mwembemdogo
JF-Expert Member
- Feb 28, 2016
- 2,282
- 1,252
Nimeshangazwa Na msimamo wa Bunge letu kuendelea kugomea vyombo vya habari Televisheni kurusha matangazo ya Bunge.
Wananchi ndio tuliowachagua hao wabunge Na ni sisi wananchi tunaotakiwa kujua wanafanya nini ndani ya Bunge. Kuzuia kurusha matangazo Spika anaficha nini ambacho anataka sisi tuliowapa dhamana tusikijue? Mbona Serikali hii inajinadi kuwa ni ya uwazi?Mbona Mawaziri wanadiriki mpaka kusafiri Na waandishi wa habari katika ziara zao ili wasikike iweje Bunge lizuie?
Tunaliomba Bunge liruhusu vituo vya Televisheni viruhusiwe kurusha shughuli za Bunge wakati wote wa Vikao.
Wananchi ndio tuliowachagua hao wabunge Na ni sisi wananchi tunaotakiwa kujua wanafanya nini ndani ya Bunge. Kuzuia kurusha matangazo Spika anaficha nini ambacho anataka sisi tuliowapa dhamana tusikijue? Mbona Serikali hii inajinadi kuwa ni ya uwazi?Mbona Mawaziri wanadiriki mpaka kusafiri Na waandishi wa habari katika ziara zao ili wasikike iweje Bunge lizuie?
Tunaliomba Bunge liruhusu vituo vya Televisheni viruhusiwe kurusha shughuli za Bunge wakati wote wa Vikao.