Kwa tanzania yetu mzigo namba moja unaotunyima maendeleo ni bunge letu. Bunge ndio chombo cha kusimamia na kushauri serikali lakini chombo hiki hakitambui wajibu na mamlaka yake.
Malaka ya bunge juu ya serikali ni sawa na jinsi bodi ya kampuni inavyosimamia utendaji wa kampuni au unavyoweza kuwa unajenga nyumba yako ukamtafuta mtaalamu kusimamia na kumshauri mkandarasi "contractor" kukujengea nyumba yako.kitakuwa ni kituko umemuweka mtaalamu asimamie na kushauri ujenzi wa nyumba yako ukute anamwambia mjenzi kuwa "mimi mweshimiwa injinia nilikuwa nafikiri hapa ukuta mngeunyoosha na simenti msiweke mchanga mwingi lakini mimi naunga mkono ujenzi wenu mia kwa mia"msimamizi sahihi ambaye siyo mzigo wa ujenzi ya nyumba yako kwanza anamuomba mjenzi ampe aina ya vifaa anavyotaka kuvitumia ili aangalie ubora na kutoa ruhusa, wakati wa ujenzi akikuta ukuta umepinda kidogo anamwambia mjenzi bomoa ujenge ulionyooka, sementi kidogo mchanga mwingi anasema hiyo mwaga lazima uweke uwiano unaokubalika.
Bunge letu linaendeshwa kama debate za sekondari "upande unaopinga na upande unaosapoti mada", bado hawajui wanachokifanya maana maana ya bunge haijulikani maana si wawakilishi wa wananchi kusimamia serikali bali limegeuka uwanja wa mabishano wa vyama vya siasa.kama tunataka maendeleo kila mbunge chama chake kibaki mlangoni wabunge wote wanakuwa kambi moja na serikali inayohojiwa kambi nyingine lakini mkubwa pale ni bunge "hapa lijitambue kuwa lina wajibu wa kurekebisha upuuzi wa serikali"mfano kuna tabia ya mawaziri kupeleka fedha za maendeleo katika maeneo kwa upendeleo hasa majimbo yao, kwa mfumo holela tulionao kila atakayeingia atafanya hivyo. Bunge ndio chombo cha kwanza kuondoa upuuzi huu kwa kutumia njia kama hii.
Kwanza mnaagiza serikali kuweka malengo ya kitaifa ya maendeleo kama kufikia mwaka fulani tunataka huduma ya maji mijini kufikia asilimia fulani na vijini kufikia asilimia fulani.sasa takwimu za taifa zima kuangalia kila wilaya imefikia asilimia ngapi ya utekelezaji wa mpango huo wa taifa, vinaaandaliwa vigezo vya utekelezaji mfano kipaumbele kinawekwa kwa wilaya ambazo bado ziko chini na miradi ya kuchochea uchumi kitaifa. Waziri anapoleta bajeti yake ni kuangalia kama yuko katika kutekeleza mpango wa maendeleo wa taifa na fedha anazigawa kwa vigezo.ni upuuzi mtupu kuona mbunge anasiamama na kudai kama kujiji fulani hakitegewi fungu anatoa shilingi wakati huo pengine wilaya yake imevuka lengo na sehemu ambayo wako chini kabisa ya malengo tena hawapewi nafasi kuchangia katika hiyo mada.
Ili kusimamia serikali lazima bunge liwe na sauti moja ya wananchi na sio vyama vya siasa na liwe na kauli moja ya kuwa na nini waziri anatakiwa kufanya na kumpima kwa mapendekezo aliyoyaleta na yale aliyotakiwa kufanya sio kila mmoja huyu anatokea kilabuni, huyu anatokea kwenye biashara zake huyu anatokea sijui wapi wanakutana kujadili hoja za serikali kila mmoja anasema yake na mwisho hawana maamuzi.ni wapumbavu tu wanaoweza kusoma majukumu ya bunge kuwa ni kushauri wakaenda bungeni kusimama na kusema wanayofikiri kuwa kama wabunge wametimiza wajibu wao.
Wajibu wa mbunge si kusema anayowaza na kuyahalalisha kwa kutanguliza wananchi wangu wamenituma, bali lazima kuwe na mfumo rasimi wa kitakwimu kuonyesha mwenendo wa maisha ya watanzania na serikali inapanga nini na kutekeleza nini kuhusu maisha haya ya watanzania.hivyo kwa mbunge mambo muhimu ni takwimu za hali maisha ya watanzania, mipango ya maendeleo ya kitaifa, mipango ya mapato na matumizi, utekeleza wa mipango. Na mbunge anapokaa bungeni ni kujadili mambo ya kitaifa kwa maana ya kwamba unakuja na hali iliyoko jimboni kwako, zinalinganishwa na takwimu za kitaifa na hivyo utekelezaji wa serikali lazima ufuate malengo ya kitaifa na hali halisi.serikali inapokuja bungeni lazima kila waziri aambatane na watu muhimu katika wizara yake kila mmoja anajibu maswali katika eneo lake.
Haiwezekani bandarini kuna tatizo waziri hajui chochote yeye ndiye anakaa kujibu maswali hata mambo ya kweli anapinga kujilinda kwa nini mkurugenzi wa bandari asiwe pale na kama anamawazo bora ambayo waziri amekuwa hayapi kipaumbele kwa sababu mkurugenzi hajipendekezi kwake bunge linayapitisha pale pale na kama anamakosa ambayo yanaonekana hayamgusi sana waziri bunge linaagiza awajibishwe.
Malaka ya bunge juu ya serikali ni sawa na jinsi bodi ya kampuni inavyosimamia utendaji wa kampuni au unavyoweza kuwa unajenga nyumba yako ukamtafuta mtaalamu kusimamia na kumshauri mkandarasi "contractor" kukujengea nyumba yako.kitakuwa ni kituko umemuweka mtaalamu asimamie na kushauri ujenzi wa nyumba yako ukute anamwambia mjenzi kuwa "mimi mweshimiwa injinia nilikuwa nafikiri hapa ukuta mngeunyoosha na simenti msiweke mchanga mwingi lakini mimi naunga mkono ujenzi wenu mia kwa mia"msimamizi sahihi ambaye siyo mzigo wa ujenzi ya nyumba yako kwanza anamuomba mjenzi ampe aina ya vifaa anavyotaka kuvitumia ili aangalie ubora na kutoa ruhusa, wakati wa ujenzi akikuta ukuta umepinda kidogo anamwambia mjenzi bomoa ujenge ulionyooka, sementi kidogo mchanga mwingi anasema hiyo mwaga lazima uweke uwiano unaokubalika.
Bunge letu linaendeshwa kama debate za sekondari "upande unaopinga na upande unaosapoti mada", bado hawajui wanachokifanya maana maana ya bunge haijulikani maana si wawakilishi wa wananchi kusimamia serikali bali limegeuka uwanja wa mabishano wa vyama vya siasa.kama tunataka maendeleo kila mbunge chama chake kibaki mlangoni wabunge wote wanakuwa kambi moja na serikali inayohojiwa kambi nyingine lakini mkubwa pale ni bunge "hapa lijitambue kuwa lina wajibu wa kurekebisha upuuzi wa serikali"mfano kuna tabia ya mawaziri kupeleka fedha za maendeleo katika maeneo kwa upendeleo hasa majimbo yao, kwa mfumo holela tulionao kila atakayeingia atafanya hivyo. Bunge ndio chombo cha kwanza kuondoa upuuzi huu kwa kutumia njia kama hii.
Kwanza mnaagiza serikali kuweka malengo ya kitaifa ya maendeleo kama kufikia mwaka fulani tunataka huduma ya maji mijini kufikia asilimia fulani na vijini kufikia asilimia fulani.sasa takwimu za taifa zima kuangalia kila wilaya imefikia asilimia ngapi ya utekelezaji wa mpango huo wa taifa, vinaaandaliwa vigezo vya utekelezaji mfano kipaumbele kinawekwa kwa wilaya ambazo bado ziko chini na miradi ya kuchochea uchumi kitaifa. Waziri anapoleta bajeti yake ni kuangalia kama yuko katika kutekeleza mpango wa maendeleo wa taifa na fedha anazigawa kwa vigezo.ni upuuzi mtupu kuona mbunge anasiamama na kudai kama kujiji fulani hakitegewi fungu anatoa shilingi wakati huo pengine wilaya yake imevuka lengo na sehemu ambayo wako chini kabisa ya malengo tena hawapewi nafasi kuchangia katika hiyo mada.
Ili kusimamia serikali lazima bunge liwe na sauti moja ya wananchi na sio vyama vya siasa na liwe na kauli moja ya kuwa na nini waziri anatakiwa kufanya na kumpima kwa mapendekezo aliyoyaleta na yale aliyotakiwa kufanya sio kila mmoja huyu anatokea kilabuni, huyu anatokea kwenye biashara zake huyu anatokea sijui wapi wanakutana kujadili hoja za serikali kila mmoja anasema yake na mwisho hawana maamuzi.ni wapumbavu tu wanaoweza kusoma majukumu ya bunge kuwa ni kushauri wakaenda bungeni kusimama na kusema wanayofikiri kuwa kama wabunge wametimiza wajibu wao.
Wajibu wa mbunge si kusema anayowaza na kuyahalalisha kwa kutanguliza wananchi wangu wamenituma, bali lazima kuwe na mfumo rasimi wa kitakwimu kuonyesha mwenendo wa maisha ya watanzania na serikali inapanga nini na kutekeleza nini kuhusu maisha haya ya watanzania.hivyo kwa mbunge mambo muhimu ni takwimu za hali maisha ya watanzania, mipango ya maendeleo ya kitaifa, mipango ya mapato na matumizi, utekeleza wa mipango. Na mbunge anapokaa bungeni ni kujadili mambo ya kitaifa kwa maana ya kwamba unakuja na hali iliyoko jimboni kwako, zinalinganishwa na takwimu za kitaifa na hivyo utekelezaji wa serikali lazima ufuate malengo ya kitaifa na hali halisi.serikali inapokuja bungeni lazima kila waziri aambatane na watu muhimu katika wizara yake kila mmoja anajibu maswali katika eneo lake.
Haiwezekani bandarini kuna tatizo waziri hajui chochote yeye ndiye anakaa kujibu maswali hata mambo ya kweli anapinga kujilinda kwa nini mkurugenzi wa bandari asiwe pale na kama anamawazo bora ambayo waziri amekuwa hayapi kipaumbele kwa sababu mkurugenzi hajipendekezi kwake bunge linayapitisha pale pale na kama anamakosa ambayo yanaonekana hayamgusi sana waziri bunge linaagiza awajibishwe.