Bunge live 'limeanza'!

Hata walio masikini hujikusanya mahali wakaona.
Tuwe wakweli, hao maskini unaowasema ndio wale wanaofuata drama za bungeni si lolote la maana. Katika awamu hii maskini wanatakiwa wafanye kazi kwa bidii ili wajikwamue kutoka kwenye umaskini wao.
 
Nimekupata vzr. Nimewajibu wenye mawazo kama yako wawaambie Azam TV et al wapeleke fedha zikanunue vitanda vya akina mama wajawazito wanaolala chini hospitalini!
 

Huu unafki tulionao watanzania utaisha lini? ?
 
Hatavmwanafunzi asiye na dawati na mama mjamzito anayelala chini hospitali naye ni HAKI YAKE kupata huduma kutoka kwenye hiyo Kodi unayozungumzia. Kupanga ni kuchagua!
 
Mara nyingi akili ya yange yange hupeperushwa na upepo,naona kama ID yako na akili yako vinashabihiana na huyo ndege
 
Unaona watz walivyowajinga wanataka kuibiwa hadi mchana kweupe. Kama magufuli mtoto wa kiume aache kuingilia bunge na aacha liee wazi. Huyu mtu sijui anayo akili zipi .
 
kumbe kule azam tv na star tv serikali ndo ilikuwa inalipia! basi hapa lazima wananchi masikini tanzania watakula milo kumi kwa siku maana ni matirioni ya pesa yatakuwa yameokolewa!
Kama yapo matrilioni ya kuokolewa itakuwa kheri maana kila mwanafunzi ataketi kwenye dawati, wagonjwa wote mahospitalini watapata dawa na kulala pazuri kama walikokuwa wakilala mahospitalini India, Afrika Kusini walikokuwa wakienda kutibiwa mafua hao Wabunge wenu mnaotaka sana kuwaona wanachofanya bungeni!
 
....

.....JF
 
Inaelekea mleta mada hajui nini umuhimu wa Bunge lenye uwajibikaji katika kutatua hizo changamoto za hao wananchi wa kawaida
Wawajibike na watatue. Ndiyo kazi yao kwani lazima tuwaone live bungeni. Twataka tuwaone live wakitatua matatizo majimboni.
 
kwa maoni yako bora ungesema kusiwe na TV yeyote kuonyesha vipindi wakati wa kazi maana kama ni suaka la kuangalia hata vipindi vingine watu watataka kuangalia
 
Mimi huwa nachoshwa sana na watu wa aina yako, hasa wanaojifanya wao wana weka maslai yao mbele wakidai ni wazalendo na wanampigania haki wale wananchi masikini, au wana weka kifua mbele wakidai ni wanaharakati za kumkomboa mlalahoi, Maskini hivi wewe unamtetea maskini yupi huyo anayetaka bunge live lisionyeshwe? Sijaelewa nini hasa dhamira yako kama ni kama GHARAMA serikali inajitwisha na wakati gharama za uendeshaji ni sehemu ya kodi yangu nayolipia tena nakatwa kodi kubwa sana hususani kwenye mshahara wangu PAYE bado nisipate huduma ya kupata habari kwenye tv station ya umma,

Pia Nina imani kubwa sana nchi yetu DEMOKRASIA imefika hapa kwa mchango wa BUNGE LIVE , hapo hapo uchaguzi wa mwaka jana ushindani ulikuwa ni mkubwa sana kwa kuwa wananchi wamekomaa kisiasa wanajua nani wa kumchagua na atoke chama gani kwa kuwa BUNGE LIVE limewakuza watu kisiasa kwa kuangali mijadala ya kisiasa , na kupitia BUNGE LIVE ile ni sehemu wabunge wanajituma kwa kuwa wana hofu jimboni kwake watu pale jimboni kwake wanamfutilia hasa kwa ahadi zake na je anawakilisha vipi mahitaji ya jimbo lake, pia BUNGE LIVE ni muhimu kwa kuwa wana uchumi, wawekezaji na wafanya biashara mbalimbali BUNGE LIVE kwao ni muhimu hasa kwa kipindi cha kuandaa bajeti mpaka inapo pitishwa kujuwa yapi ya kwenye bajeti yaliyo jadiliwa relating to the scope and nature ya uwekezaji wao,

Sasa wewe ndo unajiita mzalendo, mpigania haki za masikini, hivi masikini unaemtetea ni kwa namna ipi unamtetea wakati una una unga mkono bunge live lisionyeshwe wakati masikini huyo huyo hapati haki ya kupata habari aisehh wewe ni jipu na una uhitaji wa maombi, eti mimi ni masikini tu kweli acha uwe masikini tu kwa fikra hizi huwezi kupiga hatua, na utaendelea kuwa masikini hivyo hivyo kwa kuwa akili imeganda, jiongeze ati
 
Hivi wewe mtoa post ni kwamba kichwa ulipewa uvalie kofia tu au??? SHAME ON U.........hata kama unaandika pumba andika pumba itakayovutia hata mbururaz wenzako. This was too low for this forum.
 
Hivi mleta Mada unafahamu kwamba hata wale walioko nje ya Tanzania walikua wanategemea kuona Bunge live na kuelewa kinachojiri nyumbani kupitia hiyo Live?!

Why are you people so selfish mmekazana kutoa hoja nyepesi eti watu wako na kazi mida ya kuangalia Bunge?! Did you know that we could watch Bunge live as far as Johannesburg, Malawi, Botswana na hata Lusaka?! Even Pittsburgh watu walikua wanafuatilia live online jamani!!

Nashindwa kabisa kubaini upeo wa alietoa idea ya kusitisha kuonyesha Bunge live, I am very sure something is very wrong kwa ubongo wake ama his balls (it's a man i'M sure)!!
 
Afadhali mara mia ungeacha kuandika upuuzi huu. Kwani hiyo pesa inayookolea wanagawiwa hao maskini au wanagawana hao hao wanaoziokoa. Uliza chenji ya rada na ile EPA ilipo usikie majibu.

Kwani hao AZAM Tv waliozuiliwa wasionyeshe live kwa gharama yao mmepata faida gani?
Ama huko Kenya, Rwanda, Botswana, South Africa wanakoonyesha live wao hawafsnyi kazi mchana? Acheni kuwanyanyapaa wananchi kwa kisingizio cha umaskini wakati kila siku Magufuli anasema nchi yetu ni tajiri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…