisha mafisadi.

Bunge mko wapi?
 
Mpaka tutakapokubali kuwaheshimu wanaojitolea kutuelimisha na kuacha kuwakejeli kwa majina ya ajabu!

Leo hii bila ule mwamko ulioanzishwa Mwembeyanga na yule mzee wetu huenda haya mambo yangekuwa funika kombe mwanarahamu apite!! Kuna watu bado wanaona ni kazi ndogo kuwataja watu hatari!

Saizi wananchi wanaelewa, na siku za huu mfumo au genge la wezi zinahesabika!
 

inaonekana hii haikusumbui kichwa. pengine ndugu zako inawaumiza. Kwa nini tulipie kitu ambacho hakipo? umeshaona zima moto wanaliokoa gari linaloteketea? Watakuja eneo la tukio wakakwambia hawana maji kwa hiyo wanaomba hela ya mafuta wakati gari limeshaungua
 
Subiri zamu yako, hajasikia kutesa kwa zamu? tulia tu mkuu
 
Tupo kimya tu ! kweli watanzania tuna moyo watakuja kutuambia wake zetu walale magogoni kwa ajiliya usafi bado tuta kaa kimya tu sasa kutoka elfu tano mpaka elfu arobaini wapi na wapi !
 
Bunge ilipitisha kwamba wale wote wanaorenew road licence lazima walipie huduma ya moto. Hapo mwanzoni hii huduma ya moto ilikuwa Tsh 3,000/ leo hii hiyo huduma imepanda kuanzia Tsh 40,000/ kwenda juu.

Sasa hii huduma ya moto iliyopitishwa na bunge ni la nini wakati hatuna hata zima moto moja kwenye maeneo nyeti kama airport. huu mrani ni wa nani na kwa nini. TRA inatumaliza na kodi zinazowanufaisha mafisadi.

Bunge mko wapi?

Bunge lenyewe si linaendeshwa na kodi kama hizo?
wewe ungeweza kuamini kwamba wabunge wenye akili wangeweza kupitisha sheria ya kuleta magari ya miaka chini ya 8?
Umeshawahi kuyaona magari ya kutoka japan ya 2000?
Ni bora kuliko magari ya serikali.
wabunge hawa hawa si walipitisha sheri hiyo bila kutafakari?
Sasa unashangaa nini kipya?
 
Tupo kimya tu ! kweli watanzania tuna moyo watakuja kutuambia wake zetu walale magogoni kwa ajiliya usafi bado tuta kaa kimya tu sasa kutoka elfu tano mpaka elfu arobaini wapi na wapi !

Niliwahi kusema siku moja watakuja na sera za kubinafsisha wake zetu. Bado kidogo kila mtoto atakapozaliwa lazima ulipe kodi! Am waiting for more taxes to come. Ukiishi zaidi ya miaka 50 tunakulima kodi. Yes!
 
Inapokwenda sasa kila huduma ya Jamii tutaichangia kivyake. Utakuja kusikia huduma ya askari wa doria inakatwa kwa Mwenyekti wa serikali za mitaa mara huduma ya maji kwenye bili za maji, huduma ya umeme kwenye umeme yaani sasa hivi bongo na bunge lake kila kitu ni dili tuu. K.
 
Inapokwenda sasa kila huduma ya Jamii tutaichangia kivyake. Utakuja kusikia huduma ya askari wa doria inakatwa kwa Mwenyekti wa serikali za mitaa mara huduma ya maji kwenye bili za maji, huduma ya umeme kwenye umeme yaani sasa hivi bongo na bunge lake kila kitu ni dili tuu. K.

Tangia hapo huduma za jamii zinatakiwa kuchangiwa na wananchi.

Kama wananchi hawachangii huduma za jamii kwa kiasi chao unategema huduma hizi zijiendesheje? Kwa bakuli la kufadhiliwa na wahisani?

Tatizo langu si kwamba wananchi wanachangishwa kuchangia huduma za jamii.

Tatizo langu ni kwamba, hata baada ya wananchi kuchangishwa huduma za jamii, huduma za jamii hazipati michango hiyo ya wananchi.

Wewe angalia barabara crucial kama ya Mandela, Dar-es-salaam wanapokaa wajanja na viongozi wao.

Haina hata taa!

Na kodi watu wanalipa.
 
hili swala linakera nadhani kuna bahadhi ya vitu bunge linapitisha alivijui, tofauti ya asilumia 1500,na wabunge wanapitisha sasa hawa wanaojiita upinzani na wanaojiita chama tawala wote lao moja tuu, kupigia kelele nani kala nani kala bila kujali wanapitisha kitu cha kwenda kuwaumiza wananchi walio wengi. WABUNGE WOTE HAKUNA KITU.
 
Yaani hii imeongezwa kwa 1,500% This is Crazy!
Insane... Mungu Wangu. hivi hili bunge wanaelewa kweli wanachokifanya

Tumekwisha. Wabunge Wetu vihiyo kweli kweli.
 
Bunge ilipitisha kwamba wale wote wanaorenew road licence lazima walipie huduma ya moto. Hapo mwanzoni hii huduma ya moto ilikuwa Tsh 3,000/ leo hii hiyo huduma imepanda kuanzia Tsh 40,000/ kwenda juu.

Sasa hii huduma ya moto iliyopitishwa na bunge ni la nini wakati hatuna hata zima moto moja kwenye maeneo nyeti kama airport. huu mrani ni wa nani na kwa nini. TRA inatumaliza na kodi zinazowanufaisha mafisadi.

Bunge mko wapi?

Mhhh!ngoja nipite kwanza,nchi kama haina vichwa!
 
Kuna haja ya kuangalia upya swala la kodi kwani kama serikali inaanzisha wakala wa kukusanya mapato na kutoa huduma, basi kodi zinazolipwa serikalini zipungue kwa kiwango kinachowiana na makusanyo ya wakala hizo.
Kuanzishwa kwa wakala nyingi za kukusanya mapato bila kutoa huduma ni wizi na uovu dhidi ya raia.
Kazi ya zimamoto siyo kukusanya mapato bali kutoa huduma ya kuzima moto.
Hata hivyo wananchi wanatakiwa kuangalia upya watunga sera na sheria ambao kwa hali ilivyo mambo yakiendelea hivi wanatakiwa kutangazwa maadui namba moja wa wananchi!
Hali hii haikubaliki na haitakiwi iachwe iendelee!
 
Hii nchi ni ya wajanya watapata wapi pesa za kuweka uswiswi
 
Back
Top Bottom