Ni jambo la wazi kwa sasa kuwa bunge limekuwa ni tanuru la moto la kuchoma magamba ya CCM.
Kuanzia Spika(Makinda), Naibu spika(Ndugai), Katibu mkuu wa CCM(Kinana), Naibu katibu wa CCM(Mwigulu) hadi mwenyekiti wa CCM(Kikwete) na baraza lote la mawaziri, wote wamevuliwa nguo na kuingia aibu baada ya CHADEMA kuwaumbua watu hao ndani ya bunge la bajeti.
Kwa sasa hata TBC inapata wakati mgumu kurusha matangazo ya bunge 'live' kwani yamekuwa sumu ya kuia CCM kijamii na huku yakiipandisha Chati kisiasa CHADEMA.
Hapo kabla alipangwa kuwa bunge lisirushwe tena 'live' lakini kelele za wadau zikawafanya waogope na kusitisha mpango huo. Kwa sasa ni TBC pekee ndio wamepewa ruhusa ya kurusha matangazo ya bunge na wakati huo huo TBC inaonekana mikoa michache na kwa sasa haionekani kwa baadhi ya mikoa iliyokuwa inatumia Satelite kuona TBC. Na mara kadhaa TBC imekuwa akikata matangazo ya bunge pasipo sababu hususani pale CCM na washirika wake wanaporaruliwa.
Ni juzi tu, Naibu spika wa bunge, Job Ndugai amakaririwa akisema kuwa hatawagusa tena wabunge wa CHADEMA kwa kuwa kila akifanya hivyo wabunge hao wameonekana mashujaa mbele ya jamii na yeye kuambulia aibu kutoka kwa wananchi na jamii kwa ujumla.